Swali kuhusu tabia ya kususa, kugomea au kuzira: Je, si tabia za kike, si utoto?

Binafsi walichokifanya ni sawa kama watalifikisha mwisho wake lakin watakapojirudi wenyewe afu likaisha juu kwa juu hapo ndipo kususa kunakuwa ujinga na utoto,
 
Huwezi kutumia nguvu zako kuingiza timu huku ukijua tayari mshindi ni fulani sio ushindi tu ila ameshinda kwa hila na hizo hila ulizijua kabla ya kuingiza timu uwanjani na huna namna ya kuzizuia hizo hila maana adui yako ndio kila kitu..
Yeye ndio huamua nani waamuzi wa mechi, yeye ndio hulipia mashabiki hela za kiingilio, yeye ndio hulipia gharama za matangazo, yeye ndio huchagua kiwanja, yeye ndio hupanga mpaka aina ya jezi na vifaa vyoote.

Wapinzani mkiendelea kulialia na kucheka cheka hakuna siku mtafanikiwa, Tafuteni njia nyingine ya kupambana na adui..
Ajabu hata mpira wenyewe hugusi yaani we unatakiwa uwepo tu uwanjani basi ukifungwa goli unachukua mpiara unaweka kati wao wanaanzisha wenyewe unafungwa goli lingine unafuata mpira unaweka kati wanaanzisha tena afu bado unaacha shughuli zako unaenda uwanjani ka sio ujinga ni nn
 
we endelea kumnukuu kinana ila lililowazi ni kuwa upinzani utakuwepo bila kujali nani yuko upinzani usijidanganje kwa kuwa hata MUNGU alipata upinzani na wala hakuutokomeza na ndivyo ilitakavyokuwa kwenu ntajitahidi lakini hamtaweza kuzuia UHALISIA WA DUNIA
Hata chadema ikifa au turudi kwenye chama kimoja upinzani utakuwepo tu huo ndo uhalisia
 
Naona mambo ya kususa yanarudi!.
Watu wakisusa, wengine twala!.

Ila uamuzi huu wa Chadema ni wa busara, kwa chaguzi zote za maradio, nashauri sio tuu Chadema wajitoe, bali vyama vyote wajitoe ili CCM ipite bila kupingwa tuokoe muda, fedha, rasilimali za taifa na kitu kikubwa zaidi, tuokoe machozi, jasho na damu zenye roho za Watanzania.

P.
Truth
 
Wanabodi,

Hili mada ya swali kuhusu tabia ya kususa, kisiasa, huu mtindo wa kuzira au kususa susa, kususia kila jambo usilokubaliana nalo, sio tabia za kike hizi?, au sio tabia za kitoto?!. Mtu unasusia jambo fulani la kisiasa, ili upate nini?. Kususia jambo lolote la kisiasa bila kupiga hesabu ya what do you want to achieve na kususa huko, sio political suicide?.

The Motive Behind Kususa.
Jee ni nini the motive behind kususa jambo fulani, una susa ili uachieve nini, na baada ya kususa, jee hao wasusaji huwa wanakipata kile walichokusudia?!. Kususa jambo fulani bila malengo, sio tuu ni utoto, bali ni ujinga, kwa sababu ni sawa na kumsusia ngedere shamba la mahindi!, utayavuna mabua!.


My Take. (Maoni Yangu).
Kususia kushiriki uchaguzi sio suluhisho, huku ni kujiua kabisa kisiasa, dawa ni kujenga hoja madhubuti na kukaa mezani kuzungumza, vingine tuitumie mahakama yetu kuzifumua sheria kandamizi za uchaguzi ili zituletee uchaguzi huru na wa haki.


1. Tume yetu ya Uchaguzi NEC, japo sio inclusive lakini ni Tume Huru, licha ya kuteuliwa na rais ambaye ni Mwenyekiti wa chama kimojawapo, kwa uhuru ule ule wa Mahakama zetu ambazo majaji huteuliwa na rais huyo huyo ambaye pia humteua Mtendaji Mkuu wa Bunge letu. Kama Bunge limeweza kuwa huru kwa mfumo huu, na Mahakama ni huru, hata Tume pia ni huru, ila ionekane kuwa huru, something more needs to be done kwenye Tume Hii.
2. Sheria yetu ya uchaguzi, ina mapungufu makubwa yanayohitaji kufanyiwa marekebisho ili kutoa ushindani wa haki. Tusiilaumu Tume kwa chochote kinachotokea kwa sababu Tume inatekeleza sheria zilizopo, kama ni sheria kandamizi, ni kosa la sheria na aliyezitunga na sio kosa la mtekelezaji.
3. The political game playing field is not level, we need to create a level playing field ili kupata ushindani wa haki. Hili nalo ni tatizo la kikanuni, mfano uchaguzi wa 2020, kuna mgombea mmoja anaingia kwenye kinyanganyiro na vingora, msafara, media, na wasaidizi kibao, huku budget yake is fully footed by state, ashindane na makapuku!, unategemea nini?. Tangu tumeanza uchaguzi wa vyama vingi, kuna chama dola kinashindana na vyama makapuku!.
4. Now it's high time vyama vya siasa, vianze kutake responsibilities kwa matokeo ya utendaji wa vyama vyetu kwenye chaguzi mbalimbali, kwa kukubali kushiriki uchaguzi katika mazingira haya, na tukishindwa kihalali kwenye sanduku la kura, katika uchaguzi huru na wa haki, tukubali matokeo, na sio kutafuta visingizio.
5. Lazima tufike mahali, kwa pale ambapo uchaguzi ulikuwa huru na wa haki licha ya kasoro za hapa na pale, ambazo hazitaathiri, matokeo ya jumla ya uchaguzi huo, tujifunze kukubali matokeo na kushindwa kihalali, asiyekubali kushindwa sio mshindani. Kisha turudi nyuma kujitathmini where did we go wrong. Tulipaswa kufanya nini ili kupata ushindi katika mazingira kama haya.
Conclusion.
The bitter reality kwa wapenda demokrasia wa kweli wa mfumo wa vyama vingi nchini, mimi nikiwemo, tumeshuhudia hali hii ndio uwezo wa ushindani kwa vyama vyetu vya upinzani nchini Tanzania ndio umefikia hapa baada ya miaka 26 ya vyama vingi, naweza kusema kuwa this is the peak ya upinzani Tanzania, upinzani Tanzania, ndio imefika mwisho wake sasa!. Sasa tuanze kujiuliza, jee kama hali ni hii sana, je hali itakuwaje kwa uchaguzi wa 2020?. Kama wapinzani hawatabadili mbinu na strategies, za namna ya kushindana na CCM kwenye ushindani usio sawa kupitia sanduku la kura, then, uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, kuna hatari kubwa kwa CCM, kuyarejesha majimbo yote ya uchaguzi yaliyokuwa yanashikiliwa na upinzani, hivyo kuirudisha Tanzania kuwa ni nchi rasmi ya chama kimoja cha siasa, something which is not healthy at all to true modern democracy!.


Hongereni sana CCM kwa ushindi mtamu.
Poleni sana Chadema/Ukawa kwa kupoteza majimbo, wabunge na madiwani.


Tanzania kama taifa, tujipe pole kwa gharama kubwa za chaguzi hizi, ila tuombe sana Mungu alisaidie taifa letu kama gharama hizi za uchaguzi wa kinachoitwa demokrasia ya uchaguzi huru na wa haki, zinajumuisha, machozi, jasho na damu za Watanzania, kwa kugharimiwa na damu na roho za Watanzania, hakuna namna nyingine yoyote ya fidia kwa damu za watu na roho za watu, zaidi vya karma!'

Nawatakia Furahi Day ya Ijumaa Njema.

Wasalaam.

Paskali

Rejea za kuhusu Kususa.
Baada ya uchaguzi wa 2010, Chadema ilisusia matokeo na kujidai kuwa hawamtambui JK, ila bunge tuu lilipoanza, niliibua mjadala huu
Chadema Yakubali Yaishe! Yamtambua Rais!, Yampongeza Rais!.


Matokeo ya Chadema Kususia Hotuba ya JK na Kuapishwa kwa Pinda

Media Kususia Habari za Fulani: Jee Tanzania Tuna Independent Media Yenye Jeuri Hiyo?.

Uchaguzi wa 2015 Ukawa wakadai Lowassa ndie mshindi, hivyo wakajifanya kususa, na kutomtambua Magufuli, mimi niliwapa ushauri ufuatao
Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali ya Magufuli ni Serikali Haramu. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!.


Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura; Kaa kimya, Mungu ndiye akupiganie!

CUF kushiriki Uchaguzi wa Marudio Zanzibar si hiyari, Ni lazima! Vinginevyo, huo ndio mwisho wake - JamiiForums

Hatimaye CUF 'Wameridhia' Rasmi, Kushiriki Uchaguzi Wa Marudio Zanzibar!. - JamiiForums

Japo umegharimiwa kwa machozi, jasho na damu, ulikuwa huru na wa haki!. Hongera CCM, CHADEMA poleni!. Mungu saidia Tz - JamiiForums

Ujio wa Lowassa CHADEMA: Kuna kundi wamesusa, wanapanga kurejea CCM! - JamiiForums
I personally respect your opinions but sometimes you are completely out of scope!!
Kwa mazingira wanayopitia wapinzani ni magumu mno,kwa maoni yangu,watu wenye weledi wa kufikiri na wenye kuamini kwenye demokrasia na utawala wa sheria wangeungana na upinzani na sio kubez wala kuuliza maswali ya kinafiki(rhetoric questions)
Hakuna aliyesalama na mfumo na wala tusiwachie wapinzani??.Kwa hali ilivyo huhitaji kuhadithiwa shuruba wanazopitia wapinzani.Mimi nawaheshimu sana akina Mbowe pamoja na mapungufu yao as long wote tunamapungufu!!!
Tusibeze tukifikiri sisi hayatuhusu!!!
 
Subiri uchaguzi wa marudio bila ushiriki vyama rasmi vya upinzani kushuhudia utapeli zaidi wa ccm. Kwa akili zake mbovu chama kikongwe kitarubuni vijitu vya hovyo kabisa mitaani na kudai ndio wakilishi wa upinzani ambao wamekaidi agizo la rasmi la upinzani kutoshiriki uchaguzi.Hizo ndizo akili za master strategists wa chama kikongwe.
 
Mkuu The Big Boss, naomba nikuhakikishie katika maisha yangu yote, sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. Paskali, hanunuliki na yeyote kwa lolote kwa sababu hana price tag. Mimi ni priceless, sio CCM wa Chadema, wala Ukawa, wala Lowassa wala Magufuli, ana uwezo wa kuninunua, kwa sababu I'm not for sale, na sina any price tag!.

Naomba uniamini hili ni swali tuu, nimeuliza hawa wanaosusa, wamesusa ili wapate nini?!.

Ni swali tuu.

Paskali
Kununuliwa siyo lazima uwe mwanachama wa chama cha siasa.Kwanza hiyo ni siri kati ya mnunuzi na mnunuliwa so usingeweza kuja hapa kukiri kununuliwa.
Pili, tume huru ni tume ya aina gani? Utakuwa kichaa kusema iliyopo Tz ni tume huru. Pascal anajitoa fahamu makusudi sijui labda anamfurahisha bwana wake. Viongozi wa Tume wameteuliwa na Raisi ambaye ni Mkiti wa Ccm wataachaje hawa kutekeleza matakwa ya aliyewateuwa. YAANI MECHI YA SIMBA NA YANGA REFA NI HAJI MANARA kisa tu eti kuna sheria 17 za soka basi Manara hawez kuwabeba simba. Ukichaa.
 
I personally respect your opinions but sometimes you are completely out of scope!!
Kwa mazingira wanayopitia wapinzani ni magumu mno,kwa maoni yangu,watu wenye weledi wa kufikiri na wenye kuamini kwenye demokrasia na utawala wa sheria wangeungana na upinzani na sio kubez wala kuuliza maswali ya kinafiki(rhetoric questions)
Hakuna aliyesalama na mfumo na wala tusiwachie wapinzani??.Kwa hali ilivyo huhitaji kuhadithiwa shuruba wanazopitia wapinzani.Mimi nawaheshimu sana akina Mbowe pamoja na mapungufu yao as long wote tunamapungufu!!!
Tusibeze tukifikiri sisi hayatuhusu!!!
Huyu Mayalla amini usiamini kwa sasa ubongo wake uko controlled pale Lumumba. Yuko ktk mradi maalumu, kwa sasa yeye si mtanzania ni mgeni wa kinachoendelea nchini.
 
Kununuliwa siyo lazima uwe mwanachama wa chama cha siasa.Kwanza hiyo ni siri kati ya mnunuzi na mnunuliwa so usingeweza kuja hapa kukiri kununuliwa.
Pili, tume huru ni tume ya aina gani? Utakuwa kichaa kusema iliyopo Tz ni tume huru. Pascal anajitoa fahamu makusudi sijui labda anamfurahisha bwana wake. Viongozi wa Tume wameteuliwa na Raisi ambaye ni Mkiti wa Ccm wataachaje hawa kutekeleza matakwa ya aliyewateuwa. YAANI MECHI YA SIMBA NA YANGA REFA NI HAJI MANARA kisa tu eti kuna sheria 17 za soka basi Manara hawez kuwabeba simba. Ukichaa.
Kama kuanzia Jaji Mkuu na majaji wote wanateuliwa na rais, na bado Chadema inapata haki mahakamani, why not Tume?!. Bungeni ndani ya bunge hili kuna wabunge zaidi ya 100 wa upinzani, lakini kwenye bunge la 2020, akifanikiwa kuingia mbunge, then ni mmoja tuu Zitto!, na hii sio issue ya NEC bali Magufuli ni game changer, someni hizi nyuzi hapa chini, kitu muhimu muangalie ziliandikwa lini
Je, Kasi ya Magufuli itaua Upinzani Uchwara na Kuimarisha Upinzani Makini? - Prof. Kitila Mkumbo - JamiiForums

Trend Reading: Wanaohamia CCM wasibezwe! Wanaona mbali, 2020 Majimbo yote kurejeshwa. Je tunarejea nchi ya Chama kimoja? - JamiiForums

Swali la Ukweli Mchungu: Je, 2020 Magufuli ana mpinzani au mshindani, au Ni Magufuli tu?!. - JamiiForums

Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020? - JamiiForums

Je, CHADEMA inaweza kushinda 2020? Is it serious, credible & mature enough opposition?!. - JamiiForums

In 2015 Election, Tanzania had A Choice To Choose From. Jee Kwa 2020, Do We Still Have A Choice?. - JamiiForums

CHADEMA Chama cha Ajabu Sana!.Kwenda Mahakamani Kwa Non Issue, Serious Issue ya Katiba ni UKUTA!. - JamiiForums

Sheria ya Uchaguzi Ni Bad Law!, Kuendelea Kuitumia ni Ujinga?, Kuwabebesha Masikini Gharama za Uchaguzi ni Dhambi!. - JamiiForums

P.
 
Mkuu The Big Boss, naomba nikuhakikishie katika maisha yangu yote, sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. Paskali, hanunuliki na yeyote kwa lolote kwa sababu hana price tag. Mimi ni priceless, sio CCM wa Chadema, wala Ukawa, wala Lowassa wala Magufuli, ana uwezo wa kuninunua, kwa sababu I'm not for sale, na sina any price tag!.

Naomba uniamini hili ni swali tuu, nimeuliza hawa wanaosusa, wamesusa ili wapate nini?!.

Ni swali tuu.

Paskali
Tunawatambua watu kwa matendo yao.kwahiyo huna haja ya kujieleza sana kwa sisi watu tuliosomea sayansi ya akili.Hayo maelezo yako yafaa uwaeleze watoto wa chekechea au vichaa.
 
Wanabodi,

Hili mada ya swali kuhusu tabia ya kususa, kisiasa, huu mtindo wa kuzira au kususa susa, kususia kila jambo usilokubaliana nalo, sio tabia za kike hizi?, au sio tabia za kitoto?!. Mtu unasusia jambo fulani la kisiasa, ili upate nini?. Kususia jambo lolote la kisiasa bila kupiga hesabu ya what do you want to achieve na kususa huko, sio political suicide?.

The Motive Behind Kususa.
Jee ni nini the motive behind kususa jambo fulani, una susa ili uachieve nini, na baada ya kususa, jee hao wasusaji huwa wanakipata kile walichokusudia?!. Kususa jambo fulani bila malengo, sio tuu ni utoto, bali ni ujinga, kwa sababu ni sawa na kumsusia ngedere shamba la mahindi!, utayavuna mabua!.


My Take. (Maoni Yangu).
Kususia kushiriki uchaguzi sio suluhisho, huku ni kujiua kabisa kisiasa, dawa ni kujenga hoja madhubuti na kukaa mezani kuzungumza, vingine tuitumie mahakama yetu kuzifumua sheria kandamizi za uchaguzi ili zituletee uchaguzi huru na wa haki.


1. Tume yetu ya Uchaguzi NEC, japo sio inclusive lakini ni Tume Huru, licha ya kuteuliwa na rais ambaye ni Mwenyekiti wa chama kimojawapo, kwa uhuru ule ule wa Mahakama zetu ambazo majaji huteuliwa na rais huyo huyo ambaye pia humteua Mtendaji Mkuu wa Bunge letu. Kama Bunge limeweza kuwa huru kwa mfumo huu, na Mahakama ni huru, hata Tume pia ni huru, ila ionekane kuwa huru, something more needs to be done kwenye Tume Hii.
2. Sheria yetu ya uchaguzi, ina mapungufu makubwa yanayohitaji kufanyiwa marekebisho ili kutoa ushindani wa haki. Tusiilaumu Tume kwa chochote kinachotokea kwa sababu Tume inatekeleza sheria zilizopo, kama ni sheria kandamizi, ni kosa la sheria na aliyezitunga na sio kosa la mtekelezaji.
3. The political game playing field is not level, we need to create a level playing field ili kupata ushindani wa haki. Hili nalo ni tatizo la kikanuni, mfano uchaguzi wa 2020, kuna mgombea mmoja anaingia kwenye kinyanganyiro na vingora, msafara, media, na wasaidizi kibao, huku budget yake is fully footed by state, ashindane na makapuku!, unategemea nini?. Tangu tumeanza uchaguzi wa vyama vingi, kuna chama dola kinashindana na vyama makapuku!.
4. Now it's high time vyama vya siasa, vianze kutake responsibilities kwa matokeo ya utendaji wa vyama vyetu kwenye chaguzi mbalimbali, kwa kukubali kushiriki uchaguzi katika mazingira haya, na tukishindwa kihalali kwenye sanduku la kura, katika uchaguzi huru na wa haki, tukubali matokeo, na sio kutafuta visingizio.
5. Lazima tufike mahali, kwa pale ambapo uchaguzi ulikuwa huru na wa haki licha ya kasoro za hapa na pale, ambazo hazitaathiri, matokeo ya jumla ya uchaguzi huo, tujifunze kukubali matokeo na kushindwa kihalali, asiyekubali kushindwa sio mshindani. Kisha turudi nyuma kujitathmini where did we go wrong. Tulipaswa kufanya nini ili kupata ushindi katika mazingira kama haya.
Conclusion.
The bitter reality kwa wapenda demokrasia wa kweli wa mfumo wa vyama vingi nchini, mimi nikiwemo, tumeshuhudia hali hii ndio uwezo wa ushindani kwa vyama vyetu vya upinzani nchini Tanzania ndio umefikia hapa baada ya miaka 26 ya vyama vingi, naweza kusema kuwa this is the peak ya upinzani Tanzania, upinzani Tanzania, ndio imefika mwisho wake sasa!. Sasa tuanze kujiuliza, jee kama hali ni hii sana, je hali itakuwaje kwa uchaguzi wa 2020?. Kama wapinzani hawatabadili mbinu na strategies, za namna ya kushindana na CCM kwenye ushindani usio sawa kupitia sanduku la kura, then, uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, kuna hatari kubwa kwa CCM, kuyarejesha majimbo yote ya uchaguzi yaliyokuwa yanashikiliwa na upinzani, hivyo kuirudisha Tanzania kuwa ni nchi rasmi ya chama kimoja cha siasa, something which is not healthy at all to true modern democracy!.


Hongereni sana CCM kwa ushindi mtamu.
Poleni sana Chadema/Ukawa kwa kupoteza majimbo, wabunge na madiwani.


Tanzania kama taifa, tujipe pole kwa gharama kubwa za chaguzi hizi, ila tuombe sana Mungu alisaidie taifa letu kama gharama hizi za uchaguzi wa kinachoitwa demokrasia ya uchaguzi huru na wa haki, zinajumuisha, machozi, jasho na damu za Watanzania, kwa kugharimiwa na damu na roho za Watanzania, hakuna namna nyingine yoyote ya fidia kwa damu za watu na roho za watu, zaidi vya karma!'

Nawatakia Furahi Day ya Ijumaa Njema.

Wasalaam.

Paskali

Rejea za kuhusu Kususa.
Baada ya uchaguzi wa 2010, Chadema ilisusia matokeo na kujidai kuwa hawamtambui JK, ila bunge tuu lilipoanza, niliibua mjadala huu
Chadema Yakubali Yaishe! Yamtambua Rais!, Yampongeza Rais!.


Matokeo ya Chadema Kususia Hotuba ya JK na Kuapishwa kwa Pinda

Media Kususia Habari za Fulani: Jee Tanzania Tuna Independent Media Yenye Jeuri Hiyo?.

Uchaguzi wa 2015 Ukawa wakadai Lowassa ndie mshindi, hivyo wakajifanya kususa, na kutomtambua Magufuli, mimi niliwapa ushauri ufuatao
Kama Hii ni Kweli, Then, Serikali ya Magufuli ni Serikali Haramu. Hukumu ya Karma ii Juu Yake!.


Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura; Kaa kimya, Mungu ndiye akupiganie!

CUF kushiriki Uchaguzi wa Marudio Zanzibar si hiyari, Ni lazima! Vinginevyo, huo ndio mwisho wake - JamiiForums

Hatimaye CUF 'Wameridhia' Rasmi, Kushiriki Uchaguzi Wa Marudio Zanzibar!. - JamiiForums

Japo umegharimiwa kwa machozi, jasho na damu, ulikuwa huru na wa haki!. Hongera CCM, CHADEMA poleni!. Mungu saidia Tz - JamiiForums

Ujio wa Lowassa CHADEMA: Kuna kundi wamesusa, wanapanga kurejea CCM! - JamiiForums
U DC unanukia
 
Paschal sio hajui sababu ya cdm kugomea uchaguzi hila anachofanya ni dhihaka tu.Nashangaa hata kwanini tunacomment ujinga wake.alipaswa alete hoja ya sababu za cdm kugomea mfano Mawakala wa cdm kutolewa vituoni,kuna kituo kina voters 303 CCM wapepata 277etc but not that sarcasm.Heshima yake Paschal inashuka.
 
Kaka Pascal naelewa sana unachosema. Mbali na lugha ya udhalilishaji uliyotumia, nimeelewa hoja yako. Kinachoendelea kinaonesha wazi kuwa CDM wamekosa mbinu mbadala. Kususa au kugoma siyo suluhisho hasa kwa Viongozi wasioelewa hata maana ya demokrasia. Siasa za nchi zilizoendelea ni tofauti kabisa na za nchi zetu hizi zisizoendelea. Kuzira au kususa kisiasa havioneshi kuitishia serikali. Ni muda wa upinzani kutumia njia nyingine zinazoweza kuwapa haki zao za msingi. Hapa ndo tujadiliane njia mbadala tofauti na njia hizi zinazotumika sasa zisizo na matunda kwa wapinzani.
 
Hivi ukishaona askari ndo wanashangilia ushindi wa ccm badala ya wananchi wenyewe wapiga kura, kweli bado utaendelea kushiriki kwenye chaguzi hizo!!! Utakuwa mwehu kabisa.
 
Back
Top Bottom