Sabi Sanda
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 409
- 31
Wakuu,
Jana kupitia TBC Taifa nilimsikia Mkulima mmoja wa Korosho akisema kuwa hawajui ni umbali gani unatakiwa uwepo kati ya mkorosho mmoja na mwingine wakati wa kupanda. Habari hii kwa kweli ilinisikitisha sana. Nchi hii kwa sasa ina upungufu wa Maafisa Ugani wasiopungua 11,000. Kama kweli tunataka kuleta mapinduzi ya kweli katika kilimo hatuna njia nyingine bali kuhakikisha kuwa wakulima wetu wanaelimika kiasi cha kutosha. Moja ya njia rahisi na yenye gharama nafuu katika kuwaelimisha wakulima wetu kwa kiwango kikubwa ni kuendesha SHAMBA DARASA kupitia njia ya Televisheni. Uwekezaji wa shilingi milioni 10 tu kila mwaka kwa miaka mitano katika kila kijiji kwa ajili ya umeme jua utatusaidia kwa kiwango kikubwa. Tunaweza kuamua kuwa na Televisheni Maalum ya Kilimo kwa ajili ya kuwafikia wakulima wetu kwa mamilioni au TBC inaweza kuwezeshwa kwa kupatiwa angalau shilingi bilioni 10 kila mwaka kwa miaka 10 na kuanzisha CHANNEL MAALUM YA KILIMO na kuhakikisha inapatikana kila kona ya nchi hii.
Jana kupitia TBC Taifa nilimsikia Mkulima mmoja wa Korosho akisema kuwa hawajui ni umbali gani unatakiwa uwepo kati ya mkorosho mmoja na mwingine wakati wa kupanda. Habari hii kwa kweli ilinisikitisha sana. Nchi hii kwa sasa ina upungufu wa Maafisa Ugani wasiopungua 11,000. Kama kweli tunataka kuleta mapinduzi ya kweli katika kilimo hatuna njia nyingine bali kuhakikisha kuwa wakulima wetu wanaelimika kiasi cha kutosha. Moja ya njia rahisi na yenye gharama nafuu katika kuwaelimisha wakulima wetu kwa kiwango kikubwa ni kuendesha SHAMBA DARASA kupitia njia ya Televisheni. Uwekezaji wa shilingi milioni 10 tu kila mwaka kwa miaka mitano katika kila kijiji kwa ajili ya umeme jua utatusaidia kwa kiwango kikubwa. Tunaweza kuamua kuwa na Televisheni Maalum ya Kilimo kwa ajili ya kuwafikia wakulima wetu kwa mamilioni au TBC inaweza kuwezeshwa kwa kupatiwa angalau shilingi bilioni 10 kila mwaka kwa miaka 10 na kuanzisha CHANNEL MAALUM YA KILIMO na kuhakikisha inapatikana kila kona ya nchi hii.