Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Kuna habari kuwa shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF hawataongeza muda wa mkataba wa kuifundisha timu ya taifa ya Tanzania kwa kocha Marcio Maximo utakapokwisha mwezi wa Juni. Hivyo shirikisho hilo linategemea kutangaza nafasi hiyo ili kuweza kupata kocha wa kuchukua mikoba ya Maximo.
Juzi katika kipindi cha michezo TBC, kocha wa timu ya Manyema Rangers Abdallah Kibadeni "King Mputa" aliweka wazi kuwa yeye kama kocha mzawa ataomba nafasi hiyo kama mzawa kwa kuwa ana vigezo na uwezo wa kumaliza kiu ya watanzania kupata mafanikio katika medani ya soka la kimataifa.
Pia kocha mwingine kutoka visiwani Zanbibar, Hemed Morocco ambaye aliiwezesha Zanzibar kushika nafasi ya tatu katika mashindano ya Challenge hivi karibuni naye alionyesha nia ya kuomba nafasi hiyo. Tanzania ina makocha wa soka wengi tu wenye sifa zinazotofautiana miongoni mwao. Mbali ya hao niliowataja hapo juu wapo pia watu kama Charles Boniface Mkwasa, Fredi Felix Minziro, Juma Mwambusi, Sunday Kayuni, Syllersaid Mziray, Salum Madadi na wengine wengi.
Je tunadhani ili kupata mafanikio katika soka Tanzania inahitaji kocha wa aina gani? Kwani wazawa wamekuwa mstari wa mbele kuonyesha kuwa wanaweza kama watapata support aliyopewa Maximo, pia kuna makocha wa kigeni walionyesha pia nia ya kuitaka kazi hiyo....Nawasilisha.
Juzi katika kipindi cha michezo TBC, kocha wa timu ya Manyema Rangers Abdallah Kibadeni "King Mputa" aliweka wazi kuwa yeye kama kocha mzawa ataomba nafasi hiyo kama mzawa kwa kuwa ana vigezo na uwezo wa kumaliza kiu ya watanzania kupata mafanikio katika medani ya soka la kimataifa.
Pia kocha mwingine kutoka visiwani Zanbibar, Hemed Morocco ambaye aliiwezesha Zanzibar kushika nafasi ya tatu katika mashindano ya Challenge hivi karibuni naye alionyesha nia ya kuomba nafasi hiyo. Tanzania ina makocha wa soka wengi tu wenye sifa zinazotofautiana miongoni mwao. Mbali ya hao niliowataja hapo juu wapo pia watu kama Charles Boniface Mkwasa, Fredi Felix Minziro, Juma Mwambusi, Sunday Kayuni, Syllersaid Mziray, Salum Madadi na wengine wengi.
Je tunadhani ili kupata mafanikio katika soka Tanzania inahitaji kocha wa aina gani? Kwani wazawa wamekuwa mstari wa mbele kuonyesha kuwa wanaweza kama watapata support aliyopewa Maximo, pia kuna makocha wa kigeni walionyesha pia nia ya kuitaka kazi hiyo....Nawasilisha.