Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,202
- 218
Ndugu Wazalendo wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Nimesikitishwa sana na Tukio la Arusha , Ambapo Polisi wa Kutuliza Ghasia walitumia Nguvu Kujaribu kuwaondosha Wananchi wa Arusha waliokuwa Njiani kuelekea Uwanja wa NMC kwa ajili ya Mkutano Leo .
Baada ya hapo ni fujo zilizoenea maeneo kadhaa katika mji huo , mpaka ninapoandika Ujumbe hii inasemekana Dr Slaa na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema wamechukuliwa na askari hao wa kutuliza ghasia , Hapo kabla taarifa zilisema Ndugu Freeman Mbowe na Mama Slaa walikamatwa Na FFU .
Pamoja na hayo kumetokea Tukio la kurushiwa mawe kwa Jengo la Ofisi za CCM mkoani Arusha ambapo vioo Kadhaa vimepasuka , wapangaji kwenye jengo hilo walikimbia hivyo kujaribu kujiokoa kutokana na mawe hayo .
Kitendo hichi ni cha kupingwa kwa mfano na viongozi wetu wa dini pamoja na serikali pamoja na vyama vya kisiasa , Asasi za kiraia na Mashirika ya kutetea haki za Binadamu .
Tukio la leo limeiweka Nchi yetu Tanzania Haswa Arusha GENEVA ya Afrika katika Ramani nyingine ya dunia , Jinsi watu wanavyojadili tukio hili kwenye vyombo vya habari kuanzia radio mpaka mitandao na tovuti kadhaa za maoni Hatujui huko majumbani Habari hizi watazichukuliaje na hata hatujui kesho Tanzania itaamkaje .
Kwa tukio hili la mengine yaliyotokea katika kipindi cha miezi 2 iliyopita toka kumalizika kwa uchaguzi mkuu inaonyesha nchi yetu ina matatizo ya kutokuaminiana na ule mshikamano wa wananchi kwa wenyewe na viongozi wao unaonyesha kupungua kwa kiasi kikubwa sana .
Tunaomba viongozi wafanye liwezalo kukaa chini kumaliza Tofauti hizi na kutoa tamko la pamoja kumaliza matatizo yaliyopo sasa hivi nchini yanayohusiana na uchaguzi uliopita ili tuweze kuendelea mbele .
Mwaka huu nchi yetu inatimiza miaka 50 toka kupata uhuru Itasikisha sana kusheherekea miaka 50 ya uhuru kwa vurugu na uvunjivu wa amani unaoendelea nchini .
Jamani tuwe Wazalendo na kukaa mezani kwa majadiliano utumiaji wa nguvu kwa pande zote hauwezi kuwa suluhisho la kudumu , utumiaji wa nguvu mara nyingi unahusisha na visasi na utaacha vidonda ambavyo ni ngumu kuponyesha kwa kipindi kifupi .
NCHI YETU NI YETU SOTE TUKAE TUJADILIANE KUMALIZA TOFAUTI TUSONGE MBELE .
Nimesikitishwa sana na Tukio la Arusha , Ambapo Polisi wa Kutuliza Ghasia walitumia Nguvu Kujaribu kuwaondosha Wananchi wa Arusha waliokuwa Njiani kuelekea Uwanja wa NMC kwa ajili ya Mkutano Leo .
Baada ya hapo ni fujo zilizoenea maeneo kadhaa katika mji huo , mpaka ninapoandika Ujumbe hii inasemekana Dr Slaa na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema wamechukuliwa na askari hao wa kutuliza ghasia , Hapo kabla taarifa zilisema Ndugu Freeman Mbowe na Mama Slaa walikamatwa Na FFU .
Pamoja na hayo kumetokea Tukio la kurushiwa mawe kwa Jengo la Ofisi za CCM mkoani Arusha ambapo vioo Kadhaa vimepasuka , wapangaji kwenye jengo hilo walikimbia hivyo kujaribu kujiokoa kutokana na mawe hayo .
Kitendo hichi ni cha kupingwa kwa mfano na viongozi wetu wa dini pamoja na serikali pamoja na vyama vya kisiasa , Asasi za kiraia na Mashirika ya kutetea haki za Binadamu .
Tukio la leo limeiweka Nchi yetu Tanzania Haswa Arusha GENEVA ya Afrika katika Ramani nyingine ya dunia , Jinsi watu wanavyojadili tukio hili kwenye vyombo vya habari kuanzia radio mpaka mitandao na tovuti kadhaa za maoni Hatujui huko majumbani Habari hizi watazichukuliaje na hata hatujui kesho Tanzania itaamkaje .
Kwa tukio hili la mengine yaliyotokea katika kipindi cha miezi 2 iliyopita toka kumalizika kwa uchaguzi mkuu inaonyesha nchi yetu ina matatizo ya kutokuaminiana na ule mshikamano wa wananchi kwa wenyewe na viongozi wao unaonyesha kupungua kwa kiasi kikubwa sana .
Tunaomba viongozi wafanye liwezalo kukaa chini kumaliza Tofauti hizi na kutoa tamko la pamoja kumaliza matatizo yaliyopo sasa hivi nchini yanayohusiana na uchaguzi uliopita ili tuweze kuendelea mbele .
Mwaka huu nchi yetu inatimiza miaka 50 toka kupata uhuru Itasikisha sana kusheherekea miaka 50 ya uhuru kwa vurugu na uvunjivu wa amani unaoendelea nchini .
Jamani tuwe Wazalendo na kukaa mezani kwa majadiliano utumiaji wa nguvu kwa pande zote hauwezi kuwa suluhisho la kudumu , utumiaji wa nguvu mara nyingi unahusisha na visasi na utaacha vidonda ambavyo ni ngumu kuponyesha kwa kipindi kifupi .
NCHI YETU NI YETU SOTE TUKAE TUJADILIANE KUMALIZA TOFAUTI TUSONGE MBELE .