Tamaa za ngono haziwezi kuondolewa na maombi ama maombezi

Kambi ya Fisi

JF-Expert Member
Feb 3, 2018
13,514
21,997
Hii inawahusu wote wanahangaika kutafuta maombezi kwa mitume na manabii kwamba waombewe ili tamaa za ngono itoweke nawaombeni mjifunze kitu hapa.

Mpendwa usihangaike kukusanya sadaka ya Kumpelekea nabii eti akufungue uache ngono, hakuna kitu kama hicho. Hata huyo nabii unayetaka akuombee huwa anakutamani akuonje na ukizubaa kidogo tunda linaliwa tena sio kimasihara bali kwa kukusudia.

Iko hivi..... Mungu haondoagi tamaa zetu za ngono kwa sababu ngono ni hitaji lililo rasmi la mwili. Hii ni kama vile ilivyo kwa Mungu kutoondoa hitaji letu la chakula hivyo kaweka njaa ili tule na tushibe.

Haja ya ngono imejengwa na Mungu mwenyewe ndani ya mwili wa mwanadamu kwa makusudi maalum hivyo hata kukemea roho ya uasherati hakuwezi kukuweka safi kingono unaweza kwenda na maji siku upwiru ukikomaa na wewe.

Jifunze kitu kwa mfano huu.... Yesu alimsamehe mwanamke ambaye alikamatwa katika tendo la uzinzi, alimhoji maswali machache tu kisha akamtangazia msamaha na akamshauri aache(asitende) dhambi (uzinzi) tena. Hapo Yesu alimaanisha uzinzi ni chaguo, na SIO pepo mchafu. Iwapo uzinzi lingekuwa pepo, basi Yesu angelikemea kwa wema ili limtoke huyo mwanamke, hakufanya hivyo kwa sababu uzinzi ama kuwa uzinzi ni chaguo la mtu na sio la pepo mchafu.

Wa kulala naye huwa ni chaguo la mhusika. Ndiyo maana Mungu anatuamuru tuwe wanyoofu kingono. Anasema, "Usizini." Iwe umeoa au umeolewa, Mungu anasema, “Ikimbieni zinaa - 1 Wakorintho 6:18.

Ikiwa hujaoa ama kuolewa na unawaka tamaa kupeleka ama kupelekewa moto mara kwa mara, ni vyema ukichukua hatua ya kupata mwenza na ukafunga naye ndoa muendelee kupelejeana moto kihalali (1Kor 7:8-9).

Ikiwa umeoa /umeolewa, heshimu ndoa yako na uweke kitanda chako kiwe safi (Ebr 13:4). Hivyo kila mtu anaweza kudhibiti hamu yake ya ngono kwa kuheshimu ndoa yake.

Biblia inakazia njia moja ya kuepukana na uasherati nayo ni kufanya ngono mara kwa mara katika ndoa, kwa maana hakuna kunyimana (1Kor 7:2-5).

Sasa basi kumwombea mtu aache ngono ni sawa na Kumwombea mtu akose chakula, ombezi hilo huwa haliwezeshwi na mungu.

Ubarikiwe.
 
Matatizo mengi ya tabia za watu huwa yanapewa majina ya kiroho ili kusingizia mapepo kuwa ni chanzo wakati si kweli.

Tabia za hovyo au nzuri za mtu ni matokeo ya chimbuko lake yaani makuzi aliyopitia tokea akiwa kichanga au asili ya tabia za wazazi wake.

Unakuta mtu anatabia za umalaya hasikii wala kurekebishwa tabia yake unasingizia mapepo, wewe chunguza wazazi wake na familia alipotokea utapata majibu yako.

Ni nadra sana wazazi wenye maadili na misimamo ya misingi bora ya kifamilia kulea na kukuza mtoto mwenye tabia za hovyo ambazo hazivumiliki.
 
Kwa Yesu hakuna lisilowezekana...

Mwanamke kahaba baada ya kuombewa na Yesu aliacha
Tofautisha Kahaba na malaya. Kahaba anaweza kuacha maana kwake si furaha kuruka na wanaume kama njia ya kujikimu.

Maana hata ukichunguza wanawake wa sasa kwa asilimia 99% mnaolewa kwasababu za kikahaba yaani mwanaume aishi na wewe akikulipia gharama za mahitaji yako kwa mshahara wa kumpa huduma za mahaba ikiwapo unyumba kitandani na si kwamba na wewe umpe yeye anything interms of gharama za maisha.


So kimsingi, wanawake wapo malaya na makahaba.
 
Luka 7: 36-50
Mwanamke anayezungumziwa hapa dhambi zake hazitajwi ni zipi, ni kweli Yesu alimsamehe dhambi ila hakukemea mapepo kwa huyo mwanamke kwa sababu hakuwa na mapepo.
Mariamu Magdalena mwanamke
Mariam Magdalena ndiye aliyekuwa na mapepo 7 na yalikemewa na Yesu hadi yakamtoka yote na baada ya hapo akawa ni mfuasi wa Yesu, habari za Mariam Magdalena unaweza kuzisoma Luka 8:2 na kuendelea.

Kwa hao wanawake wawili Biblia haiwataji kuwa walikuwa na mapepo ya ngono au ya ukahaba.

Nikuombe tu ukubali kwamba tamaa ya ngono haiondolewi kwa maombezi maana hata Yesu hakudili na hilo tatizo kwa njia ya maombezi bali wenye shida kama hizo aliwashauri tu wafanye nini, na hata mtume Paulo alifanya kama alivyofanya Yesu yaani alitoa tu ushauri.
 
Mwanamke anayezungumziwa hapa dhambi zake hazitajwi ni zipi, ni kweli Yesu alimsamehe dhambi ila hakukemea mapepo kwa huyo mwanamke kwa sababu hakuwa na mapepo.
Mariam Magdalena ndiye aliyekuwa na mapepo 7 na yalikemewa na Yesu hadi yakamtoka yote na baada ya hapo akawa ni mfuasi wa Yesu, habari za Mariam Magdalena unaweza kuzisoma Luka 8:2 na kuendelea.

Kwa hao wanawake wawili Biblia haiwataji kuwa walikuwa na mapepo ya ngono au ya ukahaba.

Nikuombe tu ukubali kwamba tamaa ya ngono haiondolewi kwa maombezi maana hata Yesu hakudili na hilo tatizo kwa njia ya maombezi bali wenye shida kama hizo aliwashauri tu wafanye nini, na hata mtume Paulo alifanya kama alivyofanya Yesu yaani alitoa tu ushauri.
Sidhani kama unaelewa maana halisi ya Yesu kufa msalabani...

Hakika kama ungeelewa usingeandika hili uliloandika...

Hapa inaonyesha vile huamini kifo chake kilivyomaliza yote pale msalabani...

Maana inaonyesha vile unamuangalia Yesu kama mwanadamu..
 
Sidhani kama unaelewa maana halisi ya Yesu kufa msalabani...

Hakika kama ungeelewa usingeandika hili uliloandika...

Hapa inaonyesha vile huamini kifo chake kilivyomaliza yote pale msalabani...

Maana inaonyesha vile unamuangalia Yesu kama mwanadamu..
Naomba. Nieleweshe Donatila , kifo cha yesu pale golgota na kuwakwa tamaa za ngono, kama mtoa bandiko alivyoelezea
 
Back
Top Bottom