Gazeti la RAI lilichapisha utafiti ambao ulileta mashaka kwa wengi na kupotosha kwa kiasi kikubwa kuhusu atakayeshinda uchaguzi wa arumeru mashariki.Tunawaomba mara baada ya uchaguzi kufanyika na mshindi aliyetangazwa kujulikana,ambaye ni tofauti na matokeo ya utafiti wao sasa wajitokeze na kuwaomba radhi wasomaji wa gazeti lao.Vinginevyo wamepoteza imani ya wengi wa wasomaji wa gazeti hili ambao hawapendi kuona gazeti la uchambuzi kama hili linapoteza mwelekeo na kutoa habari ambazo hazijengi kukuza demokrasia nchini.