Swali la mwendokasi: Lowassa akirudi CCM, CHADEMA watatuambia nini na CCM watatuambia nini?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Mar 11, 2015
1,522
2,112
Mtakumbuka kua CHADEMA walipita nchi nzima mchana wa jua linawaka kua Lowasa ni fisadi na endapo wangeingia ikulu angekabiliwa na mashtaka mungu mkubwa Lowasa kaamua kuwafuata huko huko.

Badala ya kumpeleka mahakamani wakaanza kumnadi kuwa anafaa sana kuwa rais. CHADEMA wakiwa wanasema hayo, CCM walitulia kimyaaa kana kwamba hawajui wala hawasikii lolote. tabu ilianza alipotoka kwao mara tukasikia wanamsakama usiku na mchana kuwa ni mwizi na fisadi anastahili kuwa jela.

Je ikitokea lowasa akarudi CCM, CHADEMA watatuambia nini? CCM pia watatuambia nini?
 
Lowasa Baba nyota yako ya kisiasa ni kali sana na tena inang'aa mno ndo maana kila kukicha watu humu JF wanaandika habari zako tu sijui umewanyang'anya mke hawa kwani hawaishiwi vimaneno maneno tena vya kitototo msikie mwingine huyo hapo juu??
 
Swali la nyongeza: watumishi wote wa umma ambao tulikuwa watumishi awamu ya nne (na hapa naongezea na wanasiasa wote wa vyama vyote waliokuw kwenye tasnia ya siasa wakati wa awamu ya nne)...NI NANI HAKUWA FISADI?

Sent from my MediaPad 7 Youth 2 using JamiiForums mobile app
 
mtakumbuka kua chadema walipita nchi nzima mchana wa jua linawaka kua lowasa ni fisadi na endapo wangeingia ikulu angekabiliwa na mashtaka mungu mkubwa lowasa kaamua kuwafuata huko huko. badala ya kumpeleka mahakamani wakaanza kumnadi kua anafaa sana kua rais. cdm wakiwa wanasema hayo ccm walitulia kimyaaa kana kwamba hawajui wala hawasikii lolote. tabu ilianza alipotoka kwao mara tukasikia wanamsakama uck na mchana kua ni mwizi na fisadi anastahili kua jela. JE IKITOKEA LOWASA AKARUDI CCM CHADEMA WATATUAMBIA NINI? CCM PIA WATATUAMBIA NINI?
Kabla hujajibiwa swali lako la mwendo kasi hube tukumbushie, wakati hao CDM wakisema Lowassa ni fisadi je, CCM waliwajibu vipi CDM ......Kisha utuambie je,baada ya Lowassa kuingia Cdm, CCM walikuwa wanamuitaje ............... na CDM walipowauliza mbona alikuwa huko hamkuchukua hatua yoyote ccm wamejibu vipi ............ ukifafanua haya utapata jibu sahihi kwenye swali lako la mwendo kasi.
 
Back
Top Bottom