Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
SUMAYE AONYA NCHI INAELEKEA KUBAYA
WAZIRI Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, ameonya kwamba nchi inaelekea kubaya kwa kuwa watu wanatumia fedha nyingi kwa kasi kuusaka uongozi na baadaye kuishia kuwanyanyasa
.. Pia amewaasa wanasiasa kuacha kuwatumia wanafunzi wa vyuo vikuu kuusaka uongozi kwa maslahi yao binafsi kwa kuwa njia hiyo ni hatari kwa mustakabali wa taifa.
Akizungumza katika mkutano wa viongozi wa Shirikisho la Wanafunzi wa Elimu ya Juu (Tahliso), Sumaye alisema nchi inaelekea kubaya kwa kuwa watu wanatumia fedha nyingi kupata uongozi na kwamba wakiingia madarakani wanakuwa wababe kwa wananchi waliomchagua.
Hivi sasa kuna kila dalili, ukitaka uongozi katika nafasi yoyote mpaka za chini, lazima utumie fedha sana, wapiga kura wananunuliwa na mwisho wa yote, wananchi wanaongozwa na kiongozi mbabe na asiyetaka kushauriwa na watu, alisema Sumaye.
Alisema utaratibu wa kununua uongozi ni hatari kwa sababu nchi inaweza kuingia kwenye matatizo makubwa kuwa kuwa kiongozi huyo anakuwa amepata madaraka kwa njia ya mkato, vijana wanapaswa kulisaidia taifa kwa kutokubali kutumika kuwaingia baadhi ya viongozi madarakani.Aliwataka vijana kuwa makini kwa kuwa wamekuwa wakitumiwa na viongozi wa vyama vya siasa kupata madaraka kwa ahadi kwamba vijana hao watapewa fedha au cheo baada ya kumaliza chuo.
Alisema wanasiasa wanakuwa wastarabu na kuonyesha upole wakati wa kuomba kura, lakini wakipata madaraka wanakuwa wakali na kutumia ubabe katika kufanya uamuzi wa kitaifa. Watu wakitaka uongozi wanakuwa wa pole sana katika kipindi cha kuomba kura, lakini wakipata madaraka wanakuwa wakali kama simba, hawataki kushauriwa na matokeo yake wanafanya maamuzi ya kibabe ambayo yanasababisha madhara makubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla,alisema Sumaye.
Alisema hivi sasa viongozi wamekuwa katika mijadala mingi kuhusu tatizo la ajira bila kutoa ufumbuzi wa tatizo hilo.Jambo hili limekuwa likizungumziwa kwa urahisi sana, kuzungumzia ajira bila kuzungumzia kiwanda ni sawa na kuhangaika na joto la mgonjwa badala ya kushughulikia ugonjwa unaosababisha joto hilo kupanda,alisema Sumaye. Alisema tatizo la ajira linatatuliwa na kiwanda cha kuzalisha ajira ambacho ni uchumi utakaosambaa na kunufaisha watu wote na siyo kuwanufaisha watu wachache.
Sumaye aliwataka wanavyuo na wasomi wa masuala ya uchumi kujadili tatizo la ajira kwa kuitisha makongamano ili kuwarekebisha wataalamu na wachambuzi wa mambo kwa lengo la kulisaidia taifa.Alisema endapo vijana watatumika vizuri na nchi kuongozwa na viongozi wenye uwezo kutakuwa na maendeleo makubwa na kuondoa tatizo linaloinyemelea taifa la kununua uongozi.
Naye Mwenyekiti wa Tahliso, Paul Mkonda alisema hivi sasa kumekuwa na muamko mkubwa wa kisiasa baada ya nchi za Kaskazini mwa Afrika na kuleta hamasa kubwa katika vyuo vikuu nchini.
Wanasiasa wanawafanya wanafunzi kuweka mkazo zaidi katika siasa kwa maslahi yao binafsi, na kusababisha wanafunzi wengi kuaathirika kimasomo. Sisi tunaomba wanasiasa wawaache wanavyuo kwa kuwa siasa za chuo na za wanasiasa ni tofauti sana, alisema Mkonda. Alisema suala la wanafunzi kushiriki katika siasa, inatishia ubora wa elimu katika vyuo vikuu na utulivu.
Alisema wanapaswa kuweka mikakati thabiti kwa vyama vyote vya siasa ili kuhakikisha waanadhibiti na kukemea wanasiasa ambao wanawashirikisha wanafunzi katika siasa malengo yao. Tahliso inaandaa mikakati ya kuwa na programu ya kuandaa viongozi wa nchi kwa kutoa mafunzo mbalimbali ya uongozi.
Akizungumza katika mkutano wa viongozi wa Shirikisho la Wanafunzi wa Elimu ya Juu (Tahliso), Sumaye alisema nchi inaelekea kubaya kwa kuwa watu wanatumia fedha nyingi kupata uongozi na kwamba wakiingia madarakani wanakuwa wababe kwa wananchi waliomchagua.
Hivi sasa kuna kila dalili, ukitaka uongozi katika nafasi yoyote mpaka za chini, lazima utumie fedha sana, wapiga kura wananunuliwa na mwisho wa yote, wananchi wanaongozwa na kiongozi mbabe na asiyetaka kushauriwa na watu, alisema Sumaye.
Alisema utaratibu wa kununua uongozi ni hatari kwa sababu nchi inaweza kuingia kwenye matatizo makubwa kuwa kuwa kiongozi huyo anakuwa amepata madaraka kwa njia ya mkato, vijana wanapaswa kulisaidia taifa kwa kutokubali kutumika kuwaingia baadhi ya viongozi madarakani.Aliwataka vijana kuwa makini kwa kuwa wamekuwa wakitumiwa na viongozi wa vyama vya siasa kupata madaraka kwa ahadi kwamba vijana hao watapewa fedha au cheo baada ya kumaliza chuo.
Alisema wanasiasa wanakuwa wastarabu na kuonyesha upole wakati wa kuomba kura, lakini wakipata madaraka wanakuwa wakali na kutumia ubabe katika kufanya uamuzi wa kitaifa. Watu wakitaka uongozi wanakuwa wa pole sana katika kipindi cha kuomba kura, lakini wakipata madaraka wanakuwa wakali kama simba, hawataki kushauriwa na matokeo yake wanafanya maamuzi ya kibabe ambayo yanasababisha madhara makubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla,alisema Sumaye.
Alisema hivi sasa viongozi wamekuwa katika mijadala mingi kuhusu tatizo la ajira bila kutoa ufumbuzi wa tatizo hilo.Jambo hili limekuwa likizungumziwa kwa urahisi sana, kuzungumzia ajira bila kuzungumzia kiwanda ni sawa na kuhangaika na joto la mgonjwa badala ya kushughulikia ugonjwa unaosababisha joto hilo kupanda,alisema Sumaye. Alisema tatizo la ajira linatatuliwa na kiwanda cha kuzalisha ajira ambacho ni uchumi utakaosambaa na kunufaisha watu wote na siyo kuwanufaisha watu wachache.
Sumaye aliwataka wanavyuo na wasomi wa masuala ya uchumi kujadili tatizo la ajira kwa kuitisha makongamano ili kuwarekebisha wataalamu na wachambuzi wa mambo kwa lengo la kulisaidia taifa.Alisema endapo vijana watatumika vizuri na nchi kuongozwa na viongozi wenye uwezo kutakuwa na maendeleo makubwa na kuondoa tatizo linaloinyemelea taifa la kununua uongozi.
Naye Mwenyekiti wa Tahliso, Paul Mkonda alisema hivi sasa kumekuwa na muamko mkubwa wa kisiasa baada ya nchi za Kaskazini mwa Afrika na kuleta hamasa kubwa katika vyuo vikuu nchini.
Wanasiasa wanawafanya wanafunzi kuweka mkazo zaidi katika siasa kwa maslahi yao binafsi, na kusababisha wanafunzi wengi kuaathirika kimasomo. Sisi tunaomba wanasiasa wawaache wanavyuo kwa kuwa siasa za chuo na za wanasiasa ni tofauti sana, alisema Mkonda. Alisema suala la wanafunzi kushiriki katika siasa, inatishia ubora wa elimu katika vyuo vikuu na utulivu.
Alisema wanapaswa kuweka mikakati thabiti kwa vyama vyote vya siasa ili kuhakikisha waanadhibiti na kukemea wanasiasa ambao wanawashirikisha wanafunzi katika siasa malengo yao. Tahliso inaandaa mikakati ya kuwa na programu ya kuandaa viongozi wa nchi kwa kutoa mafunzo mbalimbali ya uongozi.