Taarifa ya Mahakama kuhusu Makala ya Gazeti la Mwananchi "Mtandao wa Rushwa Mahakamani"

Maboso

JF-Expert Member
Feb 18, 2013
5,164
5,761
attachment.php

TAARIFA KWA UMMA


MAKALA YA GAZETI LA MWANANCHI YA TAREHE 21-07-2015 YENYE KICHWA CHA HABARI "MTANDAO WA RUSHWA MAHAKAMANI HUU HAPA"



1. UTANGULIZI



NAFASI YA VYOMBO VYA HABARI MAKALA MAALUM YA GAZETI LA MWANANCHI LA TAREHE 21/07/2015 UK. 25 - 26


Mahakama ya Tanzania inatambua nafasi ya vyombo vya habari katika kuwafikishia wananchi habari na kuwaelimisha. Vile vile tunatambua nafasi ya kipekee ya vyombo vya habari katika kukosoa utendaji wa taasisi za umma na binafsi. Kwa kutambua hilo Mahakama imeunda jukwaa la mahakama na vyombo vya habari (Judiciary- Media forum)

USHIRIKIANO WA MAHAKAMA NA VYOMBO VYA HABARI
Katika kudhihirisha dhamira yake ya kushirikiana na vyombo vya habari ili kuboresha huduma na utoaji habari, tarehe 3/12/2014 Mahakama iliandaa kongamano la kujadili changamoto zinazoikabili pamoja na nafasi ya vyombo vya habari. Kongamano hili lilihusisha wahariri wa vyombo vyote vya habari. Katika kongamano hilo, pamoja na mambo mengine, tulikubaliana yafuatayo:-

  • Kuimarisha ushirikiano kwa kupeana taarifa muhimu
  • Mahakama kutoa ufafanuzi wa masuala yasiyoeleweka kwa waandishi wa habari ili kuepusha upotoshaji
  • Kushirikiana katika kujengeana uwezo wa kuandika habari za mahakama.

UTEKELEZAJI WA MAKUBALIANO


Mahakama inatekeleza makubaliano haya kwa kutoa taarifa na maelezo ya kina kuhusu masuala mbalimbali hasa ya kesi zinazoendelea mahakamani. Mahakama inafanya hivyo kwa ufanisi zaidi pale ambapo mtaka taarifa anataja namba ya kesi na mahakama ilipo kesi au mtumishi anayelalamikiwa. Bila kutolewa kwa taarifa hizi ni vigumu kwa mahakama kuchukua hatua.

2. UMUHIMU WA TAARIFA HII


Katika gazeti la Mwanachi la tarehe 21/07/2015 ukurasa wa 25 na 26 kulikuwa na habari yenye maneno "Mtandao wa rushwa Mahakamani huu hapa." Katika habari hiyo Mwandishi ametoa tuhuma kwamba kuna rushwa Mahakamani kwa kutolea mifano kama ifuatavyo:-

2.1 Bw. Muhidini Ngulumwa, anashitakiwa kwa jinai katika Mahakama ya Mwanzo Magomeni lakini mlalamiko hafiki Mahakamani kwa miaka mitatu sasa ambapo pia aliombwa rushwa ya shilingi laki tano.


  • Bi. Kuruthum Majjid, alitoa rushwa ya laki moja ili Polisi wamkamate mtuhumiwa. Mtuhumiwa alifikishwa katika Mahakama ya Mwanzo Mogomeni ambapo amepewa dhamana lakini haudhurii Mahakamani kwa muda wa miezi kumi na tatu sasa.
  • Bw.Abdallaha Majata, kesi yake inazungushwa mahakama ya Mwanzo Mbagala kwa madai kuwa uchunguzi haujakamalika na kwamba kuna mshauri wa Mahakama anamwomba wamalize kesi nje ya Mahakama.
  • Bi. Halima Abdan, ametoa fedha polisi na Mahakamani kuwezesha ndugu yake apewe dhamana bila mafanikio. Mwandishi hakutaja Mahakama ilipo kesi husika.
  • Bw. Claudiana Mbazigwa, amepoteza milioni moja na laki nne katika jitihada ya kumdhamini ndugu yake katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo bila mafanikio.
  • Bw. Abdallh Mpondela amepoteza laki tano akijaribu kumdhamini ndugu yake bila mafanikio Mwandishi hajataja Mahakama ilipo kesi husika.
  • Bw. Laizer Kaanan ametoa shilingi laki sita katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo ili kumdhamini ndugu yake bila mafanikio.

3.0. UFUATILIAJI WA TUHUMA

Mahakama imeguswa na kusikitishwa na tuhuma hizi. Kwa vile kesi katika Mahakama husajiliwa kwa nambari za usajili kwa ajili ya utambulisho, na kwa vile katika Makala Mwandishi hataji namba za kesi na kwa kuzingatia uzito wa habari yenyewe, Mahakama imeanza uchunguzi juu ya tuhuma hizi kwa hatua zichukuliwe na Idara ya Ukaguzi wa Huduma za Mahakama na Maadili kwenda ofisi za gazeti la Mwananchi (tarehe 22/7/2015) kupata taarifa zitakazowezesha kuchukuliwa hatua.

Hadidu za rejea zifuatazo zilitumika:-

  1. Kufahamu iwapo mwandishi wa makala anafahamu anuani au namba za simu za walalamikaji ili wasaidie kutoa taarifa zaidi ikiwa ni pamoja na nambari za kesi kwa ajili ya uchunguzi na hatua zifaazo.
  2. Kufahamu iwapo mwandishi wa makala anafahamu nambari za kesi za matukio aliyoandika.
  3. Kufahamu iwapo mwandishi anawafahamu au ana anuani au namba za simu za wazee wa baraza aliohojiana nao.
  4. Kufahamu iwapo mwandishi alipata namba za simu ya askari aliyezungumza na Halima Abdan baada ya kuunganishwa na mzee wa baraza.
  5. Kupata maelezo ya aina ya uchunguzi aliofanya mwandishi ili kujiridhisha na ukweli wa habari.

4.0. MATOKEO YA UCHUNGUZI

Katika ofisi za gazeti la Mwananchi Ofisa wa ngazi za juu wa Mahakama alikutana na Bw. Joster Mwangulumbi ambaye ni Mhariri wa Habari za uchunguzi. Bw. Joster alimfahamisha Mkurungenzi Msaidizi mambo yafuatayo:-

  • Mwandishi wa makala hayo (Bi. Kalunde Jamal ) yuko safarini na asingepatikana kwa mahojiano lakini alimpigia simu wakaongea kuthibitisha masuala kadhaa.
  • Mwandishi wa makala ni mwandishi wa habari za Mahakama na katika kufanya kazi zake alipata malalamiko aliyoyatolea taarifa ofisini akatakiwa kufanya uchunguzi na matokeo ya uchunguzi ndiyo yaliyochapishwa.
  • Katika ufuatiliaji Mahakimu Wafawidhi wa Mahakama za Mwanzo na Wilaya hawakuwa tayari kuzungumzia na kufafanua malalamiko hayo.
  • Ofisi za gazeti na Mwananchi na mwandishi wa makala hawafahamu nambari za kesi zinazolalamikiwa, anuani na hata namba za simu za walalamikaji waliotajwa. Pia hawana namba za simu za wazee wa baraza au askari polisi aliyewasiliana na Halima Abdan na kwamba hawawezi kupata anuani au namba za simu hizo.

Mapungufu haya yanaleta mashaka juu usahihi wa taarifa zilizoandikwa katika makala hayo. Licha ya upungufu wa dhahiri ambao hauiwezeshi Mahakama kuchukua hatua zozote, katika toleo la tarehe 22/07/2015 gazeti hili lilitoa tahariri yenye kusisitiza yaliyomo katika makala yenye utata ila yenye kuvutia.

5.0. HARAKATI ZA MAHAKAMA KUBORESHA

5.1. HATUA ZA KUBORESHA HUDUMA

Mahakama inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kuboresha huduma zake. Mahakama pia kama Taasisi ya Umma iko tayari na imekwisha toa fursa kwa wadau kutoa maoni yao kuhusu namna ya kuboresha huduma zake kupitia matangazo kwenye magazeti Mwananchi la tarehe 29/5/2015 na Mtanzania la tarehe 03/6/2015 ambapo maoni yanaendelea kupokelewa. Mahakama pia iko tayari kukosolewa kwa njia zote halali kwa lengo la kuboresha huduma, ili mradi taarifa hizo ziweze kusaidia kuchukua hatua kwa sasa na kuwa kama chachu ya mabadiliko/mageuzi yanayoendelea ndani ya Taasisi hii muhimu ya uendeshaji wa Nchi yetu.

5.2. WITO KWA WANANCHI NA WADAU

Ili kuondoa kero zilizobainishwa na gazeti la Mwananchi, Mahakama inatoa rai kwa gazeti la Mwananchi au mtu yeyote mwenye taarifa sahihi kuipatia ushirikiano ili kupata nambari za kesi zilizolalamikiwa na mahakama zilikofunguliwa.

Kwa lengo hilo la ushirikiano Mahakama inaomba wale wote waliotajwa katika makala iliyochapishwa tarehe 21/07/2015 kuhusu mtandao wa rushwa Mahakamani (Kama wapo) ambao ni Muhidini Ngulumwa, Kuruthum Majjid, Abdallah Majata, Halima Abdan, Claudiana Mbazigwa, Abdallah Mpondela na Laizer Kaanan wafike Makao Makuu ya Mahakama, Mahakama ya Rufani ya Tanzania, No 11409 Kivukoni Front, waonane na Mkurungenzi Msaidizi wa Malalamiko katika Idara ya Ukaguzi wa Huduma za Mahakama na Maadili ili watatuliwe kero zao. Inasisitiza tena ili kuondoa rushwa, maadili yasiyofaa huduma suala la uwazi wa utoaji huduma na kuboresha mawasiliano ni muhimu kuanzia tarehe 6 Desemba, 2014.

Mahakama imeweka namba ya simu Na. 0752- 500 400 ambayo inapokea malalamiko, maoni na mapendekezo ya wananchi na wadau mbalimbali kwa njia ujumbe mfupi na mitandao ya kijamii (WhatsApp, na barua pepe info@judiciary.go.tz)
Matokeo ya utaratibu huu ni mafanikio makubwa ambayo Gazeti la Mwananchi ingeyatumia pia kwa manufaa ya Wananchi, kwa kutoa ushahidi na taarifa kamilifu.

"
PAMOJA TUNABORESHA HUDUMA"


IMETOLEWA NA:

MTENDAJI MKUU

MAHAKAMA YA TANZANIA

 

Attachments

  • heading.png
    heading.png
    16.4 KB · Views: 3,388
  • 272534081-TAARIFA-KWA-UMMA-JUU-YA-MAKALA-ILIYOTOLEWA-NA-MWANANCHI.pdf
    114.3 KB · Views: 201
Hawa Mahakama na wenzao Polisi lao moja, ukiwaandika madudu yao wanakutembelea eti uthibitishe? Kiboko yao JF WHERE WE DARE TALK OPENLY!
 
Sasa mnatuambia nn na huo ujinga mlo andika?kwani sisi hatuwajui ninyi mahakimu?au hizo taarifa mnawapa wazungu wasio ishi hapa tz?
 
Ingawa mada ni tofauti lakini huwa nashangaa nikienda Mahakama Kuu:

Yaani mnasubiria kuitwa Kwenye Kesi mko kama 100 Halafu wote mmesimama hakuna viti! Yaani hakuna utaratibu ni kelele tupu. Mawakili kelele mtindo mmoja! Yaani hakuna ustaarabu kabisa!

Hivi nyingi Watu wa Mahakama hakuna Akili ya ziada mnayoweza kufanya kuleta ustaarabu?

Ninapoyasikia na kuona ubabaidhaji unaofanywa na Mahakama Za chini nakumbuka ya Mahakama Kuu!
 
Ingawa mada ni tofauti lakini huwa nashangaa nikienda Mahakama Kuu:

Yaani mnasubiria kuitwa Kwenye Kesi mko kama 100 Halafu wote mmesimama hakuna viti! Yaani hakuna utaratibu ni kelele tupu. Mawakili kelele mtindo mmoja! Yaani hakuna ustaarabu kabisa!

Hivi nyingi Watu wa Mahakama hakuna Akili ya ziada mnayoweza kufanya kuleta ustaarabu?

Ninapoyasikia na kuona ubabaidhaji unaofanywa na Mahakama Za chini nakumbuka ya Mahakama Kuu!
Mahakama Kuu na majaji wengi ni vituko vitupu
 
Mwandishi kuandika ndo afwatwe hadi ofisini!!??? Nani nchi hii asojua ukweli.... wala wasisumbuke na waamdishi.... hata hivyo mwisho wa dhuluma umefikia kikomo....octoba mwaka huu..... tutaona ni waandishi ndo wabaya au nani...
 
wala rushwa nyie.imewachoma?
Hii habari ya gazeti la mwananchi ilinifurahisha sana! Haikuficha chochote ila ni ukweli usiopingika! Mfano upo mahakama ya kibaha, hata kesi ya kijinga huwa kiasi cha chini kwao ni 500,000/- yaani yote ni hivyo ila kibaha ni so expensive kwani usipotoa wanakutishia kifungo bila faini
 
Mahakama zetu mhhh. Wacheni majibu ya shortcut. Ni aibu tupu hapa. Watu woote hapa wanakubaliana na gazeti. Lazima ujiulize uliyeandika kutetea mahakama. Tuivunje hii tuanze upya kama Kenya. Mmesahau mawakili na makarani wa mahakama hawa ndio balaa kabisa
 
Hawa Mahakama na wenzao Polisi lao moja, ukiwaandika madudu yao wanakutembelea eti uthibitishe? Kiboko yao JF WHERE WE DARE TALK OPENLY!

DARE TO TALK OPENLY WITHOUT CONCLUSIVE EVIDENCE NI UMBEA TUU.

Haya sasa chukulia mfano wa hilo gazeti mwananchi. Umeshafikisha ujumbe, wahusika wamesikia na wamekuja ili wawasaidie wale waliotoa malalamiko chakushangaza namba za simu hawana, namba za kesi hawana, walalamikaji wanapopatikana haijulikani. Thats means hiyo article japokuwa ina lengo zuri lakini haijasaidia kwa lolote lile.
 
Watoe namb sa simu au kesi zão ili iweje! katika hali ya kukata tamaa wananchi wanapaza sauti São kupigia média il taasisi husika ifanye nazi saké sio mtu mmoja mmoja apeleke ushahidi tendeni haki kwa wananchi mnapotupeleka sipo.
 
Hawasafishiki watu wa mahakama, Kuna rushwa balaa

Nilikuwa na kesi ambayo sikuridhika na hukumu yake, nikaenda Kinondoni kukata rufaa. Kufika tu Mahakamani nikakaribishwa na rundo la makarani akina mama. Nikafikiri ni customer care, kumbe wanashangilia rushwa. Nikaghairi hapo hapo !
 
Dah, hii nchi bado sana. Yaani hadidu za rejea zote ni kumchunguza mwandishi, badala ya kuchunguza kilichoandikwa na huyo mwandishi.

Wanafanya watu hawana akili, kumbe wao ndo hawana akili!
 
Back
Top Bottom