Somalia kumekucha: Rais mteule anusurika kuuawa

Bishop Hiluka

JF-Expert Member
Aug 12, 2011
7,140
14,678
Rais mpya wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamud, amenusurika jaribio la kumuua mjini Mogadishu.
Milipuko miwili imetokea nje la lango la makao ya rais huyo katika hoteli ya Al-Jazeera wakati rais
huyo alipokuwa anajiandaa kufanya mkutano na waandishi wa habari.

Taarifa zinasema kuwa waziri wa mambo ya nje wa Kenya Sam Ongeri pia alikuwa katika hoteli hiyo
wakati wa shambulizi. Hata hivyo wawili hao wamenusurika. Ingawa inaarifiwa kuwa mtu mmoja ameuawa.

Source: BBC
 
Ooooh! Hawa al-shabab si ndio tulisikia kuwa wanasaidiwa na wakubwa wa magharibi? vipi wakubwa wa magharibi wameona masilahi yao hayatalindwa na huyu raisi mpya? Poleni Somalia! Poleni Afrika
 
Slaa akienda kule ndo angejifunza kuwa na heshima na polisi
 
Ni Sheikh Mahmoud wa Somalia aliyechaguliwa juzi akimshinda Rais wa Serikali ya Mpito,Sheikh Sharrif Sheikh Ahmed. Rais Mahmoud alikuwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya ambaye pia alinusurika. Ni tukio la Mogadishu. Kazi inaendelea...
 
Hiyo ndiyo Somalia. Hawa jamaa wanapaswa kuvamiwa na mataifa yote jirani na kugawana nchi ili kuituliza vinginevyo itaendelea kuwa balaa kwa majirani zake.
 
ss dunia itambue kua hawajamaa somalia kusini si watu.kwani wenzao waliojitenga kaskazini wanaishi kwa amani
 
somaliland imefanikiwa kujenga aman demokrasia imeboresha maisha imefungua mashule na vyuo vikuu lakini hawajatambuliw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom