Tanzania Railways Corp
JF-Expert Member
- Mar 23, 2018
- 251
- 595
Shirika la Reli Tanzania - TRC linautaarifu umma kuwa mnamo tarehe 18 Machi 2023 lilitokea tukio la kushambuliwa kwa mfanyakazi wa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa - SGR aitwaye Lucy Paulo mwenye fani ya upishi katika kambi ya mradi wa SGR Fela mkoani Mwanza.
Lucy alishambuliwa na raia wa taifa la China aitwaye Bwana Zheng Yuan Feng majira ya saa tatu kasoro asubuhi eneo la jikoni kwa kumtolea lugha chafu na kumpiga, kitendo hiki kilipelekea Lucy kupata majeraha na kupelekwa hospitali ya Bugando na Siku ya Jumatatu tarehe 20 Machi 2023 alipatiwa matibabu a kuruhusiwa siku ya Jumanne ya tarehe 21 Machi 2023 majira ya asubuhi na kwasasa yupo kambini ya Fela chini ya angalizi wa Daktari wa mradi.
Kufuatia tukio hilo Bwana Zheng alikamatwa a kuzuiliwa kwenye kituo cha Polisi Reli na baadaye kuhamishiwa kituo cha Polisi wilaya ya Misungwi, Mamo tarehe 24 Machi 2023 alipandishwa katika mahakama ya Wilayani Misungwi a Kusomea Mashtaka yake kwa kosa la kujeruhi kesi Na 44 ya mwaka 2023.
Kwasasa yupo rumande katika kituo cha Polisi Misungwi baada ya kushindwa masharti ya dhamana.
TRC imemtaka Mkandarasi kampuni ya CCECC-CRCC kuhakikisha Lucy Paulo anapatiwa stahiki kwa kufuata sheria, taratibu na kuhakikisha anafanya kazi kwa uhuru wakati wote wa mradi, mkandarasi ameridhia kutekeleza matakwa hayo na TRC itaendelea kutatilia.
Shirika linakemea kitendo hicho na vitendo va aina voyote vene lengo la kuleta uonevu na unvanavasaji kwa wafanvakazi na kuwataka wakandarasi kutatilia nvendo zote za wafanvakazi na kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria za chi na matakwa ya kimkataba.
Lucy alishambuliwa na raia wa taifa la China aitwaye Bwana Zheng Yuan Feng majira ya saa tatu kasoro asubuhi eneo la jikoni kwa kumtolea lugha chafu na kumpiga, kitendo hiki kilipelekea Lucy kupata majeraha na kupelekwa hospitali ya Bugando na Siku ya Jumatatu tarehe 20 Machi 2023 alipatiwa matibabu a kuruhusiwa siku ya Jumanne ya tarehe 21 Machi 2023 majira ya asubuhi na kwasasa yupo kambini ya Fela chini ya angalizi wa Daktari wa mradi.
Kufuatia tukio hilo Bwana Zheng alikamatwa a kuzuiliwa kwenye kituo cha Polisi Reli na baadaye kuhamishiwa kituo cha Polisi wilaya ya Misungwi, Mamo tarehe 24 Machi 2023 alipandishwa katika mahakama ya Wilayani Misungwi a Kusomea Mashtaka yake kwa kosa la kujeruhi kesi Na 44 ya mwaka 2023.
Kwasasa yupo rumande katika kituo cha Polisi Misungwi baada ya kushindwa masharti ya dhamana.
TRC imemtaka Mkandarasi kampuni ya CCECC-CRCC kuhakikisha Lucy Paulo anapatiwa stahiki kwa kufuata sheria, taratibu na kuhakikisha anafanya kazi kwa uhuru wakati wote wa mradi, mkandarasi ameridhia kutekeleza matakwa hayo na TRC itaendelea kutatilia.
Shirika linakemea kitendo hicho na vitendo va aina voyote vene lengo la kuleta uonevu na unvanavasaji kwa wafanvakazi na kuwataka wakandarasi kutatilia nvendo zote za wafanvakazi na kuchukua hatua kwa mujibu wa Sheria za chi na matakwa ya kimkataba.