Tanzania yatumia zaidi ya shilingi bilioni 60 US ndani ya miaka miwili !

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,999

Wakati serikali ya Tanzania imekuwa katika hali ya ukata wa kifedha nchini na kusababisha baadhi ya miradi na malipo mbalimbali kushindwa kufanyika serikali hiyo hiyo imekamilisha ununuzi mwingine mkubwa wa tatu wa majengo nchini Marekani ndani ya miaka miwili. Serikali ya Tanzania imekamilisha ununuzi wa jengo kubwa huko New York ambalo limegharimu dola za Kimarekani milioni 24.5 karibu sawa na shilingi bilioni 41.6 za Tanzania.


Jengo hilo jipya liitwalo Timekeeper Building (pichani) ni la ghorofa sita na lenye ukubwa wa futi 40,000 za mraba lipo jijini New York karibu na Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Jengo hilo limenunuliwa toka kampuni ya madalali wa majengo ya Amerimar ya huko Philadelphia jimbo la Pennsylvania. Kampuni ya Amerimar ilinunua jengo hilo mwaka 2005 kwa gharama ya dola milioni 15.45 kutoka kwa kampuni nyingine ya Mittman Associates. SOMA ZAIDI KWENYE FIKRAPEVU
 
Wanasema tutakodisha ofisi

Lakini kabla ya hapo tungependa kuambiwa nani kafanya cost evaluation pamoja na value evaluation

Manake uskute hiyo kitu ni kifuu tundu
 
Hakuna uhakika kama kweli ni tanzania ndo imenunua kwa sababu watanzania wala wawakilishi wao hawajaambiwa. nadhani kuna taratibu za ununuzi wa serkali je zimezingatiwa? Kabla ya kujadili kama inafaida au hapana kwanza tujiulize kama kweli hilo jengo limenunuliwa na serkali ya JMT au ni mali binafsi kwa mgongo wa serkali. Na kama ni kweli serkali ndo imenunua je taratibu zimefuatwa?
 
what is the main reason to buy a house in new york? and hili jengo litatusaidia nini haswa? nan ni watu gani hao wanaoisahuri serekali yetu kufanya manunuzi ya namna hii? je hatuna jengo la ubalozi marekani?....... kweli 40 billion TSh duh hapo unapata dawa kwenye hospitali ngapi za wilaya? madawati mangapi? maabara mangapi ya shule za sekondari? unasomesha watoto wangapi chuo kikuu ? kuna maswali najiuliza napata shida kuyajibu(kama kuna washauri serekali hii wote ciwaelewi)
 
what is the main reason to buy a house in new york? and hili jengo litatusaidia nini haswa? nan ni watu gani hao wanaoisahuri serekali yetu kufanya manunuzi ya namna hii? je hatuna jengo la ubalozi marekani?....... kweli 40 billion TSh duh hapo unapata dawa kwenye hospitali ngapi za wilaya? madawati mangapi? maabara mangapi ya shule za sekondari? unasomesha watoto wangapi chuo kikuu ? kuna maswali najiuliza napata shida kuyajibu(kama kuna washauri serekali hii wote ciwaelewi)
Tatizo la Serikali hii sio Vipaombele..........sio kwamba hawawezi kuviweka. NO.
Nobody cares as long as kila mmoja anafanya kinachompa maslahi binafsi.

Wakati watoto wa masikini wanasoma madarasa mawili kwenye chumba kimoja cha darasa.
chumba-kimoja-cha-darasa-katika-shule-ya-msingi-darpori-ambacho-kinatumika-kwa-madarasa-ya-tatu-na-nne-wanafundishwa-kwa-wakati-mmoja-na-kuleta-usumbufu-mkubwa.jpg
 
Ni idea nzuri sana ya kumiliki jengo la Ubalozi katika nchi ambayo Tz ina mwakilishi (balozi)....kwa sababu unakuwa umepunguza kwa kiasi kikubwa kodi ambayo huwa ni ya bei ya juu sana kwa mwaka kama inavyodaiwa. Lakini hii yote inatakiwa iende na vipaumbele sasa shida Serikali yetu haina vipaumbele inakurupuka tu ili mradi wamefanya.

Na kabla ya kununua jengo au chochote kwa ajili ya Ubalozi wowote popote pale lazima kufanyike mchakato wa ku-evaluate umuhimu wa kuwa na jengo hilo na kama kweli litapunguza costs, etc etc etc. na huu mchakato lazima uhusishe wawakilishi wa wananchi na uwe wazi kwa public sio mambo ya kufanyika kisiri siri. Lakini in this case, it seems nothing like that has taken place other than watu kujiekea maslahi yao binafsi. 40 Billion kwa jengo??? something isnt right somewhere.
 
Tatizo la Serikali hii sio Vipaombele..........sio kwamba hawawezi kuviweka. NO.
Nobody cares as long as kila mmoja anafanya kinachompa maslahi binafsi.

Wakati watoto wa masikini wanasoma madarasa mawili kwenye chumba kimoja cha darasa.
chumba-kimoja-cha-darasa-katika-shule-ya-msingi-darpori-ambacho-kinatumika-kwa-madarasa-ya-tatu-na-nne-wanafundishwa-kwa-wakati-mmoja-na-kuleta-usumbufu-mkubwa.jpg

Bigirita,

Hapa ndipo na mimi ninapotatizika!! Tuna matatizo lukuki tu ambayo yanahitaji immediate intervention!! MKJJ hapo juu ameongeza kuna na umeme, walisema mgao umekwisha, sasa siku hizi nasiki ndo worse, unakatika hovyo hovyo bila mpango!!

Mashule, walimu, wanafunzi wa elimu ya juu, barabara, mishahara ya watumishi, and FYI haya ni machahe tu....

Watu wanakimbilia kununua jengo NY. Najua siku wakijibu watasema gharama za mapango ni kubwa!! Sasa kwani wamejua leo ni kubwa? Au ubalozi wa TZ huko uko leo?

Commanding-In-Chief yuko zake shopping tu anapeta, akirudi huko atakuja na sera za kuhalalisha ushoga ili bakuli lake lijae, si umemsikia David!!!!
 
Hakuna uhakika kama kweli ni tanzania ndo imenunua kwa sababu watanzania wala wawakilishi wao hawajaambiwa. nadhani kuna taratibu za ununuzi wa serkali je zimezingatiwa? Kabla ya kujadili kama inafaida au hapana kwanza tujiulize kama kweli hilo jengo limenunuliwa na serkali ya JMT au ni mali binafsi kwa mgongo wa serkali. Na kama ni kweli serkali ndo imenunua je taratibu zimefuatwa?
You sound like "doubting Thomas" in your questions whose answers are available in every "kijiwe" in the country..which are a) The building has been bought by the government b)It was single sourced because of the agency stipulated in requisition to purchase c) The fund come from the budget which was passed by parliament. The question now to ask would be (and originator of the thread had asked ) Is it a priority to buy such a "lavish" structure in New York at this time? Nahisi ule msemo kupanga ni kuchagua unamaana hapa
 
kwa hilo si tatizo kwani ni uwekezaji uwekezaji mzuri na muda si mrefu wataanza kupata kodi na kuepusha matumizi yasiyo ya lazima kwa nchi yetu pindi viongozi wetu wanapokuwa huko
 
You sound like "doubting Thomas" in your questions whose answers are available in every "kijiwe" in the country..which are a) The building has been bought by the government b)It was single sourced because of the agency stipulated in requisition to purchase c) The fund come from the budget which was passed by parliament. The question now to ask would be (and originator of the thread had asked ) Is it a priority to buy such a "lavish" structure in New York at this time? Nahisi ule msemo kupanga ni kuchagua unamaana hapa

What is said in every kijiwe in the country may not reflect the reality but also remember incidences relating to ccm government foreign purchases which ended up being real scandals such as Prof. Mahalu and italian embassy, Magamba and Richmond/dowans or Mr. Chenge and Radar etc etc. Those transactions involved professional people and registered genuine foreign companies. In this country of chukua chako mapema philosophy bringing up evidences from foreign companies or parliament authorization of any government transaction does not prove anything.
 


Wakati serikali ya Tanzania imekuwa katika hali ya ukata wa kifedha nchini na kusababisha baadhi ya miradi na malipo mbalimbali kushindwa kufanyika serikali hiyo hiyo imekamilisha ununuzi mwingine mkubwa wa tatu wa majengo nchini Marekani ndani ya miaka miwili. Serikali ya Tanzania imekamilisha ununuzi wa jengo kubwa huko New York ambalo limegharimu dola za Kimarekani milioni 24.5 karibu sawa na shilingi bilioni 41.6 za Tanzania.


Jengo hilo jipya liitwalo Timekeeper Building (pichani) ni la ghorofa sita na lenye ukubwa wa futi 40,000 za mraba lipo jijini New York karibu na Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Jengo hilo limenunuliwa toka kampuni ya madalali wa majengo ya Amerimar ya huko Philadelphia jimbo la Pennsylvania. Kampuni ya Amerimar ilinunua jengo hilo mwaka 2005 kwa gharama ya dola milioni 15.45 kutoka kwa kampuni nyingine ya Mittman Associates. SOMA ZAIDI KWENYE FIKRAPEVU

Pesa zikipungua serikali itachapisha pesa mpya.
 
mmmh nina shaka hapa kama kina Ambassador Mwanaidi Majar hawajapiga cha juu...mmmh au JK huyuhuyu, mi naona ufanyike uchunguzi, labda to put record clear Comrade Mwanakijiji upo hapo Detroit, je umeshafanya uchunguzi wowote? hatutaki tume ya bunge wala nini? wala macorps wetu, na mimi naanza kufatilia week kesho tu, nitafika pale kwenye hilo jengo mpaka baada ya one week nitaleta at least half a job hapa jamvini
 
Back
Top Bottom