JuaKali
JF-Expert Member
- Nov 14, 2007
- 776
- 118
Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, jana ililipa kisasi baada ya kuifunga Msumbiji `The Mambas` kwa bao 1-0 katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliofanyika kwenye uwanja mkuu wa taifa jijini Dar es Salaam.
Stars ilipokea kipigo kama hicho kutoka kwa Msumbiji wakati timu hizo zilipokutana Septemba 8 mwaka jana kwenye uwanja huohuo mkuu wa taifa.
Baada ya kukukuruka kwa dakika 78 ikitafuta bao katika mchezo huo wa jana, Stars hatimaye ilifanikiwa kuona mwezi katika dakika ya 79 baada ya Kigi Makassi kufunga akipokea pasi kutoka kwa Mrisho Ngasa aliyeuwahi mpira uliopigwa na Abdi Kassim.
Dakika 22 Msumbiji ilikosa bao kupitia kwa Alimiro Lobo baada ya krosi safi iliyopigwa na mchezaji mmoja wa timu hiyo na kuokolewa na Godfrey Bonny wa Stars na kumkuta Lobo aliyeshindwa kufunga licha ya kuwa katika nafasi nzuri.
Jerry Tegete dakika sita baadae naye alishindwa kufunga akiwa ndani ya mita 18 baada ya beki wa Msumbiji Antonio Gravata kuuwahi mpira na kuokoa hatari katika lango la Msumbiji.
Idd Moshi Boban nusura aipatie Stars bao katika dakika ya 35 lakini alishindwa kumalizia kazi nzuri iliyofanywa na Juma Jabu baada ya kupiga shuti dhaifu na kuokolewa na beki wa Msumbiji Guilherme Manhique.
Msumbiji ilifanya shambulio jingine la nguvu katika dakika ya 44 lakini Antonio Gravata alishindwa kuifungia bao baada ya kupaisha mpira juu ya goli akiunganisha vibaya krosi ya Ticotico.
Stars kupitia kwa beki wake Shadrack Nsajigwa nusura ifunge baada ya mchezaji huyo kupanda na kupiga shuti kali lakini kipa wa Msumbuji Marcelino Cumbane alifanya kazi nzuri kuokoa mpira huo kabla haujatinga wavuni.
Kocha wa Stars, Marcio Maximo alisema baada ya mchezo huo, kuwa mchezo ulikuwa mgumu kama alivyotarajia na Msumbiji walicheza vizuri licha ya kufungwa kwani walipata nafasi nyingi lakini walishindwa kuzitumia.
Alisema kuwa ushndi huo utawaongezea ari wachezaji wake kwa ajili ya pambano lijalo dhidi ya Sudan litakalofanyika Novemba 29 jijini Dar es Salaam kusaka kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka katika ligi za nyumbani tu.
Naye kocha wa Msumbiji, Mooij Martinus alisema kuwa ushindi huo ni zawadi tosha ya Krismas kwa Stars pia aliweapongeza wapinzani wao kwa ushindi huo, ambapo alisisitiza kuwa kwa sasa timu yake inajifua kwa ajili ya hatua ya pili ya kufuzu kwa mashindano ya Mataifa ya Afrika na Kombe la Dunia.
Timu zilikuwa; Taifa Stars: Shabaan Dihile, Shadrack Nsajigwa, Juma Jabu, Nadir Haroub `Cannavaro`, Salum Sued, Godfrey Bonny, Mrisho Ngassa/Mussa Hassan Mgosi (dk.89), Henry Joseph/Nurdin Bakari (dk.74), Jerry Tegete/Nizar Khalfan (dk. 59), Haruna Moshi `Boban`/Abdi Kassim (dk.71) na Athumani Iddi `Chuji\'/Kigi Makassi (dk.63).
Msumbiji: Marcelino Cumbane, Antonio Gravata, Gonclaves Fumo/Momed Hagi (dk. 59), Elias Pelembe, Manuel Bucuane, Dario Monteiro/Lus Muchue (dk.55), Guilherme Manhique/Nasser Carimo (dk.77), Carlos Parruque/Carlos Chimomole (dk.89), Francisco Massinga, Alimiro Lobo na Fanuel Massingue
Stars ilipokea kipigo kama hicho kutoka kwa Msumbiji wakati timu hizo zilipokutana Septemba 8 mwaka jana kwenye uwanja huohuo mkuu wa taifa.
Baada ya kukukuruka kwa dakika 78 ikitafuta bao katika mchezo huo wa jana, Stars hatimaye ilifanikiwa kuona mwezi katika dakika ya 79 baada ya Kigi Makassi kufunga akipokea pasi kutoka kwa Mrisho Ngasa aliyeuwahi mpira uliopigwa na Abdi Kassim.
Dakika 22 Msumbiji ilikosa bao kupitia kwa Alimiro Lobo baada ya krosi safi iliyopigwa na mchezaji mmoja wa timu hiyo na kuokolewa na Godfrey Bonny wa Stars na kumkuta Lobo aliyeshindwa kufunga licha ya kuwa katika nafasi nzuri.
Jerry Tegete dakika sita baadae naye alishindwa kufunga akiwa ndani ya mita 18 baada ya beki wa Msumbiji Antonio Gravata kuuwahi mpira na kuokoa hatari katika lango la Msumbiji.
Idd Moshi Boban nusura aipatie Stars bao katika dakika ya 35 lakini alishindwa kumalizia kazi nzuri iliyofanywa na Juma Jabu baada ya kupiga shuti dhaifu na kuokolewa na beki wa Msumbiji Guilherme Manhique.
Msumbiji ilifanya shambulio jingine la nguvu katika dakika ya 44 lakini Antonio Gravata alishindwa kuifungia bao baada ya kupaisha mpira juu ya goli akiunganisha vibaya krosi ya Ticotico.
Stars kupitia kwa beki wake Shadrack Nsajigwa nusura ifunge baada ya mchezaji huyo kupanda na kupiga shuti kali lakini kipa wa Msumbuji Marcelino Cumbane alifanya kazi nzuri kuokoa mpira huo kabla haujatinga wavuni.
Kocha wa Stars, Marcio Maximo alisema baada ya mchezo huo, kuwa mchezo ulikuwa mgumu kama alivyotarajia na Msumbiji walicheza vizuri licha ya kufungwa kwani walipata nafasi nyingi lakini walishindwa kuzitumia.
Alisema kuwa ushndi huo utawaongezea ari wachezaji wake kwa ajili ya pambano lijalo dhidi ya Sudan litakalofanyika Novemba 29 jijini Dar es Salaam kusaka kufuzu kwa fainali za Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza soka katika ligi za nyumbani tu.
Naye kocha wa Msumbiji, Mooij Martinus alisema kuwa ushindi huo ni zawadi tosha ya Krismas kwa Stars pia aliweapongeza wapinzani wao kwa ushindi huo, ambapo alisisitiza kuwa kwa sasa timu yake inajifua kwa ajili ya hatua ya pili ya kufuzu kwa mashindano ya Mataifa ya Afrika na Kombe la Dunia.
Timu zilikuwa; Taifa Stars: Shabaan Dihile, Shadrack Nsajigwa, Juma Jabu, Nadir Haroub `Cannavaro`, Salum Sued, Godfrey Bonny, Mrisho Ngassa/Mussa Hassan Mgosi (dk.89), Henry Joseph/Nurdin Bakari (dk.74), Jerry Tegete/Nizar Khalfan (dk. 59), Haruna Moshi `Boban`/Abdi Kassim (dk.71) na Athumani Iddi `Chuji\'/Kigi Makassi (dk.63).
Msumbiji: Marcelino Cumbane, Antonio Gravata, Gonclaves Fumo/Momed Hagi (dk. 59), Elias Pelembe, Manuel Bucuane, Dario Monteiro/Lus Muchue (dk.55), Guilherme Manhique/Nasser Carimo (dk.77), Carlos Parruque/Carlos Chimomole (dk.89), Francisco Massinga, Alimiro Lobo na Fanuel Massingue