DAKA MTUMBA
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 1,288
- 801
Ni familia ya watu saba, kapona mmoja aliyekuwa matembezini usiku.Alipofika nyumbani usiku saa 6 akakuta nyumba inawaka moto,milango yote ilikuwa imefungwa na haikuwa rahisi kuivunja.
Chanzo cha moto huo inasemekana ni shoti ya umeme.
Ndugu wote sita wamefia ndani na muda huu ndio maiti zainapelekwa hospitali.
Chanzo: Mdau aliyepo eneo la tukio!!!
Chanzo cha moto huo inasemekana ni shoti ya umeme.
Ndugu wote sita wamefia ndani na muda huu ndio maiti zainapelekwa hospitali.
Chanzo: Mdau aliyepo eneo la tukio!!!
Sina taarifa kwa kina ila ni watu ninaowajua sana. Wamefariki Mume, Mke na wajukuu. It's so Sad.
Watu sita wamekufa kwa moto baada ya nyumba inayomilikiwa na mzee David Mpili, kuteketea kwa moto huko Kipunguni Ukonga jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo Jumamosi Februari 7, 2015. Taarifa zinasema, familia hiyo ambayo ina uhusiano na waziri wa nchi ofisi ya rais kazi maalum, Profesa Mark Mwandosya iliokana na hitilafu ya umeme. Profesa Mwandosya mwenyewe ni miongoni mwa watu waliofika kwenye eneo la tukio mapema leo hii Jumamosi, ili kuwapa pole na kujionea uharibifu na maafa yaliyosababishwa na moto huo, pichani majirani ndugu jamaa na marafiki, wakiangua kilio kwenye eneo la ajali mapema leo.
Profesa Mark Mwandosya, (Mwenye suti), akiangalia uharibifu uliofanywa na moto huo, alipofika eneo la ajali mapema leo Jumamosi februari 7, 2015
Hii ndiyo hali halisi, mabaki ya nyumba hiyo yakionekana leo jumamosi Februari 7, 2015
Majirani wakiondoa mabaki ya nyumba hiyo.