MchunguZI
JF-Expert Member
- Jun 14, 2008
- 4,009
- 2,171
Wana JF,
Asubuhi ya leo nimepata taarifa toka jimbo la Mh Sita kwamba Walinzi wake wamejeruhi watu wa PCCB na baadhi ya wajumbe wa CCM.
Jana jioni vijana wa PCCB wakiwa na mwenyekiti wa kitongoji ambacho leo hii kingetembelewa na wagombea wote, walivamia mkutano uliokuwa ukifanyika usiku kwa lengo la kuwaweka sawa wana-CCM kabla ya siku ya kampeni. Bila kutegemea Mh Sita pia alikuwepo na walinzi wake.
Bila kutegemewa wafuatiliaji hawa waliambulia kipigo. Mh. Sita bado ana walinzi toka serikalini aliopewa akiwa spika.
Nadhani magazeti yatakuwa yatapata undani huu maana nasikia wengine wamelazwa.
Asubuhi ya leo nimepata taarifa toka jimbo la Mh Sita kwamba Walinzi wake wamejeruhi watu wa PCCB na baadhi ya wajumbe wa CCM.
Jana jioni vijana wa PCCB wakiwa na mwenyekiti wa kitongoji ambacho leo hii kingetembelewa na wagombea wote, walivamia mkutano uliokuwa ukifanyika usiku kwa lengo la kuwaweka sawa wana-CCM kabla ya siku ya kampeni. Bila kutegemea Mh Sita pia alikuwepo na walinzi wake.
Bila kutegemewa wafuatiliaji hawa waliambulia kipigo. Mh. Sita bado ana walinzi toka serikalini aliopewa akiwa spika.
Nadhani magazeti yatakuwa yatapata undani huu maana nasikia wengine wamelazwa.