The road towards 2010 Elections

Kati ya hawa nani atafaa kutuongoza 2010-2015?

  • Edward Lowassa

    Votes: 0 0.0%
  • Dr. Slaa

    Votes: 7 38.9%
  • Prof. Lipumba

    Votes: 0 0.0%
  • Mizengo Pinda

    Votes: 5 27.8%
  • Samwel Sitta

    Votes: 0 0.0%
  • Jakaya Kikwete

    Votes: 2 11.1%
  • Mark Mwandosya

    Votes: 2 11.1%
  • Harisson Mwakyembe

    Votes: 2 11.1%
  • None of The above

    Votes: 0 0.0%

  • Total voters
    18
  • Poll closed .
..wanasingizia kila kitu mfumuko wa bei ya mafuta huku tumejaza Gas kutoka songosongo ambayo ingeweza kutupatia umeme wa kutosha kama kuna mipango mizuri lakini ndio kwanza kwa nusu akili zao wanaongeza mitambo ya Madiesel tuu kuzalisha umeme .....tumejaza wapumbavu watupu!
 
Akihutubia mkutano wa hadhara mjini Tunduma, Lowassa alisema kwa vile serikali iliyopo madarakani imechaguliwa kwa kura nyingi, ndiyo maana hawalali usiku na mchana kuhakikisha wanatimiza ahadi zote wazozitoa wakati wakiomba kura.

Siyo huyu EL aliyekuwa anasema anakula wakati wanafunzi kule Ukraine wanapigwa baridi nje ya ubalozi wa UK?

Alishindwa kutoa kauli kwa dakika moja ati anakula na sasa anasema halali usiku na mchana? Ama kweli machozi ya mamba.
 
Ninachoweza kusema ni kuwa ifikapo 2010 wenye akili watamkumbuka sana Benjamin Mkapa. Pamoja na yote aliyofanya huku mwishoni tunaona wazi kuwa amefanya mengi kwenye uchumi, i wonder kwanini CCM mtandao wameshindwa kufanya aliyoweza JK.

Jamaa kwelianaelekea kuwa rais ovyo, labda mabadiliko yatokee mapema anusuru hali.
 
hawalali uski na mchana wakisafiri kwenda ulaya,
tena yeye alisafiri kwenda kumaliza dili la Buzwagi, hivi ni lini Huyu jamaa atridhika.?ndio maana alipokuwa Bungeni na hoja ya Buzwagi ilipoibuka alikaa kimya, mie nilijiuliza sana kwanini Lowassa azungumzi kwa niaba ya serikali kumaliza mjadala, akawa anamuachi yule sham, benga buriani.

Kumbe aliogopa kuwa Msaliti?
hata maandiko katika wagalatia 5:20,UFISADI ni moja ya matendo yasiyo ya kiroho na automatically maFISADi wote hawaendi Mbinguni.

Mie nawaombea Mungu awapige na Matatizo tu
 
Hivi hiyo Ilani ya CCM inayozungumziwa inawezwa kuwekwa hapa kwenye bodi tuanze kuiangalia. Miaka 2 sio mbali.
 
Lowassa: Tusipotekeleza ahadi zetu mtunyonge 2010

Shedrack Sagati

WAZIRI Mkuu Edward Lowassa amesema iwapo serikali haitatekeleza ahadi walizoainisha ndani ya Ilani ya CCM, basi wananchi wawanyonge katika uchaguzi wa mwaka 2010.

Akihutubia mkutano wa hadhara mjini Tunduma, Lowassa alisema kwa vile serikali iliyopo madarakani imechaguliwa kwa kura nyingi, ndiyo maana hawalali usiku na mchana kuhakikisha wanatimiza ahadi zote wazozitoa wakati wakiomba kura.

Lowassa alitoa ahadi hiyo baada ya kuulizwa kero mbalimbali za maji pamoja na ahadi za ujenzi wa barabara ya Tunduma kwenda Sumbawanga.

Alisema barabara hiyo itawekewa lami ndani ya kipindi cha miaka mitano, kauli ambayo wananchi hawakuridhika nayo, lakini akawahakikishia kwa kueleza, “jamani yaani mnataka sisi tukisema tu leo na kesho ianze kuwekwa lami, haiwezekani ndugu zangu, lakini mtuamini kuwa tutaijenga barabara hii kwa kiwango cha lami.”

Waziri Mkuu alisema serikali iko makini kutekeleza ahadi zake na ikifika mwaka 2010 watakuwa wametekeleza kile walichoahidi. “Ikifika 2010 bila maji msiichague CCM; lakini nawahakikishia kuwa tutatekeleza ahadi zote,” alisema Waziri Mkuu.

Kuhusu maji ambayo ni moja ya kero kubwa zinazowasumbua wananchi wa eneo hilo, aliwahakikishia wananchi hao kutohofu kwani kuna miradi kadhaa ambayo imetengewa fedha ambayo itatekelezwa katika Wilaya ya Mbozi.

Awali Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge aliwaambia wananchi hao kuwa moja ya ahadi za serikali ni kuijenga barabara hiyo ambayo kwa muda mrefu imekuwa inalalamikiwa na wananchi.

“Hili tutalifanya kwani limo kwenye ilani yetu, alisema Chenge ambaye amefuatana na waziri mkuu na amekuwa anajibu maswali yote yanayoulizwa na wananchi juu ya kero za barabara.

Source: HabariLeo

Siasa kama kawaida, Ila I hope hiyo barabara itakamilika.
 
Na kuondoa ufisadi iko kwenye ilani?

kwani wewe ufisadi unafahamu vipi?

nnaona kama hiyo ilni kuna mtu naweza kutuletea hapa ni bora iletwe mie nnayo hardcopy na kuiscan itakuwa shughuli.

ila kila asubuhi huipita, baada ya kunywa chai na kusoma Quraan, huvuta ilani ya chama na kuangalia ni vipi tumeweza kuleta maendeleo ktk jamii.


tunajitahidi na serikali ya JK kwa kweli inapiga hatua nzuri, mapungufu ya kibinaadamu hayakosi.

na ahadi iko wazi tukishindwa 2010 msitupe tena nchi wapeni kina Mrema si basi
 
kwani wewe ufisadi unafahamu vipi?

nnaona kama hiyo ilni kuna mtu naweza kutuletea hapa ni bora iletwe mie nnayo hardcopy na kuiscan itakuwa shughuli.

ila kila asubuhi huipita, baada ya kunywa chai na kusoma Quraan, huvuta ilani ya chama na kuangalia ni vipi tumeweza kuleta maendeleo ktk jamii.

tunajitahidi na serikali ya JK kwa kweli inapiga hatua nzuri, mapungufu ya kibinaadamu hayakosi.

na ahadi iko wazi tukishindwa 2010 msitupe tena nchi wapeni kina Mrema si basi

Haiko kwenye website ya CCM? ata site yenyewe siijui lakini
 
hawalali usiku na mchana wanafikiri ni jinsi gani ya kuwapiga changa la macho wananchi ili wawape kura wakae madarakani mwaka 2010.

serikali ya kikwete bado haijafanya kitu, labda safari nyingi nje ya nchi.
 
Miye nimechoka kusubiri ajizi na danganya toto za kila siku. JK katamka, sifukuzi mtu, hakuna mwizi au fisadi. Mambo ni murua, sisi ni masikini hatuna mtaji, waacheni wawekezaji wavune dhahabu ingalawa twapata hata hiyo 3% ni win win situation.

Sasa twajua yeye shabiki wa Chelsea ingawa alipewa jezi ya New Castle! Kadai Dodoma ni lazima tuhamie katika miaka miwili.

Sasa najiuliza, wakati tunamshupalia koo Balali atoe siri kabla ya kwufwa, kwa nini tusiache yaliyopita aykijipika tartibu, tukaganga kwa yanayokuja 2010?

Ni mipango gani tuliyonayo kama Taifa kuhakikisha kuwa Uchaguzi wa 2010 utaleta mageuzi ya kweli kwa Taifa na si win win situation?

Mfano, Kwa nini Upinzani usimsimamishe Zimbwe kama mgombea Uraisi wao?

Kwa nini Upinzani unazubaa kujijenga kutwa japo 40% ya Bunge ili kulazimisha zile Kura za Theluthi Mbili za CCM kuwa batili kwa kushindwa?

Je katia CCM, ni nani wako tayari kuachana na Chama Cha Mafisadi na kuwa Watekelezaji wa Chama cha Mapinduzi?

We have 3 years to be constructive, otherwise February 2011, we will be talking about Ushindi wa Elnino na kusubiri Wafadhili watusaidie kuung'oa unyang'au wa CCM (Mafisadi) ambao umeboresha Umasikini, Ujinga, Njaa na Maradhi!

Kheri ya Krismas, Hannuka na Eid Mubarak!
 
By the way, I know that Zimbwe will not be able to meet the constitutional age of 40 by 2010, so if we think of him in 2015 atakuwa amechachuka and evaporated!

Lets, find a popular face to fight Kikwete in 2010!

Mbowe, Mnyika, Maalim, Mtikila, Cheyo na Zimbwe wasilianeni nami kibinafsi niwauzie mkakati!
 
dawa ni kuwang'oa tuu CCM la sivyo hakuna chochote njaa itakuwa mbele kwa mbele tuu
 
dawa ni kuwang'oa tuu CCM la sivyo hakuna chochote njaa itakuwa mbele kwa mbele tuu

Koba mimi bado nina wasiwasi, nakubaliana sana na wewe kuwa CCM ni mzizi wa matatizo yetu, lakini swali linakuja solution iko wapi? Aondolewe CCM aingie nani? Huyo atakayeingia atakuwaje, amejiandaa kiasi gani kushika dola? These are troubling questions to me.

Tulisema sana kuwa tunataka serikali isiwe ya wazee kama kina Kingunge, tulisema wengi tunakata vijana, na ndiyo maana Kikwete kwa kutumia vazi la ujana(ingawa yeye si Kijana) alipata hizo asilimia 80 ya kura zilizopigwa, ona sasa anavyotupiga bao, sasa hivi tunaona nchi inaelekea kuwa kama ya Mwinyi, uozo tu.

Labda na sisi tungeonja utawala wa kifalme.
 
Koba mimi bado nina wasiwasi, nakubaliana sana na wewe kuwa CCM ni mzizi wa matatizo yetu, lakini swali linakuja solution iko wapi? Aondolewe CCM aingie nani? Huyo atakayeingia atakuwaje, amejiandaa kiasi gani kushika dola? These are troubling questions to me.
Tulisema sana kuwa tunataka serikali isiwe ya wazee kama kina Kingunge, tulisema wengi tunakata vijana, na ndiyo maana Kikwete kwa kutumia vazi la ujana(ingawa yeye si Kijana) alipata hizo asilimia 80 ya kura zilizopigwa, ona sasa anavyotupiga bao, sasa hivi tunaona nchi inaelekea kuwa kama ya Mwinyi, uozo tu.
Labda na sisi tungeonja utawala wa kifalme.

Tuliposema vijana hakumaanisha vijana wasio na uwezo.
 
Koba mimi bado nina wasiwasi, nakubaliana sana na wewe kuwa CCM ni mzizi wa matatizo yetu, lakini swali linakuja solution iko wapi? Aondolewe CCM aingie nani?

Huyo atakayeingia atakuwaje, amejiandaa kiasi gani kushika dola? These are troubling questions to me.
Tulisema sana kuwa tunataka serikali isiwe ya wazee kama kina Kingunge, tulisema wengi tunakata vijana, na ndiyo maana Kikwete kwa kutumia vazi la ujana(ingawa yeye si Kijana) alipata hizo asilimia 80 ya kura zilizopigwa, ona sasa anavyotupiga bao, sasa hivi tunaona nchi inaelekea kuwa kama ya Mwinyi, uozo tu.

Labda na sisi tungeonja utawala wa kifalme.

Hii ndio shida ingine. Sasa hao wengine utajuaje kama uwezo wanao au hawana kama hujawapa nafasi? Wape nafasi, wakishindwa unawatimua baada ya miaka yao 5 kwisha unaweka mwingine.

Ndivyo wanavyofanya nchi zingine, why not us? Woga wa mabadiliko ndio chimbuko la aibu na kushindwa katika maisha, sio tu katika siasa, katika kila nyanja ya maisha. Sisi watanzania woga umetugharimu watanzania kuliko kitu kingine chochote. Tubadilike, na tuanza kwa kuacha woga wa kuwafukuza CCM madarakani. Hata mke au mume akikukera na kukushinda unaachana naye wala hutoi visingizio vya ooh sijapata mwingine, unless hajakuchosha.

Hata juzi ANC wamemchagua Jacob Zuma sio kwamba wanaamini anaweza sana kuongoza, bali walifanya vile kwa kumkataa Thabo. Tunapaswa kuifukuza CCM madarakani kama tunaamini imeshindwa kazi na kutuchosha, tusilete vizingizio, la sivyo tutamke tu kuwa CCM bado haijatuchosha!
 
Rev. you mean Kabwe! I've been wondering, who is this new dud on the block?

Wapinzani nao wanakatisha tamaa. Bado wapo chini mno.
Sasa hivi usiwaone akina Msekwa wapo kimya, lakini ndio mipango ya 2010 inasukwa huko.
 
Back
Top Bottom