Magufuli 05
JF-Expert Member
- May 7, 2023
- 968
- 2,029
Mmewakamata asubuhi kwa makosa ya usalama barabarani,
Yes ni sahihi kabisa, lakini kwanini mnafanya oparesheni kwa matukio. Leo mmeendesha oparesheni ya kihuni kwa kisingizio kwamba mwenzao Jana Kagongwa na mwendokasi. Hivyo mmepata maagizo kutoka juu muwashugulikie.
Nyinyi askari mnachangia bodaboda wawe na tabia hizi ambazo wanazo, kwasababu zifuatazo
1. Mnapopanda bodaboda tena kwa msaada huwa hamvai kofia ngumu (helmet).
2. Bado hamjatoa elimu kwa upana kuhusu bodaboda kutambua kwamba na wao wanaendesha vyombo vya moto hivyo SHERIA za usalama barabarani zinawahusu. Media zipo lakini hamtaki kuzitumia vizuri mnababaisha tu kwenye vipindi vya dk 10 au 20.
3. Bado nyinyi hamjaamua kusimamia barabara SHERIA za usalama barabarani kwasasabu mnaendesha jeshi la polisi kana kwamba tupo mwaka 1974 kumbe ni 2023. Hivi niwaulize, dereva akivuka mataa yanayomkataza kufanya hivyo mnampataje ili kum penalize? Kwanini bodaboda wanawapita mkiwa mnaongoza magari na wala hamuhangaiki nao pale wanapo force kupita wakati mmezuia?
Sasa angalia leo hapo kanda maalumu ya trafiki, mmewakamata mnawalazimisha waende Kariakoo Kununua helmet ndiyo muwaachie. SHERIA ipi inaelekeza hivyo? Tatizo la bodaboda nchi nzima ni mfumo wenu ndiyo umelileta, hili janga. Msiwageuze kitega uchumi. Toeni elimu Kisha msimamie sheria.
Na wewe mama afande mtu mzima na maji ya kunde mwenye maneno mengi acha tabia hiyo, kuwa makini na abiria mnaowakamata hapo kwa kudhani wote ni mbumbumbu wa SHERIA. Utanaswa kwenye tundu bovu.
Yes ni sahihi kabisa, lakini kwanini mnafanya oparesheni kwa matukio. Leo mmeendesha oparesheni ya kihuni kwa kisingizio kwamba mwenzao Jana Kagongwa na mwendokasi. Hivyo mmepata maagizo kutoka juu muwashugulikie.
Nyinyi askari mnachangia bodaboda wawe na tabia hizi ambazo wanazo, kwasababu zifuatazo
1. Mnapopanda bodaboda tena kwa msaada huwa hamvai kofia ngumu (helmet).
2. Bado hamjatoa elimu kwa upana kuhusu bodaboda kutambua kwamba na wao wanaendesha vyombo vya moto hivyo SHERIA za usalama barabarani zinawahusu. Media zipo lakini hamtaki kuzitumia vizuri mnababaisha tu kwenye vipindi vya dk 10 au 20.
3. Bado nyinyi hamjaamua kusimamia barabara SHERIA za usalama barabarani kwasasabu mnaendesha jeshi la polisi kana kwamba tupo mwaka 1974 kumbe ni 2023. Hivi niwaulize, dereva akivuka mataa yanayomkataza kufanya hivyo mnampataje ili kum penalize? Kwanini bodaboda wanawapita mkiwa mnaongoza magari na wala hamuhangaiki nao pale wanapo force kupita wakati mmezuia?
Sasa angalia leo hapo kanda maalumu ya trafiki, mmewakamata mnawalazimisha waende Kariakoo Kununua helmet ndiyo muwaachie. SHERIA ipi inaelekeza hivyo? Tatizo la bodaboda nchi nzima ni mfumo wenu ndiyo umelileta, hili janga. Msiwageuze kitega uchumi. Toeni elimu Kisha msimamie sheria.
Na wewe mama afande mtu mzima na maji ya kunde mwenye maneno mengi acha tabia hiyo, kuwa makini na abiria mnaowakamata hapo kwa kudhani wote ni mbumbumbu wa SHERIA. Utanaswa kwenye tundu bovu.