Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,017
- 144,373
Nilpomuona IGP anakemea makamanda wa Polisi wa Mikoa,sikutaka kuamini kama kweli aliongea vile bila kuwa na jambo nyuma yake na kwamba alikuwa anamanisha anachokisema.
Sasa wale mlimuamini na kumpongeza,mpimeni kwa hatua atazochukua kwa Polisi waliovamia mkutano wa ndani wa CHADEMA huko hai.
Subirini muone kama atakemea waliogiza Polisi kuvamia huo mkutano au atamkemea Afisa wa Polisi alieagiza Polisi wavamie huo mkutano.
Kama hii miaka minne haitoshi watu kujifunza,basi inapaswa tujiulize sisi ni binadamu wa aina gani.
Naomba niishie hapa.
Sasa wale mlimuamini na kumpongeza,mpimeni kwa hatua atazochukua kwa Polisi waliovamia mkutano wa ndani wa CHADEMA huko hai.
Subirini muone kama atakemea waliogiza Polisi kuvamia huo mkutano au atamkemea Afisa wa Polisi alieagiza Polisi wavamie huo mkutano.
Kama hii miaka minne haitoshi watu kujifunza,basi inapaswa tujiulize sisi ni binadamu wa aina gani.
Naomba niishie hapa.
Hai: Polisi wazingira Ofisi za CHADEMA unapofanyika Mkutano wa ndani wa chama unaoongozwa na Mbowe
Polisi wilaya ya Hai mkoa Kilimanjaro wakiongozwa na OCD wa wilaya hiyo, Lwelwe Mpina wamezunguka ofisi ya CHADEMA wilaya ya Hai ambako mkutano wa ndani wa CHADEMA wilaya hiyo unaoongozwa na mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe unaendelea. Wengine waliomo ndani ya mkutano huo ni mwenyekiti...
www.jamiiforums.com