VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Walisemwa sana. Kwasasa wananchi wananong'ona chinichini kuwahusu. Urafiki na Serikali iliyopo madarakani unaimarika siku hadi siku. Kila mahala wanapokuwepo na kila maneno wanayoyasema, wanaisifu Serikali kadiri ya uwezo wao. Serikali hii ni ile ile iliyoingia ikijipambanua kuwa iko kwenye vita dhidi ya mafisadi. Rais huyu ni yule yule anayeuchukia ufisadi chamani na Serikalini.
Rostam, Lowassa na Chenge wako ndani ya CCM muda huu. Wako ndani ya chama 'kinachochukia' wizi na ufisadi. Wapo ndani ya chama kinachounda Serikali iliyo kwenye vita dhidi ya ufisadi na wizi chamani na Serikalini. Rostam, Lowassa na Chenge walipachikwa jina la 'Mapacha Watatu' chamani wakati ule wa Rafiki yangu Wilson Mukama.
Kutokana na mtiririko na historia yao chamani, Rostam, Lowassa na Chenge ni mafisadi au si mafisadi? Makada wa CCM tunapaswa kulijibu swali hili bila aibu wala woga. Nguvu waliyonayo chamani isifanye tumuache Rais na Mwenyekiti wetu ajongeane na 'mafisadi' hawa!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Sombetini, Arusha)
Rostam, Lowassa na Chenge wako ndani ya CCM muda huu. Wako ndani ya chama 'kinachochukia' wizi na ufisadi. Wapo ndani ya chama kinachounda Serikali iliyo kwenye vita dhidi ya ufisadi na wizi chamani na Serikalini. Rostam, Lowassa na Chenge walipachikwa jina la 'Mapacha Watatu' chamani wakati ule wa Rafiki yangu Wilson Mukama.
Kutokana na mtiririko na historia yao chamani, Rostam, Lowassa na Chenge ni mafisadi au si mafisadi? Makada wa CCM tunapaswa kulijibu swali hili bila aibu wala woga. Nguvu waliyonayo chamani isifanye tumuache Rais na Mwenyekiti wetu ajongeane na 'mafisadi' hawa!
Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Sombetini, Arusha)