PauliMasao
JF-Expert Member
- Nov 26, 2007
- 286
- 39
Mimi nimechoka na hawa traffic police hapa Arusha. Baadala ya kuongoza magari au kuangalia wavunja sheria barabarani wao hujikusanya sehemu mbali mbali ya jiji letu, kazi kubwa ni kuomba pesa. Unasimamishwa halafu wanajifanya kucheki gari wakiona hamna kitu wanakuomba japo buku tano ya lunch. Sasa kwa hesabu za haraka haraka, traffic police mmoja akisimamisha magari ishirini kwa siku, anweza kujipatia shilingi laki moja kwa siku. Je huu sio ufisadi?