gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,274
- 20,673
Haya tena jamani leo nataka tujifunze namna ya kuandaa unga wa lishe hadi jinsi ya kuupika uji huu.
Ningeomba sana kanuni nitakayo itumia hapa basi kila mmoja airekebishe kulingana na jinsi anavyopenda yeye.
KANUNI ZA KUANDAA UNGA WA LISHE.
Vifaa
=ulezi kg 1
=mahindi yasiyokobolewa kg 1/2
=ngano isiyokobolewa kg 1/2
=karanga kavu ila mbichi 1/2
=soya isiyobanguliwa 1/2.
Njia ya kuandaa,
1) chukua ulezi wako upete vizuri kwenye ungo. kisha weka kwenye maji kuupembua. Hakiksha kwamba unaupembua mara nyingi zaid kwa kutumia maji masafi na chombo cha bati hadi mawe/mchanga uishe wote kabisa. Kumbuka kwamba ulezi huwa michanga sana.
hivyo matumizi ya vitu vya bati. chuma wakati wa kupembua hukufanya uweze kuona mawe vyema, pia mawe yasiteleze sana as yanakuwa kama yananatiana na chuma hivi. so muda wa kupembua kuwa mchache tofauti na ukitumia chombo cha plastic.
2)ukishahakikisha ulezi wako ni msafi basi tenga ungo wako kisha umimine ulezi na uanike juani ili ukauke kabisa.
3) peta mahindi yako vyema toa yote yaliyo mabovu, peta ngano yako toa punje zote zilizo mbovu kisha osha vizuri kwa maji ya kutosha na anika kwenye ungo wake tofauti.
4) peta na chagua soya, kisha chemsha soya zako jikoni kwa dk 10 zitokote, kisha anza kuzimenya maganda, ni rahisi as yanakuwa yanamenyeke kwa kuteleza hivyo ukifikicha mkononi tu yanatoka. baada ya kutoa maganda yote anika hizi soya kwenye ungo wake hakikisha zinapigwa jua sana sana zikauke kabisa ziwe kama vile hazijagusa maji kabisa.
5) zikisha kauka kabisa zitie kwenye sufuria na moto mdogo sana anza kuziaanga kama vile unakaanga karanga ama ziweke kwenye oven 60 degree kwa nusu saa. zikitoka kwenye moto ziweke sehem ya wazi ili zipoe bila kupeana unyevu.
6) chagua karanga zako vizuri, hakikihsa kila punje mbovu unaitoa (jamani naomba niseme wazi kila karanga mbovu itolewe) kisha zikaange kwa moto mdogo sana ziwe kavu kabisa lkn zisiungue. ama ziweke kwenye oven kwa 60 degree for 15-20 mints. ukishazikaanga zianike tena juani ili zipoe lkn zipoe bila kuabsorb moisture kabisa.
zikishakauka kabisa zidunde kama mbegu ya ubuyu basi zimenye maganda yote kisha upete halafu uchague zile punje nzuri tu ambazo hazina rangi ya njao ama hazina kutu.
7) hakikisha wamba nafaa zako hizi zimekauka sana na hakuna hata punje moja mbovu ndipo uziwee pamoja na kuazisaga mashine. hakikaisha pia unga unaposagwa unarudiwa mara ya pili ili uwe mlaini usiwe na chenga chenga.
8) baada ya kusaga anika unga wako mahali pakavu hadi upoe, na hakikaisha wakati wa kuanika hautachafua. kuwa safe zaid ni bora ukajitahd nyumban ukawa na kitambaa ambacho unakiweka juu ya ungo wako kisha unamimina unga wako, ukiuweka juani tafuta kitambaa kingine kilicho cha nyavu nyavu uweke kwa juu kufunika unga wako usifwatwe na wadudu ama kupata uchafu.
Ukisha kauka tafuta chombo kikavu uweke na ufunike vizuri kisiwe na sehem ya kupitasha wadudu.
nitarudi baadae kueleza namna ya kuupika uji huu. ila naamini maandalizi ya awali mtakuwa mmesha yapata vyema.
da AshaDii The secretary kumbukeni kwamba uji huu anaweza kulishwa mtoto wa kuanzia miezi 6.
Kwanini zinataiwa ziwe
Ningeomba sana kanuni nitakayo itumia hapa basi kila mmoja airekebishe kulingana na jinsi anavyopenda yeye.
KANUNI ZA KUANDAA UNGA WA LISHE.
Vifaa
=ulezi kg 1
=mahindi yasiyokobolewa kg 1/2
=ngano isiyokobolewa kg 1/2
=karanga kavu ila mbichi 1/2
=soya isiyobanguliwa 1/2.
Njia ya kuandaa,
1) chukua ulezi wako upete vizuri kwenye ungo. kisha weka kwenye maji kuupembua. Hakiksha kwamba unaupembua mara nyingi zaid kwa kutumia maji masafi na chombo cha bati hadi mawe/mchanga uishe wote kabisa. Kumbuka kwamba ulezi huwa michanga sana.
hivyo matumizi ya vitu vya bati. chuma wakati wa kupembua hukufanya uweze kuona mawe vyema, pia mawe yasiteleze sana as yanakuwa kama yananatiana na chuma hivi. so muda wa kupembua kuwa mchache tofauti na ukitumia chombo cha plastic.
2)ukishahakikisha ulezi wako ni msafi basi tenga ungo wako kisha umimine ulezi na uanike juani ili ukauke kabisa.
3) peta mahindi yako vyema toa yote yaliyo mabovu, peta ngano yako toa punje zote zilizo mbovu kisha osha vizuri kwa maji ya kutosha na anika kwenye ungo wake tofauti.
4) peta na chagua soya, kisha chemsha soya zako jikoni kwa dk 10 zitokote, kisha anza kuzimenya maganda, ni rahisi as yanakuwa yanamenyeke kwa kuteleza hivyo ukifikicha mkononi tu yanatoka. baada ya kutoa maganda yote anika hizi soya kwenye ungo wake hakikisha zinapigwa jua sana sana zikauke kabisa ziwe kama vile hazijagusa maji kabisa.
5) zikisha kauka kabisa zitie kwenye sufuria na moto mdogo sana anza kuziaanga kama vile unakaanga karanga ama ziweke kwenye oven 60 degree kwa nusu saa. zikitoka kwenye moto ziweke sehem ya wazi ili zipoe bila kupeana unyevu.
6) chagua karanga zako vizuri, hakikihsa kila punje mbovu unaitoa (jamani naomba niseme wazi kila karanga mbovu itolewe) kisha zikaange kwa moto mdogo sana ziwe kavu kabisa lkn zisiungue. ama ziweke kwenye oven kwa 60 degree for 15-20 mints. ukishazikaanga zianike tena juani ili zipoe lkn zipoe bila kuabsorb moisture kabisa.
zikishakauka kabisa zidunde kama mbegu ya ubuyu basi zimenye maganda yote kisha upete halafu uchague zile punje nzuri tu ambazo hazina rangi ya njao ama hazina kutu.
7) hakikisha wamba nafaa zako hizi zimekauka sana na hakuna hata punje moja mbovu ndipo uziwee pamoja na kuazisaga mashine. hakikaisha pia unga unaposagwa unarudiwa mara ya pili ili uwe mlaini usiwe na chenga chenga.
8) baada ya kusaga anika unga wako mahali pakavu hadi upoe, na hakikaisha wakati wa kuanika hautachafua. kuwa safe zaid ni bora ukajitahd nyumban ukawa na kitambaa ambacho unakiweka juu ya ungo wako kisha unamimina unga wako, ukiuweka juani tafuta kitambaa kingine kilicho cha nyavu nyavu uweke kwa juu kufunika unga wako usifwatwe na wadudu ama kupata uchafu.
Ukisha kauka tafuta chombo kikavu uweke na ufunike vizuri kisiwe na sehem ya kupitasha wadudu.
nitarudi baadae kueleza namna ya kuupika uji huu. ila naamini maandalizi ya awali mtakuwa mmesha yapata vyema.
da AshaDii The secretary kumbukeni kwamba uji huu anaweza kulishwa mtoto wa kuanzia miezi 6.
Kwanini zinataiwa ziwe