TRUE STORY...msinirushie mawe

ina maana kila mwanamke mzuri lazima umuonje?
kwani ulikuwa na ulazima gani kuzaa nae? si ungempotezea tu?
yaani mtu unajijua umeowa alafu hawara yako anakuomba mimba na wee unampa kwa roho nyeupee.
kwakweli umeitia doa kubwa sana ndoa yako. you should tell your wife all the details
 
Sasa unaumia kichwa kitu gani??? Jifanye kama wewe sio mchezaji kwenye hilo game, then kaa pembeni uone nini kitatokea...
 
Wanaume wengine bhana, ovyoooo kabisa.

hakika umetia doa ndoa yako, hata kama ukimwambia na mkeo akakusamehe, ndoa yenu ni shida sana kurudi kama ilivyokuwa awali.

nami nakupa hongera zako nyingi sana kwa uanaume uliokuwa nao.
 
niliondoka home, nikaenda kufanya kazi mkoa fulani hapa tz, nimekaa huko kwa muda mrefu. Waifu anafanya kazi hapa dsm. ....nimeoa nina watoto. Tatizo lilinitokea, nikiwa huko nilikutana na mwanamke mmoja, ni mrefu, mwembamba kidogo ila hips kubwa, ni mzuri ajabu, mamake ni mtutsi babake mchaga wa marangu, mara ya kwanza ilikuwa kama utani, tukaanza urafiki, tukaenda kupima, tukawa negative, tukaanza kutumia ndomu, nilikuwa nakaa lodge hivyo wiki mbili za mwanzo alikuwa anahudhuria kwenye lodge kila siku.

Alihamia kabisa, na akaacha kazi, tukawa tunaishi wote kwenye lodge. Sikujua ni kitu gani aliona kwangu, sijui nilimfanya vizuri sana ila toka siku ya kwanz anilimwambia mimi nimeoa mke wangu yuko dsm na ni mkali sana na ana wivu, tukawa tunafanya tu.

Kati ya miezi karibia sita au saba, tulikaa lodge tofautitofauti, ila tulikuwa tunakaa pamoja. Kazi yangu ilikuwa ni ya kufanyia tu ndani ya lodge na kama kwenda ofisini ni kwenda naye pamoja na kuweka doc kwa bos na tunarudi wote, yeye hakutaka kuniacha hata mara moja akiogopa nitamtoroka, ati nitabadilisha lodge na kumkimbia. Alinipenda akawa analia usiku machozi ati anatamani kama angekutana na mke wangu akubaliane naye amruhusu awe mke wa pili, atamheshimu sana mke wangu, akawa anajilaumu kwamba ni kwanini mimi niliwahi kuoa kabla sijakutana na yeye?

Tukiwa sita kwa sita mara nyingi namuona anatoa mikelele kuwa kwanini nimewahi kabla sijakutana naye, manake angekuwa mke wangu. Aling'angá nia kuniita mume na mimi nikawa nakata jina hilo. Nilikuwa nashangaa, kwanini mwanamke mzuri hivi analia machozi na yuko serious, hatanii, kwamba anatamani angekuwa mke wangu hata wa pili haingekuwa shida kwake?....mimi ni mwanaume sina sura nzuri najijua, ni nunda mweusi....yeye ana weupe wa kichaga na umbo na sura ya kinyarwanda (mamake alikimbia ile genocide)....babake ni tajiri tu ana bar kibao mwanza pale.

siku moja tukiwa tumekaa, akaniambia anatamani kama angebeba damu yangu, kwasababu anajua mimi sitamuoa kwani nampenda sana mke wangu kuliko yeye. Nilimtisha kuwa mke wangu atakutoa roho ukijifanya kuning'ang'ania...mzuriiii,....nilikuwa makini kuhesabu tarehe siku za mimba na bleed yake,....nimejikuta nimetwika mimba tayari,...ana mimba ya miezi minne sasaivi,...ninahudumia mimba na yeye nampenda ile sitamuoa na nilishamwambia mkataba wetu ni mtoto tu, si yeye...amefurahi sana kubeba damu yangu tumboni mwake...sasaivi amehamia arusha anafanya kazi kule......napigiana naye simu kila siku kabla ya kufika home, ana akili sana, ni mwaminifu sana kati ya mademu niliowaikuwa nao.

Najua niliteleza, nilimtenda waifu kosa kubwa...juzi waifu anasali kwa mwingira, aliniamsha saa kumi za usiku akasema ameonyeshwa na mungu kwenye ndoto kuwa mimi nina mke mwingine, akaniambia yote niliyoyafanya...niliogopa, lakini wkasababu mimi ni mbabe kidogo nilimfokea kwanini ananivurugia usingizi na kwanini ananiambia hivyo, nikapotezea...lakini niliumia moyoni kwanini nilifanya vile...kumtelekeza mwanamke yule na mimba naona sio fresh, pamoja na kwamba anaweza kulea yeye mwenyewe, .......nitaanzaje kumwambia waifu kuwa nina mtoto nje?...waifu ananipenda sana na mimi nampenda kuliko wanawake wote duniani najua tutasameheana lakini pa kuanzia sijui....yule wa arusha na mimba yangu, nashukuru mungu hatakinukisha.....



usiwaze wala nini

kuanguka kupo na ni kawaida kwa yeyote yule
a piece of an advice ni kwamba uendelee kuihudumia damu yako ile
 
Mwingira nooma ana upako kamwambukiza na mkeo!? anaota? nimeoteshwa? hapo kazi ipo kaka.....
 
Hehehe kumbe rahisi hivi? Ngojaa siku mkewe achoke kusali huko ka mwingira ahamie kanisa l jf apate maushauri. Atakapoitisha kikao cha familia kumuambbia na yeye amemimbwa na boss wake. Yaani mtenda hutendwa, you should bear that in mind kabla hujaanza vituko,
muelezee 2 wife, alalamike muitishe kikao cha familia, mchague mtu unaemuamini kwenye family diplomacy awakalishe na ndugu zako chini, mtambulishe mtoto. .
 
yani sijui hata nianzie wapi maskini.............ulipokuwa unaanzisha na huyo chotara ungekuja MMU upewe ushauri ndugu!!! ili sasa hili goma kulicheza inabidi utegeshee mdundo ukianza nawewe ucheze
Pole na hongera
 
Hehehe kumbe rahisi hivi? Ngojaa siku mkewe achoke kusali huko ka mwingira ahamie kanisa l jf apate maushauri. Atakapoitisha kikao cha familia kumuambbia na yeye amemimbwa na boss wake. Yaani mtenda hutendwa, you should bear that in mind kabla hujaanza vituko,

ahsante Kinga'sti hahahaaaa, na mimi nasistiza Vivyo hivyo ulivyotenda na ndio mkeo atakutenda pia we subiri utakuja tu hapa JF ukitoa mapovu. kama Mungu anavyosema mu mwili mmoja si wawili tena, ndio maana kajua wewe hata ujitahidi kuwa mkali lakini yeye amejua tayari kwamba umeanguka.
 
Sasahivi ndiyo unajua unampenda mkeo kuliko wanawake wote duniani? nyama weee. Umelikoroga na uubebe mzigo wako
 
ha ha baba mchungaji amesaliti ndoa he he kweli shetani ana nguvu. pole sana ubungo ubungo kwani ukiwa safarini unasahau maombi
 
Umetisha kaka .. Umetisha.. Mwanaume kuzaa.. Ah.. Waje wake waje duniani waje.. Bado nafasi ipo waleteni tu.. Nini Kwani asizae..!! Hee huyu nae vipi tena.. Kama hizai ni wewe, kila mjinga lazima abebe ujinga wake, Mke ataambatana Na Mumewe Sasa Mke a namwacha mjidume peke yake we vipi weye.. Tena nikwambie .. Mke wako huko ulivyoenda nae walimtengeneza huku.. Na bado wanamtengeneza, MSG zako alizibamba Na akamforwadia jamaa yake, kisha wakasuka mpango ati aseme ameonyeshwa.. Ha ha haaa.. Kula tu Na vyako vyaliwa..
 
NILIONDOKA HOME, nikaenda kufanya kazi mkoa fulani hapa tz, nimekaa huko kwa muda mrefu. waifu anafanya kazi hapa dsm. ....nimeoa nina watoto. tatizo lilinitokea, nikiwa huko nilikutana na mwanamke mmoja, ni mrefu, mwembamba kidogo ila hips kubwa, ni mzuri ajabu, mamake ni mtutsi babake mchaga wa marangu, mara ya kwanza ilikuwa kama utani, tukaanza urafiki, tukaenda kupima, tukawa negative, tukaanza kutumia ndomu, nilikuwa nakaa lodge hivyo wiki mbili za mwanzo alikuwa anahudhuria kwenye lodge kila siku.

alihamia kabisa, na akaacha kazi, tukawa tunaishi wote kwenye lodge. sikujua ni kitu gani aliona kwangu, sijui nilimfanya vizuri sana ila toka siku ya kwanz anilimwambia mimi nimeoa mke wangu yuko dsm na ni mIkali sana na ana wivu, tukawa tunafanya tu.

kati ya miezi karibia sita au saba, tulikaa lodge tofautitofauti, ila tulikuwa tunakaa pamoja. kazi yangu ilikuwa ni ya kufanyia tu ndani ya lodge na kama kwenda ofisini ni kwenda naye pamoja na kuweka doc kwa bos na tunarudi wote, yeye hakutaka kuniacha hata mara moja akiogopa nitamtoroka, ati nitabadilisha lodge na kumkimbia. alinipenda akawa analia usiku machozi ati anatamani kama angekutana na mke wangu akubaliane naye amruhusu awe mke wa pili, atamheshimu sana mke wangu, akawa anajilaumu kwamba ni kwanini mimi niliwahi kuoa kabla sijakutana na yeye?

tukiwa sita kwa sita mara nyingi namuona anatoa mikelele kuwa kwanini nimewahi kabla sijakutana naye, manake angekuwa mke wangu. aling'angá nia kuniita mume na mimi nikawa nakata jina hilo. nilikuwa nashangaa, kwanini mwanamke mzuri hivi analia machozi na yuko serious, hatanii, kwamba anatamani angekuwa mke wangu hata wa pili haingekuwa shida kwake?....mimi ni mwanaume sina sura nzuri najijua, ni nunda mweusi....yeye ana weupe wa kichaga na umbo na sura ya kinyarwanda (mamake alikimbia ile genocide)....babake ni tajiri tu ana bar kibao mwanza pale.

SIKU MOJA TUKIWA TUMEKAA, akaniambia anatamani kama angebeba damu yangu, kwasababu anajua mimi sitamuoa kwani nampenda sana mke wangu kuliko yeye. nilimtisha kuwa mke wangu atakutoa roho ukijifanya kuning'ang'ania...mzuriiii,....nilikuwa makini kuhesabu tarehe siku za mimba na bleed yake,....nimejikuta nimetwika mimba tayari,...ana mimba ya miezi minne sasaivi,...ninahudumia mimba na yeye nampenda ile sitamuoa na nilishamwambia mkataba wetu ni mtoto tu, si yeye...amefurahi sana kubeba damu yangu tumboni mwake...sasaivi amehamia arusha anafanya kazi kule......napigiana naye simu kila siku kabla ya kufika home, ana akili sana, ni mwaminifu sana kati ya mademu niliowaikuwa nao.

najua niliteleza, nilimtenda waifu kosa kubwa...juzi waifu anasali kwa mwingira, aliniamsha saa kumi za usiku akasema ameonyeshwa na Mungu kwenye ndoto kuwa mimi nina mke mwingine, akaniambia yote niliyoyafanya...niliogopa, lakini wkasababu mimi ni mbabe kidogo nilimfokea kwanini ananivurugia usingizi na kwanini ananiambia hivyo, nikapotezea...lakini niliumia moyoni kwanini nilifanya vile...kumtelekeza mwanamke yule na mimba naona sio fresh, pamoja na kwamba anaweza kulea yeye mwenyewe, .......nitaanzaje kumwambia waifu kuwa nina mtoto nje?...waifu ananipenda sana na mimi nampenda kuliko wanawake wote duniani najua tutasameheana lakini pa kuanzia sijui....yule wa arusha na mimba yangu, nashukuru Mungu hatakinukisha.....
Cheating is a crime .you have no morals no values, you don't love anybody and you don't know the meaning of love .Get a life and go and xxxxx yourself .I get so irritating and disgusting even throw up .Men like you need to be thrown to jail .what if she has AIDS .
 
ACHENI KUTOA MAPOVU NYIE...story hii nimeitoa sehemu fulani, ilinitachi sana kwasababu sikuipenda ndo maana ikawa kichwani. kwa wale ambao watakuwa wameisoma sehemu, wanawezajua kuwa nimeshindwa kumachisha....poleni kwa kutoa mapovu kama nguruwe pori.....
 
jaman tupeane tu ushauri maana haya mambo ya mapenzi vitu kamahivi vinatokea sana....mm mwenyewe inanitesa kichwa changu sana ...nilikutana na mdada mmoja mzuri sana na mimi kama mwanamume kama wanaume wengine nikapenda na nikaendelea na mengine na dada yule anajua nina mke japo sina mtoto...sasa hivi anang'ang'ana kubeba ujauzito wangu na hataki tuachane niliishajaribu kufanya kila hila asepe lakini wapi
 
Pole na kwa upande mwingine hongera kwa kutaraji mtoto toka kwa huyo demu wako.Kikubwa jua ya kwamba huwezi kugawa penzi hivyo kama uliamua kuzaa nje ya ndoa yako basi huo ni usaliti mkubwa sana ndani ya ndoa yanu, je mkeo nae akiwa na DUME lingine nje utafurai? Kama ndivyo...KILA MTENDA....(Malizia) so taraji hilo jibu kwako....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom