PROF NDUMILAKUWILI
JF-Expert Member
- Mar 25, 2016
- 10,520
- 13,113
Dereva huyo ambaye ameonekana kwenye video akiwa anaendesha gari aina ya Coaster ambayo inafanya safari zake Dodoma kwenda itigi akiwa anafanya kitendo cha hatari cha kuacha gari likiwa kwenye mwendo na kisha yeye kusimama na kuanza kucheza muziki huo akamatwa.
Kesho atapandishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazo mkabili yeye pamoja na wenzake ambao alikuwa nao kwenye Gari hilo.
Picha chini ni taarifa iliyotolewa na ROAD SAFETY AMBASSADORS(RSA)baada ya dereva huyo kukamatwa!
Hawa ndio wahusika walio kuwepo kwenye tukio hilo..
=======
POLISI mkoani Singida inamshikilia dereva wa gari dogo la abiria la Super Mamuu, kwa tuhuma za kuendesha kwa mwendo wa hatari.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Mayala Towo, alimtaja dereva anayeshikiliwa kuwa ni Saidi Juma (26) mkazi wa Dodoma ambaye inadaiwa siku ya tukio alikuwa anaendesha basi aina ya Nissan Civilian lenye namba za usajili T.360 DAY huku akicheza muziki.
Inaelezwa kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 4, mwaka huu, saa 11: 00 jioni katika Mji Mdogo wa Itigi wilayani Manyoni wakati mtuhumiwa akiwa na wenzake watatu, alipoendesha gari hilo kwa mwendo wa hatari kwa kucheza muziki huku akiachiana usukani na wenzake hao wakati gari hilo likiwa kwenye mwendo.
Kamanda Towo aliwataja watuhumiwa wengine ambapo pia wanashikiliwa na Polisi kuwa ni Joseph Ramadhan (27), Ezekiel Joseph (24) na Sebastian Godfrey (23) wote wakazi wa Majengo, Itigi.
Kesho atapandishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazo mkabili yeye pamoja na wenzake ambao alikuwa nao kwenye Gari hilo.
Picha chini ni taarifa iliyotolewa na ROAD SAFETY AMBASSADORS(RSA)baada ya dereva huyo kukamatwa!
Hawa ndio wahusika walio kuwepo kwenye tukio hilo..
=======
POLISI mkoani Singida inamshikilia dereva wa gari dogo la abiria la Super Mamuu, kwa tuhuma za kuendesha kwa mwendo wa hatari.
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Mayala Towo, alimtaja dereva anayeshikiliwa kuwa ni Saidi Juma (26) mkazi wa Dodoma ambaye inadaiwa siku ya tukio alikuwa anaendesha basi aina ya Nissan Civilian lenye namba za usajili T.360 DAY huku akicheza muziki.
Inaelezwa kuwa tukio hilo lilitokea Desemba 4, mwaka huu, saa 11: 00 jioni katika Mji Mdogo wa Itigi wilayani Manyoni wakati mtuhumiwa akiwa na wenzake watatu, alipoendesha gari hilo kwa mwendo wa hatari kwa kucheza muziki huku akiachiana usukani na wenzake hao wakati gari hilo likiwa kwenye mwendo.
Kamanda Towo aliwataja watuhumiwa wengine ambapo pia wanashikiliwa na Polisi kuwa ni Joseph Ramadhan (27), Ezekiel Joseph (24) na Sebastian Godfrey (23) wote wakazi wa Majengo, Itigi.