Azimio Jipya
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 3,362
- 1,131
Koba na Bin Maryam,
Tuwe wakweli mkuu wangu let's face the truth na sio kusingizia Azimio la Arusha kwa kigezo cha mbinu alizotumia Mwalimu, bado tunao ng'ombe wetu wawili kinachotakiwa ni kuweka Azimio litakalo hakikisha ng'ombe hao wapo kwa faida ya wananachi wote na sio fungu la watu wachache.
Mkuu wangu give me a break, Mkapa kuwa kiongozi wa kusifiwa kweli?...
Mkanadara:
Mpaka hapa sina amabacho nigeongezea kwenye maelezo uliyotoa kwa hoja inayoedelea. Nimekuna kichwa nikajiuliza ni mimi sijui maana ya hili azimio la arusha au tunapishana wapi na wengine.
Nimemuelewa Mtanzania, nikisoma post za Kichuguu nazielewa... Zinanipa moyo kuwa kama kimsingi hawa wanaona kama ninavyona may be bado ninalijua Azimio la Arusha ni nini!
Uzuri wa JF tofauti na hizi yingine nilizozipitia kwa kipindihiki cha "mahangaiko ya Mapolisi" ni kuwa michango ni mingi na wakati mwingine ina vina kwelikweli. Ninafurahia JF kwa hilo.
Nafikiri nijipe muda kuangalia na kujifunza kwa undani wachangiaji wengine, nione mitizamo yao, niangalie kwa makini kabisa wanafikiri Azimio la Arusha ni nini. Bahati mbaya kabisa mimi sio mwansiasa kabisa. Na sikumbuki kufindishwa maana ya Azimio la Arusha mahali popote shuleni. Kama walifundisha basi sikuwa msikivu. Labda niliona ni kitu kisichonihusu..na kukiondolea mbali!!
Lakini hivi karibuni imebidi na imetokea nikaamua kufuatia kwa kina na mapana. Nikafikiri nimelielewa. ndio maana nikaona mtizamo inayofanana na ya baadhi ya post hapa, Nikaiona ni ok, Nikajisemea, kama ninawaelewa maoni ya badhi ya wenzangu ..nafikiri niko njiani..lakini nikaona pia kuwa kwa kutoelewa maoni mengine...nijibidiishe kujifunza Azimio la Arusha. Najipa muda!!!
Moyoni ninajua kabisa Kuna jambo ndani ya hili Azimio la Arusha. Na ninafikiri litaibuka wazi hadharani!!!
Sitegemei liwe photocopy ya lile cha 1967.... lakini kwa kuwa huu ni mfumo wa maisha ulio na structure, value na character it can come in any shape and form kutoa majibu muhimu ya ustawi wa maisha.
Na inawezekana maneno haya Azimio la Arusha yanapotosha ..kwani the tool and its system inaweza kuweko kwa ubatizo tofauti tu!! Lakini ikihudumia jamii kwa ufanisi mkubwa. Ni kama neno UMEME lisivyo husiana na KITU CHENYEWE. Na kulibadili neno umeme kwa maneno mengi kwenye nyakati tofauti na hali tofauti isivyo adhiri KITU CHENYEWE! Tutafute kitu chenyewe!