Tido Mhando alishindwa vipi TBC? Je, ataweza Azam kwa Bakhressa?

Tido mtu safi sana tatizo TBC lilikuwa CCM sasa hivi Azam TV itakuwa juu sana mimi namkubali sanaaaaaa!!!!
 
TIDO ni mtu makini na mwenye kuijua tasnia ya habari vizuri,pamoja na mkataba wake kwisha lakini kilichomuondoa pale tbc ni kipindi cha jimbo kwa jimbo kwani kiliwaumbua wengi kwa kushindwa kujibu hoja za wananchi.
 
Tido hakushindwa tbccm alifukuzwa na ccm baada ya kuanzisha kipindi cha mchakato majimboni.usijifanye umesahau.
 
mtoa mada tuambie tido alishindwa nini tbc na tokea anaondoka tbc imepiga hatua gani mbele?
 
a2.jpg


TIDO alianza TBC na inaonekana kule kulikuwa na siasa nyingi na jana tumeona Azam wamejenga studio ambayo kwa picha zinaonekana si haba!

Cha kujiuliza; Je, alishindwa vipi TBC? Na Je, ataweza AZAM kwa Bakhressa?

Ukiwa na tabia ya kusema ukweli hutakaa kamwe upatane na anaye penda kusema UONGO. so AZAM TV bila shaka nao ni wakweli kama yeye Tido!
 
Tido ni jembe usipime! amepiga kazi ya ukweli BBC mpaka kesho wanamkubali ijekua hapa Bongo? TBC waliingiza mizengwe na hta hivo alikuea kishawaweka pazuri! Tbc ipo hapo ilipo kwa sababu yake!
 
huyu nae!! Tido lilikua jembe la tbc ila toka alivoondoka tbc ndo chali kabisa na haipendwi na watu including myself kwa kua hot issues zote tbc wanakua mabubu.
 
Tido ni jembe usipime! amepiga kazi ya ukweli BBC mpaka kesho wanamkubali ijekua hapa Bongo? TBC waliingiza mizengwe na hta hivo alikuea kishawaweka pazuri! Tbc ipo hapo ilipo kwa sababu yake!

Jamani mbona BBC Swahili Service ilihanzishwa katikati ya miaka ya 1950s, Hamza Kassongo aliwahi kufanya kazi pale, Oscar Kambona na wengine wengi tu, sisi hatujui mkataba wa Tido na Serikali ulikuwa na masharti yapi - sasa haya mambo ya ku-blame blame tu Serikali bila ya kujua upande wa pili wa shillingi sio fresh kabisa, sio kwamba tuna-under rate uwezo mkubwa wa Ndugu TIDO lakini sio vizuri vile vile kuongeza chumvi.
 
Dastan Tido Mhando gwiji na jabali la habari.

ccm na hofu ya mijadala ya kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni kwa ukweli, uwazi na weledi walishindwa kuhimili kishindo cha mbabe huyu mwenye mashiko katika tasnia ya habari.

ccm wakamtimuwa Tido kwa kisingizio cha kuisha mkataba tukijuwa wazi ilikuwa kazi ya ku-review na kumpa mkataba mwingine.

Dastan Tido Mhando aliazimia kukata ngebe za ccm na wanasiasa wake kuifanya TBC isiwe yakisiasa/ccm bali chombo cha umma kwelikweli. Ccm wakaona wanaporwa pakuwahadaa watanzania kwa propaganda za kizushi, vitisho na danganya toto. Kuondoa tishio hilo ccm na kikwete wao wakakataaa katakata ku-review contract hatimaye Mhando kutoswa.

Amakweli sasa watajuta maana huyu jamaa nimbunifu sana sana. nachelea kusema Super sport na bei zao za ajabu watatoweka muda si mrefu hapa TZ. EPL namazagazaga mengine yakutosha yatapatikana AZAMTV. Na chaguo langu ITV kwa kweli imepata mshindani wa kweli.

Bilashaka Tido ataifanya Azam kuwa juuu kabisa.

Mkuu umenena vema sana! Azam Tv wataenda mbali sanaa but nina ushauri mmoja kwao: King'amuzi chao picha inaganda na tatizo hili kadri siku zinavyoenda linazidi, pia ikinyesha mvua kidogo tu inakata! najua wako humu walifanyie kazi hili limeanza kuwa kero.
 
Makamba alimwambia Tido kama hukifuti kipindi cha harakati jimboni utaona uchaguzi ukiisha.Nasikia mkataba wake mpya ulikuwa ushaandaliwa.Wakati anajiandaa kusaini uchaguzi ulipomalizika wakamwambia asante sana hatutaweza kuendelea na wewe.Jamaa alitangaza ofa ya lunch kwa wafanyakazi waliokuwepo halafu akasepa zake. Nasikia Kagame akamtaka kule Rwanda wakubwa wakamkatalia.
 
Jamani mbona BBC Swahili Service ilihanzishwa katikati ya miaka ya 1950s, Hamza Kassongo aliwahi kufanya kazi pale, Oscar Kambona na wengine wengi tu, sisi hatujui mkataba wa Tido na Serikali ulikuwa na masharti yapi - sasa haya mambo ya ku-blame blame tu Serikali bila ya kujua upande wa pili wa shillingi sio fresh kabisa, sio kwamba tuna-under rate uwezo mkubwa wa Ndugu TIDO lakini sio vizuri vile vile kuongeza chumvi.

Sijablme ila kwa trend ya tanzania ilivyo na.mifumo yake ni wazi tu kuwa Tido si wa kwanza kufanya kazi na vyombo vikubwa vya nchi hii na bdo system ikamtupa nje kama karunguyeye!
just go back to ur references utanielewa!
 
ishu ya tido kuwa azam ni nzuri na inaleta changamoto pia kwa vyombo vingine vya habari vya nyumbani ila unaposema ataonesha ushindani kwa dstv si kazi rahisi wajipange sana na kuchukua EPL SI KAZI NDOGO japo hakuna lishindikanalo chini ya jua
 
kqa pesa alizonazo bakhressa studio.inaonekana iko cheap wafanyakazi nao kuvalishwa kama.wauza ice cream.noma
 
Back
Top Bottom