Negotiator
JF-Expert Member
- Aug 9, 2010
- 303
- 44
Itakapofika October 31 mimi na familia yangu na jamaa zangu wa karibu hatutakua mmoja wa;
- wale watakaopigia kura wala kuunga mkono chama kilekile kinachokumbatia ufisadi.
- wale watakounga mkono wadogo zetu ndugu na jamaa kendelea kununua elimu kama bidhaa kutoka shule za serikali
- wale watakao unga mkono serikali iliyoshindwa kujenga uchumi imara na kulinda thamani ya shillingi yetu
- wale watakaomtukuza mgombea aliyedharau wafanyakazi, kuwabeza watoto wanaopata mimba wakiwa mashuleni na kunyanyapaa wenye VVU
- wale watakaoendeleza serikali iliyopelekea upatikanaji duni wa huduma za afya
- wale watakaoirejesha madarakani serikali iliyokubuhu katika matumizi holela ya kodi za wavujajasho wazalendo
- watakao ipa ushindi serikali ile ile isiyoheshimu katiba na sheria za nchi
- watakao ipa mwanya serikali isiyoheshimu uhuru wa vyombo vya habari