Sokomoko
JF-Expert Member
- Mar 29, 2008
- 1,915
- 127
Takukuru yaenguliwa Timu ya EPA
Na Mwandishi wetu
BAADA ya Timu Maalum ya Rais ya kuchunguza wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje katika Benki Kuu ya Tanzania (EPA) kukabidhi taarifa yake kwa Rais Jakaya Kikwete mwezi uliopita, taasisi mojawapo kati ya tatu zilizohusika imeenguliwa.
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imeengiliwa kwa agizo kutoka juu.
Hatua hiyo imechukuliwa na serikali ngazi ya juu kunatokana na mchango wa tasisi anayoiwakili mjumbe huyo kuonekana mdogo.
Timu hiyo inatakiwa kukamilisha kazi yake mwishoni mwa mwezi ujao kama ilivyoelekezwa na Rais Kikwete.
Kazi zilizobaki kwa timu hiyo ni pamoja na kusimamia urejeshwaji wa sh11 bilioni kutoka kwa makampuni yaliyohusika na ubadhilifu huo ndani ya Benki Kuu.
Pamoja na kubakia na kazi hiyo, timu hiyo imebaki na jukumu la kusimamia upatikanaji wa taarifa zitakazosaidia serikali kupata taarifa za makampuni ambayo yameficha mali zake nje ya nchi kwa kutumia ushirikiano wa polisi wa kimataifa Interpol.
Taarifa za ndani ya serikali zinaonyesha kuwa Takukuru wameondoshwa katika timu iliyokuwa ikiongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika Mkuu wa jeshi la Polisi nchini, Said Mwema pamoja na Mkurugenzi wa Takukuru, Edward Hosea.
Taasisi hiyo imeondolewa, haijajulikana bayana kama ni Rais Jakaya Kikwete ndiye alitoa maamuzi hayo.
Kimsingi ni kama Takukuru iliondoshwa katika mchakato huu katika hatua za mwisho, wakati timu ilikuwa inaandaa ripoti kwa ajili ya kuifikisha kwa Rais kama ilivyokuwa imeelekezwa, kilisema chanzo chetu.
Aidha chanzo hicho kilisema kitendo cha kuondoshwa kwa taasisi hiyo nyeti pengine inatokana na kazi za msingi za kamati hiyo kumalizika na kubakia majukumu ya kuwapeleka watuhumiwa mahakamani pamoja na kuwafuatilia walioficha mali nje ya nchi.
Chanzo chetu kinasema lengo kubwa la kuwahusisha Takukuru ilikuwa ni kutumia uwezo wao wa kiuchunguzi kuisaidia timu hiyo kuharakisha mambo zaidi.
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa huenda Takukuru wameondolewa katika timu hiyo kutokana na kuvuja kwa kazi iliyokuwa ikifanyika.
Baadhi ya siri za timu hiyo ilikuwa inaoongozwa na mwanasheria mkuu wa serikali zilikuwa zinavuja kila baada ya kikao, hivyo kuipa timu wakati mgumu wa kuendelea na kazi waliyopewa, alisema.
Pamoja na fununu hizo, lakini pia habari za uhakika zinasema hata mipango ya kuwasiliana na Interpol zimekuwa zinafanywa na watu wawili tu, ukimwondoa Hosea.
Akihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dodoma, Rais Kikwete alisema timu ilikuwa imekusanya Sh 53,738,835,392
Aidha Rais Kikwete alisema timu hiyo pia iliwabana baadhi ya watuhumiwa na kwamba wapo ambao wamekubaliana mpaka hadi Oktoba 31 mwaka huu wawe wameshalipa.
Hali hiyo inaonyesha kuwa tayari kazi ambayo ilitakiwa kufanywa na Takukuru kwa kushirikiana na vyombo vingine ilikuwa imekamilika na kwamba mpaka hapo timu ilipofikia wanaweza kufanya kazi bila Takukuru.
Source: Mwananchi
Na Mwandishi wetu
BAADA ya Timu Maalum ya Rais ya kuchunguza wizi wa fedha kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje katika Benki Kuu ya Tanzania (EPA) kukabidhi taarifa yake kwa Rais Jakaya Kikwete mwezi uliopita, taasisi mojawapo kati ya tatu zilizohusika imeenguliwa.
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imeengiliwa kwa agizo kutoka juu.
Hatua hiyo imechukuliwa na serikali ngazi ya juu kunatokana na mchango wa tasisi anayoiwakili mjumbe huyo kuonekana mdogo.
Timu hiyo inatakiwa kukamilisha kazi yake mwishoni mwa mwezi ujao kama ilivyoelekezwa na Rais Kikwete.
Kazi zilizobaki kwa timu hiyo ni pamoja na kusimamia urejeshwaji wa sh11 bilioni kutoka kwa makampuni yaliyohusika na ubadhilifu huo ndani ya Benki Kuu.
Pamoja na kubakia na kazi hiyo, timu hiyo imebaki na jukumu la kusimamia upatikanaji wa taarifa zitakazosaidia serikali kupata taarifa za makampuni ambayo yameficha mali zake nje ya nchi kwa kutumia ushirikiano wa polisi wa kimataifa Interpol.
Taarifa za ndani ya serikali zinaonyesha kuwa Takukuru wameondoshwa katika timu iliyokuwa ikiongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika Mkuu wa jeshi la Polisi nchini, Said Mwema pamoja na Mkurugenzi wa Takukuru, Edward Hosea.
Taasisi hiyo imeondolewa, haijajulikana bayana kama ni Rais Jakaya Kikwete ndiye alitoa maamuzi hayo.
Kimsingi ni kama Takukuru iliondoshwa katika mchakato huu katika hatua za mwisho, wakati timu ilikuwa inaandaa ripoti kwa ajili ya kuifikisha kwa Rais kama ilivyokuwa imeelekezwa, kilisema chanzo chetu.
Aidha chanzo hicho kilisema kitendo cha kuondoshwa kwa taasisi hiyo nyeti pengine inatokana na kazi za msingi za kamati hiyo kumalizika na kubakia majukumu ya kuwapeleka watuhumiwa mahakamani pamoja na kuwafuatilia walioficha mali nje ya nchi.
Chanzo chetu kinasema lengo kubwa la kuwahusisha Takukuru ilikuwa ni kutumia uwezo wao wa kiuchunguzi kuisaidia timu hiyo kuharakisha mambo zaidi.
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa huenda Takukuru wameondolewa katika timu hiyo kutokana na kuvuja kwa kazi iliyokuwa ikifanyika.
Baadhi ya siri za timu hiyo ilikuwa inaoongozwa na mwanasheria mkuu wa serikali zilikuwa zinavuja kila baada ya kikao, hivyo kuipa timu wakati mgumu wa kuendelea na kazi waliyopewa, alisema.
Pamoja na fununu hizo, lakini pia habari za uhakika zinasema hata mipango ya kuwasiliana na Interpol zimekuwa zinafanywa na watu wawili tu, ukimwondoa Hosea.
Akihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dodoma, Rais Kikwete alisema timu ilikuwa imekusanya Sh 53,738,835,392
Aidha Rais Kikwete alisema timu hiyo pia iliwabana baadhi ya watuhumiwa na kwamba wapo ambao wamekubaliana mpaka hadi Oktoba 31 mwaka huu wawe wameshalipa.
Hali hiyo inaonyesha kuwa tayari kazi ambayo ilitakiwa kufanywa na Takukuru kwa kushirikiana na vyombo vingine ilikuwa imekamilika na kwamba mpaka hapo timu ilipofikia wanaweza kufanya kazi bila Takukuru.
Source: Mwananchi