Soko la viatu vya Kimasai

banburydude1

Member
Oct 7, 2022
62
71
Wanajamii wenzangu wa JamiiForums,

Nimeunganishiwa deal ya kupeleka viatu vya Kimasai Ivory Coast na ndugu yangu wa ki Tanzania anayekaa na kufanya kazi kule.

Ombi langu kwenu, mwenye kujua taratibu za kufuata ili nipeleke pair 20 za viatu kule kwa kuanzia. Nahitaji kuwa na vibali kama export licence na vitu kama hivyo? Na kama ndiyo process ya kupata hivyo vibali ukoje?
PLEASE mwenye uelewa.

Asanteni.
 
Pair 20 upo serious kweli na biashara kweli? Au unaenda na mambo mengine hiyo pair 20 za kuchombezea tu??
 
Pair 20 upo serious kweli na biashara kweli? Au unaenda na mambo mengine hiyo pair 20 zakuchombezea tu??

Asante mwanajamii.
Naulizia kama kuna watu wanaosafirisha mizigo kwenda huko na taratibu zake. Kwenda mwenyewe na pair 20 tu Hapana labda baadae. Soko lipo tayari nimempa designs tofauti za hivyo viatu kapagawa, na kutaka pair 50 to start with.
 
Back
Top Bottom