Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,508
- 8,129
Habari wakuu,
Wakati sakata la rushwa kwa matrafik likiendelea nimewakumbuka Trafic 'wanaotega' kabla kidogo ya daraja la JKT Mlalakuwa (Wana kibanda chao pia pembeni). Ndugu zetu hawa asubuhi huzisimamisha daladala zote zinazoelekea Kawe kupitia Old Bagamoyo na kawaida huchukua 2,000 kwa kila daladala.
Hizi ni daladala za Kawe-Gerezani, Mbagala-Kawe, Kawe-Tandika na nyinginezo. Ni daladala nyingi sana ndani ya saa moja.
Wakipiga mkono, daladala itasimama mbele kidogo na kondakta atashuka kwenda kumalizana nae, trafic hatalisogelea gari wala kulikagua. Zipo tetesi Trafic hawa hucheza 'upatu' wa 70 elfu kwa kila mmoja kutoka kwenye mapato yanayoletwa na makondakta.
Pamoja na utawala uliopita kuruhusu 'Hela ya kubrashia' rushwa ya barabarani haikuwahi kuwa wazi kiasi hiki.
Wakati sakata la rushwa kwa matrafik likiendelea nimewakumbuka Trafic 'wanaotega' kabla kidogo ya daraja la JKT Mlalakuwa (Wana kibanda chao pia pembeni). Ndugu zetu hawa asubuhi huzisimamisha daladala zote zinazoelekea Kawe kupitia Old Bagamoyo na kawaida huchukua 2,000 kwa kila daladala.
Hizi ni daladala za Kawe-Gerezani, Mbagala-Kawe, Kawe-Tandika na nyinginezo. Ni daladala nyingi sana ndani ya saa moja.
Wakipiga mkono, daladala itasimama mbele kidogo na kondakta atashuka kwenda kumalizana nae, trafic hatalisogelea gari wala kulikagua. Zipo tetesi Trafic hawa hucheza 'upatu' wa 70 elfu kwa kila mmoja kutoka kwenye mapato yanayoletwa na makondakta.
Pamoja na utawala uliopita kuruhusu 'Hela ya kubrashia' rushwa ya barabarani haikuwahi kuwa wazi kiasi hiki.