Vitendo
JF-Expert Member
- Oct 23, 2009
- 582
- 103
ASA ni dhahiri kwamba, mkataba kati ya Serikali na Kitengo cha Kuhudumia Kontena Bandarini - TICTS, hauwezi kuvunjwa.
Hali hiyo inatokana na ukweli kwamba, kazi ya kuuvunja itaambatana na gharama kubwa ambazo kwa sasa Serikali haiwezi kuzimudu.
Akitoa taarifa ya Serikali kuhusu hatua za utekelezaji wa Azimio la Bunge juu ya utendaji usioridhisha wa TICTS mjini Dodoma, Waziri wa Maendeleo ya Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema busara imeonesha hakuna haja ya kuvunja mkataba huo kwa sasa.
Kama mkataba ukivunjwa, Serikali itapaswa kulipa fidia ya Sh bilioni 645, hali ambayo ni mzigo mkubwa kwa walipa kodi wa Tanzania.
Alisema Serikali ilimuuliza Mwanasheria Mkuu wa Serikali kama Taifa linaweza kushinda kesi hiyo ya mkataba na kubaini kwamba haiwezi kushinda kwa sababu uliingiwa kihalali.
Mkataba huu ni halali na iwapo Serikali itatumia nguvu kuvunja au kusitisha nyongeza ya muda wa ukodishaji, na suala hili likafikishwa kwa msuluhishi, Serikali ingepata hasara kwa kuilipa TICTS fidia iliyokadiriwa kuwa Sh bilioni 645, alisema Waziri Kawambwa.
Bunge lilitaka kusitishwa kwa nyongeza ya muda wa miaka 15 iliyopewa TICTS kwa kuwa nyongeza hiyo ilitolewa kinyume cha utaratibu, kwani katika mkataba wa awali kifungu cha 9.1 kiliweka bayana kuwa kifungu cha muda wa mkabata hakitafanyiwa marekebisho yoyote bila kufuata taratibu zinazooneshwa katika mkataba wa kwanza.
Aidha, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka 2007/2008 alieleza kuwa nyongeza ya miaka 15 waliyopewa TICTS haikuzingatia Sheria ya Manunuzi ya Umma namba 21 ya mwaka 2004, na hivyo nyongeza hiyo ni batili.
Katika mkutano wa 11 wa Bunge, hoja binafsi iliwasilishwa ya kuvunja mkataba na TICTS kutokana na utendaji wake usioridhisha na Bunge kupitisha azimio Aprili 25, 2008.
Pamoja na kushindwa kuvunja mkataba huo wa nyongeza, Dk. Kawambwa alisema Serikali imefanikiwa kuondoa ukiritimba wa TICTS bandarini na pia kufanya marekebisho kadhaa ya msingi yanayotaka TICTS kuwajibika zaidi bandarini na pia kuondolewa kwa nafasi yao ya kukusanya tozo na kwamba sasa bandari itafanya kazi yake hiyo yenyewe.
Mambo mengine ambayo Serikali iliibana TICTS ni pamoja na kutayarisha na kuwasilisha mpango wa uwekezaji wa miaka mitano mitano kwa kipindi cha Januari 2009 mpaka 2013, Januari 2014 mpaka 2018 na wa miaka saba, kuanzia Januari 2019 mpaka 2025.
Pia viwango vya vigezo kwa ajili ya kupima utendaji vimebadilishwa na sasa vitapimwa kwa ufanisi wa matumizi ya yadi; ufanisi wa mitambo inayotumika kuhudumia kontena katika yadi.
Aidha, TICTS kurudisha vifaa vilivyokwisha muda wake wa matumizi kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) na kurekebisha utaratibu wa kukusanya tozo kwa wanaotumia miundombinu ya bandari.
Katika hili, TICTS walikuwa wanakusanya tozo kila siku na kuilipa TPA mwisho wa mwezi, kwa sasa ukusanyaji huo wa kila siku utafanywa na bandari yenyewe, alisema Dk. Kawambwa.
Alisema Serikali na TICTS wametiliana saini mkataba mpya wa nyongeza namba tatu wa kuelewana katika utekelezaji wa masuala yaliyokubaliwa na pande zote mbili.
Dk. Kawambwa alikiri kuwapo upungufu katika baadhi ya vipengele vya Mkataba huo uliosainiwa Mei 5, 2000 ukiwa awali wa miaka 10 na kutarajiwa kwisha mwaka huu.
Mwaka 2005 mkataba huo uliongezwa kwa miaka 15 kabla ya muda wa ukodishaji wa awali kumalizika.
Utaratibu wa kubinafsisha kitengo hicho ulitumia mfumo wa Mamlaka ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC) ambapo ulikubaliwa na taasisi hiyo, Serikali na Benki ya Dunia.
Hata hivyo, Waziri Kawambwa alisema hatua zilizokwishachukuliwa zimesaidia kuongeza ufanisi katika bandari na kwa sasa utendaji kazi wa bandari hiyo unaridhisha.
Awali wadau walibainisha kuwa pamoja na matatizo katika mkataba huo, pia yapo matatizo mengine yanayozorotesha ufanisi wa utendaji katika bandari.
Matatizo hayo ni ya kukosekana kwa ufanisi wa kushughulikia kadhia ya forodha, upatikanaji wa haraka wa taarifa za malipo na uwekaji tozo ili watumiaji wa bandari wasiigeuze kuwa ghala la bidhaa zao.
Baada ya kuiondolea ukiritimba TICTS, Serikali kupitia TPA, imeanza kutekeleza mpango wa kuboresha miundombinu ya bandari kwa kujenga gati mbili mpya na kuboresha zilizopo ili kuongeza uwezo wa kuhudumia meli kubwa.
Kutokana na juhudi za kuboresha huduma ya bandari, Waziri Kawambwa amesema kwa sasa muda wa kontena kukaa bandarini umepungua kutoka wastani wa siku 20 Januari 26, 2009 kufikia siku 12 Februari mwaka huu, huku muda wa meli za kontena kusubiri nje ya lango la bandari umepungua kutoka wastani wa siku 25 Januari mwaka jana mpaka siku 3.5 Februari mwaka huu.
Taarifa hiyo haikujadiliwa na Bunge baada ya Spika Samuel Sitta kutumia vifungu vya kanuni zinazoendesha Bunge na badala yake kuiagiza Kamati ya Miundombinu kuendelea kufuatilia ufanisi wa TICTS na kulipa Bunge taarifa mara kwa mara.
Alisema Serikali imefanya inachoweza kufanya na imefikia hapo na hakuna sababu za kuendelea kulumbana.
Hali hiyo inatokana na ukweli kwamba, kazi ya kuuvunja itaambatana na gharama kubwa ambazo kwa sasa Serikali haiwezi kuzimudu.
Akitoa taarifa ya Serikali kuhusu hatua za utekelezaji wa Azimio la Bunge juu ya utendaji usioridhisha wa TICTS mjini Dodoma, Waziri wa Maendeleo ya Miundombinu, Dk. Shukuru Kawambwa, alisema busara imeonesha hakuna haja ya kuvunja mkataba huo kwa sasa.
Kama mkataba ukivunjwa, Serikali itapaswa kulipa fidia ya Sh bilioni 645, hali ambayo ni mzigo mkubwa kwa walipa kodi wa Tanzania.
Alisema Serikali ilimuuliza Mwanasheria Mkuu wa Serikali kama Taifa linaweza kushinda kesi hiyo ya mkataba na kubaini kwamba haiwezi kushinda kwa sababu uliingiwa kihalali.
Mkataba huu ni halali na iwapo Serikali itatumia nguvu kuvunja au kusitisha nyongeza ya muda wa ukodishaji, na suala hili likafikishwa kwa msuluhishi, Serikali ingepata hasara kwa kuilipa TICTS fidia iliyokadiriwa kuwa Sh bilioni 645, alisema Waziri Kawambwa.
Bunge lilitaka kusitishwa kwa nyongeza ya muda wa miaka 15 iliyopewa TICTS kwa kuwa nyongeza hiyo ilitolewa kinyume cha utaratibu, kwani katika mkataba wa awali kifungu cha 9.1 kiliweka bayana kuwa kifungu cha muda wa mkabata hakitafanyiwa marekebisho yoyote bila kufuata taratibu zinazooneshwa katika mkataba wa kwanza.
Aidha, Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), mwaka 2007/2008 alieleza kuwa nyongeza ya miaka 15 waliyopewa TICTS haikuzingatia Sheria ya Manunuzi ya Umma namba 21 ya mwaka 2004, na hivyo nyongeza hiyo ni batili.
Katika mkutano wa 11 wa Bunge, hoja binafsi iliwasilishwa ya kuvunja mkataba na TICTS kutokana na utendaji wake usioridhisha na Bunge kupitisha azimio Aprili 25, 2008.
Pamoja na kushindwa kuvunja mkataba huo wa nyongeza, Dk. Kawambwa alisema Serikali imefanikiwa kuondoa ukiritimba wa TICTS bandarini na pia kufanya marekebisho kadhaa ya msingi yanayotaka TICTS kuwajibika zaidi bandarini na pia kuondolewa kwa nafasi yao ya kukusanya tozo na kwamba sasa bandari itafanya kazi yake hiyo yenyewe.
Mambo mengine ambayo Serikali iliibana TICTS ni pamoja na kutayarisha na kuwasilisha mpango wa uwekezaji wa miaka mitano mitano kwa kipindi cha Januari 2009 mpaka 2013, Januari 2014 mpaka 2018 na wa miaka saba, kuanzia Januari 2019 mpaka 2025.
Pia viwango vya vigezo kwa ajili ya kupima utendaji vimebadilishwa na sasa vitapimwa kwa ufanisi wa matumizi ya yadi; ufanisi wa mitambo inayotumika kuhudumia kontena katika yadi.
Aidha, TICTS kurudisha vifaa vilivyokwisha muda wake wa matumizi kwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) na kurekebisha utaratibu wa kukusanya tozo kwa wanaotumia miundombinu ya bandari.
Katika hili, TICTS walikuwa wanakusanya tozo kila siku na kuilipa TPA mwisho wa mwezi, kwa sasa ukusanyaji huo wa kila siku utafanywa na bandari yenyewe, alisema Dk. Kawambwa.
Alisema Serikali na TICTS wametiliana saini mkataba mpya wa nyongeza namba tatu wa kuelewana katika utekelezaji wa masuala yaliyokubaliwa na pande zote mbili.
Dk. Kawambwa alikiri kuwapo upungufu katika baadhi ya vipengele vya Mkataba huo uliosainiwa Mei 5, 2000 ukiwa awali wa miaka 10 na kutarajiwa kwisha mwaka huu.
Mwaka 2005 mkataba huo uliongezwa kwa miaka 15 kabla ya muda wa ukodishaji wa awali kumalizika.
Utaratibu wa kubinafsisha kitengo hicho ulitumia mfumo wa Mamlaka ya Kurekebisha Mashirika ya Umma (PSRC) ambapo ulikubaliwa na taasisi hiyo, Serikali na Benki ya Dunia.
Hata hivyo, Waziri Kawambwa alisema hatua zilizokwishachukuliwa zimesaidia kuongeza ufanisi katika bandari na kwa sasa utendaji kazi wa bandari hiyo unaridhisha.
Awali wadau walibainisha kuwa pamoja na matatizo katika mkataba huo, pia yapo matatizo mengine yanayozorotesha ufanisi wa utendaji katika bandari.
Matatizo hayo ni ya kukosekana kwa ufanisi wa kushughulikia kadhia ya forodha, upatikanaji wa haraka wa taarifa za malipo na uwekaji tozo ili watumiaji wa bandari wasiigeuze kuwa ghala la bidhaa zao.
Baada ya kuiondolea ukiritimba TICTS, Serikali kupitia TPA, imeanza kutekeleza mpango wa kuboresha miundombinu ya bandari kwa kujenga gati mbili mpya na kuboresha zilizopo ili kuongeza uwezo wa kuhudumia meli kubwa.
Kutokana na juhudi za kuboresha huduma ya bandari, Waziri Kawambwa amesema kwa sasa muda wa kontena kukaa bandarini umepungua kutoka wastani wa siku 20 Januari 26, 2009 kufikia siku 12 Februari mwaka huu, huku muda wa meli za kontena kusubiri nje ya lango la bandari umepungua kutoka wastani wa siku 25 Januari mwaka jana mpaka siku 3.5 Februari mwaka huu.
Taarifa hiyo haikujadiliwa na Bunge baada ya Spika Samuel Sitta kutumia vifungu vya kanuni zinazoendesha Bunge na badala yake kuiagiza Kamati ya Miundombinu kuendelea kufuatilia ufanisi wa TICTS na kulipa Bunge taarifa mara kwa mara.
Alisema Serikali imefanya inachoweza kufanya na imefikia hapo na hakuna sababu za kuendelea kulumbana.