TAARIFA KWA SERIKALI: Bugando HospitaL total tools down kuanzia sasa..

hehehe hehehe kumbe wanaokufa ni wapinzani tu, kwani ukienda hospital ya Private ukionyesha kadi ya CCM unatibiwa bure haha hahah hahah timegundua ndio maana bababa nanihiiii hasemi kitu
 
Nafikiria serekali iakte mirija yote inayoelekea makanisani. Kwani isipofanya hivyo taifa litaangamia. Kama bugando hopsital ya kanisa inagoma kwa kuwa rais aliepo madarakani ni muislam. Nchi imeisha
 
something fishy is going on.someone,somewhere is pulling strings in an effort to bring down the gove
 
tools down maanake wamegoma kuendelea na kazi. Kichwa cha habari "Bugando hospital total tool down kuanzia sasa" ni cha udaku lakini maelezo yanaonyesha bado wako kwenye mkutano na maazimio hayajatoka. badilisha kichwa cha habari ni cha uchochezi.
 
Damn afu nina tumbo la kuhara, hivi Wabunge hawawezi kutibu??
Kama hawawez wabadilishane posho na madokta

Boss madai ya madaktari sio posho tu.
Wanataka huduma za afya ziboreshwe katika vituo vyote vya afya na mahospitali ili kurahisisha kazi yao ya utoaji huduma.
Hili la posho limeshikiwa bango tu ili kuwafinitisha madaktari na wananchi. Wanadhani wakikomalia hili, watashinda kutokana na hasira ya wananchi dhidi ya wabunge. Hii kitu tuitazame kama parcel moja, sio posho tu.
 
Bugando na KCMC ni hospitali za kanisa naomba maelezo wanaingiaje kwenye mgomo huu sambamba na Muhimbili na hospiali zingine za umma? Napata shida kupata tafsiri yake.
 
Kama hujui unachokiandka bora ukae kimya,penda kuandka vitu ambavyo una uhakika navyo.hujui kwamba serikali ina waajiriwa wake hapa?
 
Serikali na bunge kwa maafikiano wamefuta posho za wabunge kwa tangazo la Naibu Spika, Job Ndugai jana, ni budi sasa madaktari nao wakafuta mpango wao wa madai ya nyongeza za posho kama walivyofanya wenzao wabunge na kurudi kazini.
 
Kumekuwa na taarifa za kuwepo kwa kikao cha Madaktari wakazi (Resident) na Interns ambao bado walikuwa wanaona wagonjwa wa dharura sasa wameamua kuacha kila kitu na kuamua kutoa mtangazo.

Kkatika mbao za matangazo kuwa leo hakuna kazi huku kukiwapo na taarifa Madaktari bingwa wa hospitali hii wamekuwa wakionekana katika makorido ya hospitali hiyo wakijadili mgomo na kuwepo kwa tetesi kuwa walikuwa na mpango wa kukaa kikao cha kujadili mgomo na kuweka tool down..


NAOMBA KUWASILISHA

sio taarifa bali ni kweli.
 
Inabidi sasa pinda achukue madaktari wengine toka magereza,..
wengine toka FFU,....
wengine toka zimamoto,...
wengine toka mgambo,...
na kwingne alikodai atapata sijui CUBA,.....

Upuuzi kweli kujidai wewe ndio wewe na bila wewe hakuna kinacho wezekana.
Nawapongeza sana madaktari ingawa binafsi ni mhanga wa mgomo wenu lakini
potelea mbali.

Pinda show us what you've got now.
Wataalam wako wa JWTZ na JKT vipi wameweza?

Wamezidiwa,wanajeshi peke yake wont be able to handle load ya wagonjwa..
 
Inabidi sasa pinda achukue madaktari wengine toka magereza,..
wengine toka FFU,....
wengine toka zimamoto,...
wengine toka mgambo,...
na kwingne alikodai atapata sijui CUBA,.....

Upuuzi kweli kujidai wewe ndio wewe na bila wewe hakuna kinacho wezekana.
Nawapongeza sana madaktari ingawa binafsi ni mhanga wa mgomo wenu lakini
potelea mbali.

Pinda show us what you've got now.
Wataalam wako wa JWTZ na JKT vipi wameweza?

wale 15 wa awamu ya kwanza sijui kama wali-prescribe hata parasetamo moja.
 
Bugando iko chini ya kanisa katoliki, sijui kama nao wanagoma ili wapewe posho na serikali.... hata hivyo mwenye taarifa zaidi atujuze!

Hospitali teule na za rufaa ambazo zipo chini ya kanisa zinaendeshwa kwa MOU kati ya kanisa na serikali. Na katika mambo ambayo serikali inawajibika ni pamoja na kupeleka baadhi ya wataalam kwenye hospitali hizo. Katika hospitali hizo kuna waajiriwa wa kanisa na wengi wao ni waajiriwa wa serikali. Kuna baadhi ya manesi, madaktari, madaktari bingwa, clinical officers ambao ni waajiriwa wa moja kwa moja wa serikali. Hawa japo wanafanya kazi kwenye hospitali za kanisa, mwajiri wao ni serikali, na kanisa hutumika kama wakala tu wa kuwalipa kile ambacho serikali inawapa.
 
Kivipi mmiliki ni mwingine na mwajiri mwingine? fafanua. Naomba radhi kama nakukwaza lakini nataka kuelewa tu

Well,...
am never fooled that easily,...
unataka kunileta kwenye hoja za MS za kanisa na MOU.
am not into that.
kama unataka kweli kweli kujua zaidi,uilize serikali.
 
Back
Top Bottom