Tanzania agricultural television (tatv) / channel

Sabi Sanda

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
409
31
Wakuu,

Jana kupitia TBC Taifa nilimsikia Mkulima mmoja wa Korosho akisema kuwa hawajui ni umbali gani unatakiwa uwepo kati ya mkorosho mmoja na mwingine wakati wa kupanda. Habari hii kwa kweli ilinisikitisha sana. Nchi hii kwa sasa ina upungufu wa Maafisa Ugani wasiopungua 11,000. Kama kweli tunataka kuleta mapinduzi ya kweli katika kilimo hatuna njia nyingine bali kuhakikisha kuwa wakulima wetu wanaelimika kiasi cha kutosha. Moja ya njia rahisi na yenye gharama nafuu katika kuwaelimisha wakulima wetu kwa kiwango kikubwa ni kuendesha SHAMBA DARASA kupitia njia ya Televisheni. Uwekezaji wa shilingi milioni 10 tu kila mwaka kwa miaka mitano katika kila kijiji kwa ajili ya umeme jua utatusaidia kwa kiwango kikubwa. Tunaweza kuamua kuwa na Televisheni Maalum ya Kilimo kwa ajili ya kuwafikia wakulima wetu kwa mamilioni au TBC inaweza kuwezeshwa kwa kupatiwa angalau shilingi bilioni 10 kila mwaka kwa miaka 10 na kuanzisha CHANNEL MAALUM YA KILIMO na kuhakikisha inapatikana kila kona ya nchi hii.
 
Wakuu,

Jana kupitia TBC Taifa nilimsikia Mkulima mmoja wa Korosho akisema kuwa hawajui ni umbali gani unatakiwa uwepo kati ya mkorosho mmoja na mwingine wakati wa kupanda. Habari hii kwa kweli ilinisikitisha sana. Nchi hii kwa sasa ina upungufu wa Maafisa Ugani wasiopungua 11,000. Kama kweli tunataka kuleta mapinduzi ya kweli katika kilimo hatuna njia nyingine bali kuhakikisha kuwa wakulima wetu wanaelimika kiasi cha kutosha. Moja ya njia rahisi na yenye gharama nafuu katika kuwaelimisha wakulima wetu kwa kiwango kikubwa ni kuendesha SHAMBA DARASA kupitia njia ya Televisheni. Uwekezaji wa shilingi milioni 10 tu kila mwaka kwa miaka mitano katika kila kijiji kwa ajili ya umeme jua utatusaidia kwa kiwango kikubwa. Tunaweza kuamua kuwa na Televisheni Maalum ya Kilimo kwa ajili ya kuwafikia wakulima wetu kwa mamilioni au TBC inaweza kuwezeshwa kwa kupatiwa angalau shilingi bilioni 10 kila mwaka kwa miaka 10 na kuanzisha CHANNEL MAALUM YA KILIMO na kuhakikisha inapatikana kila kona ya nchi hii.

Sabi Sanda, unaona mbali, TBC inamwaga channel zaidi ya 100 hivi karibuni, sio jumu tena la TBC kuanzisha kipindi, bali kilas wizara inakuwa na programu yake, kila mamlaka ya mazao inakuwa na programu yake kama ilivyo DSTV, hadi JF, tukiamu tunakwenda hewani. Zile podcast kama za Mzee Mwanakijiji, na ma online radio kibao ikiwemo Bongo Radio, sasa ni kwa wote, tatizo sio bure bakli kwa Decoda, inalipiwa elfu 5,000 tuu!.
 
Sabi Sanda, unaona mbali, TBC inamwaga channel zaidi ya 100 hivi karibuni, sio jumu tena la TBC kuanzisha kipindi, bali kilas wizara inakuwa na programu yake, kila mamlaka ya mazao inakuwa na programu yake kama ilivyo DSTV, hadi JF, tukiamu tunakwenda hewani. Zile podcast kama za Mzee Mwanakijiji, na ma online radio kibao ikiwemo Bongo Radio, sasa ni kwa wote, tatizo sio bure bakli kwa Decoda, inalipiwa elfu 5,000 tuu!.

Hii imetulia..Tutakuwa tumekwenda mbali kihabari na Tanzania yetu.
 
Sawa wazo zuri.Lakini tatizo litakuwa ni uendeshaji tu.kwa sababu kama kukitu wa-Tz kinacho tu shinda basi ni Management ya Miradi.
 
Sawa wazo zuri.Lakini tatizo litakuwa ni uendeshaji tu.kwa sababu kama kukitu wa-Tz kinacho tu shinda basi ni Management ya Miradi.

Kwa kweli nimeamini kuwa KILIO NA SAUTI YA WENGI NI SAUTI YA MUNGU.

Hatuna njia bila televisheni na redio maalum za elimu safari yetu ya maendeleo itakuwa ndefu kupita kiasi.

Pasco, asante sana kwa hiyo update. Wengine tumeandika sana kuhusu hili. Inatia moyo kuona kuwa sasa Serikali imekubali kutumia Televisheni kufundisha wanafunzi wetu wakianzia na wale wa sekondari. Bila shaka tutafika.
 
Sabi Sanda, unaona mbali, TBC inamwaga channel zaidi ya 100 hivi karibuni, sio jumu tena la TBC kuanzisha kipindi, bali kilas wizara inakuwa na programu yake, kila mamlaka ya mazao inakuwa na programu yake kama ilivyo DSTV, hadi JF, tukiamu tunakwenda hewani. Zile podcast kama za Mzee Mwanakijiji, na ma online radio kibao ikiwemo Bongo Radio, sasa ni kwa wote, tatizo sio bure bakli kwa Decoda, inalipiwa elfu 5,000 tuu!.

Pasco,

Hebu tupe update ya hizo channels toka TBC.
 
Back
Top Bottom