Tanzania human rights record

Sijali

JF-Expert Member
Sep 30, 2010
2,589
1,679
Ukichunguza utaona Tanzania mara nyingi huokoka na kunyooshewa kidole na haya mashirika ya Kimataifa ya utetezi wa haki za binadamu au ya kupinga ufisadi,vyombo vya habari vya Kimataifa n.k. Kwa kweli limekuwa ni swali nimejiuliza siku nyingi: kwa nini kitu cha ukiukaji kikitokea kama Kenya, Uganda,Congo n.k. huwa kinashughulikiwa sana na vyombo vya habari, mashirika ya Kimataifa etc, lakini siyo Tanzania? Kuna mifano mingi: mauaji ya Mwembe Chai, Zanzibar, Migodini, Arusha nk hayakusitua moyo wa huruma wa Kimataifa.
Isipokuwa mambo yanaanza kubadilika, natumai na naomba (kwani Tanzania kuna ukiukaji mkubwa na mbaya sana wa haki za binadamu).
Katika ripoti yake ya hivi karibuni, AMNESTY INTERNATIONAL, angalau imeiweka TZ katika nchi ambazo vyombo vyake vya Usalama hukiuka haki za binadamu tena pamoja na kukebehi na kutokujali(impunity). Nukuu:
" Impunity for human rights violations by law enforcement officers
was pervasive in Burundi, Cameroon, Republic of Congo, DRC, Eritrea,Ethiopia, Gambia, Guinea, Guinea-Bissau, Kenya, Madagascar,Malawi, Mozambique, Nigeria, Senegal, Sudan, Swaziland, Tanzania
and Zimbabwe"
Swali: Jee, unafikiria ni kitu gani kimegeuka/ongozeka hata AI safari hii ikaamua kuianika TZ?
 
Back
Top Bottom