TAHADHARI: Ongezeko la Mvua

n00b

JF-Expert Member
Apr 10, 2008
1,006
2,667
Wakuu hali ya hewa inasomeka kitahadhari zaidi.
Kuna tishio la ongezeko la mvua muda mchache ujao.... soma taarifa ya Hali ya Hewa hapo chini

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAWIZARA YA UCHUKUZI
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

Simu: 255 22 2460735/2460706
FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056
Simu pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM
Tovuti: www.meteo.go.tz
Unapojibu tafadhali nakili:
Kumb. Na.: TMA/1622 Imetolewa: 31 Oktoba, 2012
TAARIFA YA ONGEZEKO LA MVUA
Taarifa Na. 20121031-01
Muda wa Kutolewa
Saa za Afrika Mashariki
Saa 10:30 Alasiri
Daraja la Taarifa:
1:Taarifa 2:Ushauri
3:Tahadhari
4:Tahadhari Kubwa:
Taarifa
Aina ya Tukio
Linalotarajiwa
Ongezeko la mvua
EneoKatika baadhi maeneo ya mikoa ya Mara, Mwanza, Shinyanga,
Geita,Simiyu, Singida, Dodoma, Rukwa, Tabora, Njombe, Iringa na
Mbeya
MaelezoKatika kipindi cha siku mbili zijazo (1-2/11/2012) kunatarajiwa
kuwa na vipindi vya mvua kubwa katika baadhi ya maeneo ya mikoa
tajwa hapo juu. Hali hii inatokana na kuwepo kwa viashiria vya
ongezeko la unyevunyevu angani sambamba na kuwepo kwa
makutano ya upepo katika maeneo hayo.
Maelezo ya ziadaHii ni taarifa ya awali, Mamlaka ya Hali ya Hewa inaendelea
kufuatilia mabadiliko ya mifumo ya hali ya hewa na itatoa taarifa
zaidi kwa kadri zitakavyo patikana
Imetolewa na
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
View attachment TAHADHARI _31-10-2012.pdf
 
Mamlaka ya Hali ya Hewa ni kama mganga wa kienyeji tu.............kesho Simba inaifunga Yanga, matokeo Simba inafungwa.
Nasubiri mamlaka hiyo itutabirie Rais ajaye wa nchi hii ni nani, maana kazi hiyo wataiweza vizuri sana na vyombo wanavyo.

Kibanga Msese
 
Mamlaka ya Hali ya Hewa ni kama mganga wa kienyeji tu.............kesho Simba inaifunga Yanga, matokeo Simba inafungwa.
Nasubiri mamlaka hiyo itutabirie Rais ajaye wa nchi hii ni nani, maana kazi hiyo wataiweza vizuri sana na vyombo wanavyo.

Kibanga Msese

Kwani wao si wanatabiri hali ya hewa??
 
Mamlaka ya Hali ya Hewa ni kama mganga wa kienyeji tu.............kesho Simba inaifunga Yanga, matokeo Simba inafungwa.


Kwani wao si wanatabiri hali ya hewa??

Mzee mwenzangu ushasahau mara hii kuwa kuna Rais wa ile nchi ya ndoto (ati Zanzibar sijui) alipoteza urais kutokana na kuchafuka kwa hali ya hewa 1984?Mimi nilimsikia Nyerere akisema RTD......Ni hawahawa TMA walitabiri
 
Ushaambiwa ninutabiri so yaweza tokea au isitokee ila mbona USA walitabiri Sandy na ikatokea why not us
we need to invest in that!
 
Unapoambiwa utabiri ujue ni utabiri si halisi tahadhari ni muhimu ndugu zangu wamaJF. Asante kwa mtoa habari hii
 
Mamlaka ya Hali ya Hewa ni kama mganga wa kienyeji tu.............kesho Simba inaifunga Yanga, matokeo Simba inafungwa.
Nasubiri mamlaka hiyo itutabirie Rais ajaye wa nchi hii ni nani, maana kazi hiyo wataiweza vizuri sana na vyombo wanavyo.

Kibanga Msese

Mvua ya Lowasa iliishia wapi kwani ile isingehitaji utabiri wa hali ya hewa na isingekuwa na mafuriko.
 
Hivi hawa watu huwa kweli serikali yetu inawatengea hela za mishahara ya kazi gani hasa,wapuuzi sana
 
Big up Mamlaka ya Hali ya Hewa. Dodoma mvua imenyesha tena ni baada ya ukame wa muda mrefu tangu msimu uliopita. Hongereni kwa kazi nzuri.
 
Back
Top Bottom