Simulizi yangu ya kwenda kwa waganga wa kienyeji sehemu mbalimbali nchini na nje ya nchi

Inaendelea

Nilifika Songea na kuanza kufanya biashara ya kununua na kuuza mahindi nilijichanganya na wazoefu biashara ikawa inaenda poa, pale nilipokuwa nimepanga kulikuwa na nyumba kama nne kwenye eneo moja kulikuwa kama kota,walipanga wafanyakazi na kuna jamaa wengine nao wafanyabishara wa mahindi na dili nyingine nyingi nyingi,dili chafu na safi walikuwa wamepanga pale pale.Nikaibiwa walivunja chumba changu na kikasafishwa kila kitu tene waliiba mchana,kuna vijana wawili walikuwa wamepigwa marufuku kuingia maeneo yale nilivyowaambia jamaa zangu wakawahisi wale vijana,wakaniambia nenda kwa Binti Ndembo ukawakomeshe,kipindi hiko Ruvuma kulikuwa na mganga anaitwa binti Ndembo alikuwa mashuhuri sana alikuwa anapatikana wilaya ya Namtumbo.

Sikwenda kwa binti Ndembo nilienda kwa mganga mmoja alikuwa anaishi karibu na msikiti wa mkoa nilifika kwake muda wa saa moja giza likiwa limeanza kuingia,nikaingia kwenye chumba cha uganga na kumuona mganga nikamueleza shida yangu akanisikiliza na kunitajia kiasi kidogo cha fedha ambacho aliniambia nitampa mara tu nitakavyopata vitu vyangu nikamuambia sawa,mganga akafanya uganga wake na alivyomaliza alianza kujaza upepo kwenye tyubu ya baiskeli aliniambia kadri anavyojaza na matumbo ya wale wezi nayo yatakuwa yanajaa
 
Inaendelea

Nilifika Songea na kuanza kufanya biashara ya kununua na kuuza mahindi nilijichanganya na wazoefu biashara ikawa inaenda poa, pale nilipokuwa nimepanga kulikuwa na nyumba kama nne kwenye eneo moja kulikuwa kama kota,walipanga wafanyakazi na kuna jamaa wengine nao wafanyabishara wa mahindi na dili nyingine nyingi nyingi,dili chafu na safi walikuwa wamepanga pale pale.Nikaibiwa walivunja chumba changu na kikasafishwa kila kitu tene waliiba mchana,kuna vijana wawili walikuwa wamepigwa marufuku kuingia maeneo yale nilivyowaambia jamaa zangu wakawahisi wale vijana,wakaniambia nenda kwa Binti Ndembo ukawakomeshe,kipindi hiko Ruvuma kulikuwa na mganga anaitwa binti Ndembo alikuwa mashuhuri sana alikuwa anapatikana wilaya ya Namtumbo.

Sikwenda kwa binti Ndembo nilienda kwa mganga mmoja alikuwa anaishi karibu na msikiti wa mkoa nilifika kwake muda wa saa moja giza likiwa limeanza kuingia,nikaingia kwenye chumba cha uganga na kumuona mganga nikamueleza shida yangu akanisikiliza na kunitajia kiasi kidogo cha fedha ambacho aliniambia nitampa mara tu nitakavyopata vitu vyangu nikamuambia sawa,mganga akafanya uganga wake na alivyomaliza alianza kujaza upepo kwenye tyubu ya baiskeli aliniambia kadri anavyojaza na matumbo ya wale wezi nayo yatakuwa yanajaa
ndo imeisha
 
Waungwana habari ya leo fuatana nami kwenye simulizi yangu hii ambapo niliwahi kwenda kwa waganga wa kienyeji sehemu mbalimbali nchini na nje ya nchi baada ya kukutana na changamoto mbalimbali za kimaisha.

Kiukweli ni vigumu kumjua yupi ni mganga wa kweli na yupi ni mganga feki ni kama vile ambavyo huwezi kumjua yupi ni mtumishi wa Mungu wa ukweli na yupi ni feki.Hali hiyo ilinifanya nihangaike kwa waganga mbalimbali ili kutatua changamoto zangu.

Wale ndugu zangu Walokole na Watakatifu wengine msiokuwa na dhambi mtanisamehe kwa hii simulizi.

Baada ya kumaliza masomo mwaka 2008 niliamua kurudi nyumbani kwetu Chunya na kujiajiri,sikupenda kuajiriwa kwa sababu kwetu Chunya marafiki zangu ambao nilisoma nao shule ya Msingi walikuwa wameishia darasa la saba walikuwa na pesa kushinda wasomi waliokuwa wameajiriwa na Serikali.

Hao marafiki zangu walikuwa machimboni kwa kuchimba au kununua dhahabu.Na Mimi nikajikita kwenye kuchimba lakini kabla ya hapo wakati nilipokuwa nasoma nilipokuwa napata nafasi nilikuwa naenda mgodini,ilikuwa rahisi kwenda machimboni kwa sababu kulikuwa na watu wengi niliokuwa nafahamiana nao.

Baada ya kuanza rasmi kuchimba madini niligundua machimboni kumetawaliwa na ushirikina wa hali ya juu,ndipo na mimi nikaanza kwenda kwa waganga wa kienyeji na kama ilivyo ada ukienda Roma ishi kama Waroma.Safari yangu ya kwenda kwa waganga ilianza kama ifuatavyo:

Mganga wa Ziwa Rukwa
Sikumbuki jina la kijiji ila kilikuwa karibu na ziwa Rukwa,nilienda kupitia Tunduma, naikumbuka barabara ilikuwa ya vumbi, milima, mabonde, miamba na yenye kona nyingi kali nilienda kwa kutumia fuso. Kijiji kilikuwa na Wafugaji wa Kisukuma wengi waliokuwa na mifugo mingi pamoja na wenyeji waliokuwa wakulima hodari wa mpunga kwenye bonde la ziwa Rukwa.

Niliipenda sana lugha ya Wenyeji kwani walikuwa wanaongea kama wanaimba au wanavuta maneno ,aina yao ya uongeaji ilinivutia sana.

Nilifika asubuhi na kumuona mganga,mganga mzee wa zaidi ya miaka sitini alikuwa hana vitu vingi vya kumtambulisha kama ni mganga wa kienyeji, nilimueleza sababu ya kwenda kwake akafanya uganga wake akaniambi usiku wa saa nane tutaenda kumalizia kufanyia uganga wake ziwani kwani huko ndiko kwenye mizimu yake, kutoka kwake hadi ziwa Rukwa kwa miguu ni saa mbili kwahiyo tulitoka kwake saa sita usiku ili tuweze kufika ziwani saa nane.

Tulitoka kwake watu wanne yaani mimi, mganga na watu wengine wawili, tulifika ziwani saa nane kasoro wakati tunaenda ilikuwa rahisi kwa sababu ilikuwa tunashuka tu kasheshe ilikuwa wakati wa kurudi kwani tulikuwa tunapandisha milima, usiku ule nilichoka sana.

Tulivyofika kwenye ufukwe wa ziwa mganga alituambia tugeuge tuangalie tulikotoka kisha alivua nguo zote akasisitiza tusimuangalie,wakati yeye anafanya uganga wake huku anaonge ongea maneno ambayo sikuyajua maana yake sisi wote watatu tulikuwa tunangalia pembeni.

Baada ya muda kidogo kukawa kimya, baada ya kama dakika tano nikasikia naitwa kwa kutajwa jina, sauti ilikuwa kubwa na yenye muungurumo, muda huo sehemu ile ya ziwa tulikuwa watu wanne tu sauti ile iliendelea kuniita lakini mtu aliyekuwa ananiita nilikuwa simuoni ila ilikuwa sauti ya mganga.

Sauti ilinitaka nielekee usawa wa ziwa, mimi kuogelea sijui ila sauti ilikuwa inanitaka niingie ziwani,wale jamaa wakaniambia kwa ukali niingie ziwani maana nilikuwa natembea kwa kusita sita, nilifika ziwani nikaingia kwenye maji nikawa naendelea kutembea kwenye maji kwa kusita sita sikuwa namuona mganga ila sauti nilikuwa naisikia ikiniambia niendelee kumfuta.

Niliendelea kutembea maji yalivyofika usawa wa magoti sauti ikanitaka nisimame nisiendelee kumfuata na mimi nikatii.
Itaendelea.

Sasa hivi najiandaa kwenda Mkwakwani kuwaona watani Yanga dhidi ya Coastal kwenye mechi yao itakayo chezwa saa kumi leo,nawatakia sare tu.

Nielekezeni jinsi ya kuipost hapa maana niliiandika yote imekamilika na ipo kwenye flash.
kutamka tu yanga umetukwaza wengine, inaonekana hii story Ni ya Simba tu, hivyo kwaheri ndugu yangu, machungu ninmengi Sina mda wa kuhangaika nawe
 
Waungwana habari ya leo fuatana nami kwenye simulizi yangu hii ambapo niliwahi kwenda kwa waganga wa kienyeji sehemu mbalimbali nchini na nje ya nchi baada ya kukutana na changamoto mbalimbali za kimaisha.

Kiukweli ni vigumu kumjua yupi ni mganga wa kweli na yupi ni mganga feki ni kama vile ambavyo huwezi kumjua yupi ni mtumishi wa Mungu wa ukweli na yupi ni feki.Hali hiyo ilinifanya nihangaike kwa waganga mbalimbali ili kutatua changamoto zangu.

Wale ndugu zangu Walokole na Watakatifu wengine msiokuwa na dhambi mtanisamehe kwa hii simulizi.

Baada ya kumaliza masomo mwaka 2008 niliamua kurudi nyumbani kwetu Chunya na kujiajiri,sikupenda kuajiriwa kwa sababu kwetu Chunya marafiki zangu ambao nilisoma nao shule ya Msingi walikuwa wameishia darasa la saba walikuwa na pesa kushinda wasomi waliokuwa wameajiriwa na Serikali.

Hao marafiki zangu walikuwa machimboni kwa kuchimba au kununua dhahabu.Na Mimi nikajikita kwenye kuchimba lakini kabla ya hapo wakati nilipokuwa nasoma nilipokuwa napata nafasi nilikuwa naenda mgodini,ilikuwa rahisi kwenda machimboni kwa sababu kulikuwa na watu wengi niliokuwa nafahamiana nao.

Baada ya kuanza rasmi kuchimba madini niligundua machimboni kumetawaliwa na ushirikina wa hali ya juu,ndipo na mimi nikaanza kwenda kwa waganga wa kienyeji na kama ilivyo ada ukienda Roma ishi kama Waroma.Safari yangu ya kwenda kwa waganga ilianza kama ifuatavyo:

Mganga wa Ziwa Rukwa
Sikumbuki jina la kijiji ila kilikuwa karibu na ziwa Rukwa,nilienda kupitia Tunduma, naikumbuka barabara ilikuwa ya vumbi, milima, mabonde, miamba na yenye kona nyingi kali nilienda kwa kutumia fuso. Kijiji kilikuwa na Wafugaji wa Kisukuma wengi waliokuwa na mifugo mingi pamoja na wenyeji waliokuwa wakulima hodari wa mpunga kwenye bonde la ziwa Rukwa.

Niliipenda sana lugha ya Wenyeji kwani walikuwa wanaongea kama wanaimba au wanavuta maneno ,aina yao ya uongeaji ilinivutia sana.

Nilifika asubuhi na kumuona mganga,mganga mzee wa zaidi ya miaka sitini alikuwa hana vitu vingi vya kumtambulisha kama ni mganga wa kienyeji, nilimueleza sababu ya kwenda kwake akafanya uganga wake akaniambi usiku wa saa nane tutaenda kumalizia kufanyia uganga wake ziwani kwani huko ndiko kwenye mizimu yake, kutoka kwake hadi ziwa Rukwa kwa miguu ni saa mbili kwahiyo tulitoka kwake saa sita usiku ili tuweze kufika ziwani saa nane.

Tulitoka kwake watu wanne yaani mimi, mganga na watu wengine wawili, tulifika ziwani saa nane kasoro wakati tunaenda ilikuwa rahisi kwa sababu ilikuwa tunashuka tu kasheshe ilikuwa wakati wa kurudi kwani tulikuwa tunapandisha milima, usiku ule nilichoka sana.

Tulivyofika kwenye ufukwe wa ziwa mganga alituambia tugeuge tuangalie tulikotoka kisha alivua nguo zote akasisitiza tusimuangalie,wakati yeye anafanya uganga wake huku anaonge ongea maneno ambayo sikuyajua maana yake sisi wote watatu tulikuwa tunangalia pembeni.

Baada ya muda kidogo kukawa kimya, baada ya kama dakika tano nikasikia naitwa kwa kutajwa jina, sauti ilikuwa kubwa na yenye muungurumo, muda huo sehemu ile ya ziwa tulikuwa watu wanne tu sauti ile iliendelea kuniita lakini mtu aliyekuwa ananiita nilikuwa simuoni ila ilikuwa sauti ya mganga.

Sauti ilinitaka nielekee usawa wa ziwa, mimi kuogelea sijui ila sauti ilikuwa inanitaka niingie ziwani,wale jamaa wakaniambia kwa ukali niingie ziwani maana nilikuwa natembea kwa kusita sita, nilifika ziwani nikaingia kwenye maji nikawa naendelea kutembea kwenye maji kwa kusita sita sikuwa namuona mganga ila sauti nilikuwa naisikia ikiniambia niendelee kumfuta.

Niliendelea kutembea maji yalivyofika usawa wa magoti sauti ikanitaka nisimame nisiendelee kumfuata na mimi nikatii.
Itaendelea.

Sasa hivi najiandaa kwenda Mkwakwani kuwaona watani Yanga dhidi ya Coastal kwenye mechi yao itakayo chezwa saa kumi leo,nawatakia sare tu.

Nielekezeni jinsi ya kuipost hapa maana niliiandika yote imekamilika na ipo kwenye flash.
ila mi Ni Simba dam dam, sijapenda tu ulivyohusisha ushabiki na story yako, hkukuwa na sababu Wala maana
 
akiishusha yote naomba nishtue maana huyu mapicha picha kaanza mapema sana
kweli jamani, Mimi pia mnitag, Mana uyu fala anajiona tuna shida Sana na story yake, Yani imekua trend Sasa jf, kwamba itaendeleaaa, naomba muwaambie mods kwamba hi Ni trend inatusumbua Sana wateja wao waipige ban, yaani unasema tu itaendeleaaa inakuwa ban ya miezi sita, Kuna wale wanaweka mwendelezo kwa link kwenye post yao ya Kwanza, wapewe heshima na ulinzi wa jkt
 
Nikamwambia sawa endelea akaanza kujaza tyubu ikawa inajaa mwishowe mpira ukapasuka mganga akaniambia tushaua,nilistuka nikamuuliza unasemaje akarudia tushaua kwa sababu Mpira ulivyopasuka na matumbo ya wezi nayo yatakuwa yamepasuka,nikamuuliza sasa tunafanyaje akaniambia ondoka urudi kesho nikamwambia sawa,nikarudi getoni huku nawaza naanza tena kununua vitu.

Nikafika geto nikawasimulia jamaa zangu kilichotokea,walichukia sana nilipowaeleza sikwenda kwa binti Ndembo lengo lao lilikuwa kusikilizia kama binti Ndembo ni mganga kweli au la.
Wale vijana sikuwahi kuwaona tens.

Jamaa walikuwa magijwi wa kuzunguka kwa waganga, walikuwa wanaenda Msumbiji, Congo kufuata waganga.

Niliendelea kufanya biashara yangu ya mahindi wakati huo Mdigo alikuwa kaenda Msumbiji kununua magari mabovu na kuyaleta Tanzania na kutatengeneza kisha kuyauza,huyu Mdigo walikuwa na uwezo mkubwa wa kutambua fursa mapema ingawa naye alikuwa bingwa kwenye mambo ya ushirikina.

Baada ya Mdigo kuondoka na Mimi nilihama kwenye zile nyumba nikaenda kupanga kwenye nyumba moja ipo mtaa wa Mahenge,nilihama kwa sababu jamaa nilikuwa siendani nao pia biashara yao chafu ingeweza kusababisha tusombwe nyumba nzima.

Sababu nyingine ya kuhama nilikuwa nimepata demu mmoja anaitwa Y myao kutoka Tunduru alikuwa anakatika kuliko panga boi,alikuwa fundi kweli kweli,ningempeleka pale kwa jamaa zangu wangembeba tu,maana wao kuchangia demu kwao ilikuwa kitu cha kawaida.Pamoja na ufundi wake Y alikuwa mkorofi sana Mara kwa Mara tulikuwa tunagombana kwa sababu za kipuuzi na Mimi nilikuwa siyo mnyonge akizingua nilikuwa namzingua Mara mbili yake,Y akapata mimba,usiku wa SAA 4 anaweza akakuagiza ukamnunulie Coca cola,nilikuwa kijana Mdogo sijui lolote akiagiza hivyo lazima nimwambie maneno ya kijeuri ambayo alikuwa anachukia sana.

Ugomvi ukawa unaendelea mwishowe akaniambia naenda kutoa mimba yako nikamwambia nenda,nikampa elfu 30 akaenda kutoa,usiku akaja geto kulala lakini Siku hiyo hatukulala tumbo lilikuwa linamuuma akawa anajinyonga nyonga usiku kucha,sababu ya kuumwa ni kuna vitu walivisahau kuvitoa,Siku ile nilijua atakufa,SAA Tisa usiku nikazima taa zote za nje na ndani nikatoka nje ,pale nyumbani kwa nyuma kulikuwa na korongo kubwa nikawa naenda kuangalia njia nitakayoitumia kwenda kutupa maiti ya Y ikitokea amekufa.

Y hakufa lakini kama ningefanya vile ungekuwa uamuzi wa kipumbavu sana maana MTU wa kwanza kukamatwa ingekuwa mimi,watu wengi waliujua uhusiano wetu.
Nikarudi ndani Y alikuwa anaendelea kuugulia maumivu makali sana huku anajinyonga nyonga nilimuonea huruma sana.Nilikuwa sijaenda kanisani miaka mingi lakini Siku ile nilijikuta nasali sala zote,nilipiga magoti ,nilinyanyuka nikawa natembea huku naomba kama Walokole.

SAA 11 asubuhi Y bado alikuwa anaugulia maumivu makali nikapiga simu kuita boda boda ikaja ikampeleka kwa Daktari aliyemtoa mimba.
Mchana akawa amepona baada ya kwenda kutolewa vitu vilivyosahaulika.
Ukorofi uliendelea tukaachana.

Siku moja nilikuwa geto nikapigiwa simu kuna tajiri anataka mzigo nikaenda kumuona alikuwa kijana mmoja kutoka Njombe jamaa zangu waliniunganishia nikaenda nikamkuta kijana Mdogo mwenye mwili mdogo,walikuwa wanakunywa na kufanya maongezi na Mimi nikajiunga nao.
Nikafanya maongezi na tajiri tukakubaliana kesho yake atapakia mzigo na kulipa fedha zote,tajiri alikuwa anawanunulia pombe jamaa zangu lakini hela alikuwa anazitoa kwenye diary, nilijiuliza maswali mengi sana,alikuwa anafunua diary na kutoa fedha,hela zilikuwa haziishi wala diary haionekani kutuna.

Kesho yake muda wa SAA mbili usiku tajiri akalipa fedha milioni nane nikazichukua nikaenda nazo geto nikafunga mlango nikaziweka kwenye begi wala sikutoka Siku ile.
Asubuhi hakukuwa hata na buku,begi halijafunguliwa mlango umefungwa lakini fedha hazipo.Nilichanganyikiwa.
Nikaenda kijiweni kwa jamaa zangu nikawaeleza majanga ya
liyonikuta walisikitika sana wakasema itakuwa tajiri kazivuta.
Nikarudi geto huku nimechanganyikiwa nilijiuliza maswali mengi sana nakumbuka machozi yalinitoka.
Jioni nikaona namba ngeni inaingia kwenye simu yangu mtandao wa MCEL wa Msumbiji alikuwa Mdigo akaniambia Msomi nasikia wamekupiga,aliendelea kusema na ukiendelea na usomi wako watakupiga sana.Ingawa nilikuwa naenda kwa waganga lakini sikuwa nakubali
sana mambo hayo mazingira tu yalinilazimisha.
Siku ile niligundua naishi kwenye Dunia ya ushirikina ,nikatamani niajiriwe yaani nianze kuhangaika kutafuta ajira, nikakumbuka ajira walizokuwa wanafanya niliomaliza nao chuo, lakini nikikumbuka mishahara yao ya laki sita nikasema wacha niendelee kuishi kama wanavyotaka, yaani niendeleze ushirikina.

Kule machimboni Chunya kuna dogo mmoja nilipomaliza shule ya msingi nilimuacha madarasa manne,yeye alianza kuchimba zamani kwahiyo alibahatika kupata hela. Siku moja tuligombana aliniambia braza wewe umenizidi elimu na umri tu...Yalikuwa maneno ya ukweli ila yaliniuma.Kila nikiyakumbuka Yale maneno huwa nazidi kupata hasira niliapa ipo Siku nitamzidi elimu,umri na fedha.

Nikapanda pikipiki nikaelekea kwa mganga alikuwa anaishi kijiji kimoja kabla hujafika Namatuhi barabara ya kwenda Msumbiji.
Nilishaanza kuwa gwiji kwenye mambo hayo.Nilifika kwa mganga asubuhi sana nilienda kwa masuala mawili tu nizipate fedha zangu na nisiibiwe tena kizembe.

Itaendelea.
 
Apig
kweli jamani, Mimi pia mnitag, Mana uyu fala anajiona tuna shida Sana na story yake, Yani imekua trend Sasa jf, kwamba itaendeleaaa, naomba muwaambie mods kwamba hi Ni trend inatusumbua Sana wateja wao waipige ban, yaani unasema tu itaendeleaaa inakuwa ban ya miezi sita, Kuna wale wanaweka mwendelezo kwa link kwenye post yao ya Kwanza, wapewe heshima na ulinzi wa jkt
Mkuu unamlipa nn? Ana kazi zake yaani kuna watu hamjielewagi eti na komandi juu kwani unalipa?
 
Daraja la miti
Kama upo kweli Mkwawani njoo upande wa jukwaa kuu kulia, tafuta mtu aliyevaa t-shirt ya njano isiyo na maandishi na nimevaa kofia nyeupe, pembeni yangu yupo mwanamsimbazi na jezi yake.

Kama una smartphone nina OTG hapa nitakuwekea story yote kupitia simu yako alafu utapost mwenyewe.
Thanks,nilichelewa kuiona,hata hivyo nilitoka mapema goli la pili la wagosi sikuliona.
 
Inaendelea

Baadhi ya watu hasa washika dini najua nawakera lakini simulizi kama hizi mnaweza kuziepuka kwa kutokuzisoma.
Ila msibague dhambi hata zingine msiwe mnazifanya maana kuna kiongozi mmoja mkubwa sana wa dini hapa Tanzania anatembea na mke wa mtu

Nilionana na mganga nikamueleza shida yangu akaniambia nenda kalete nyoya kubwa la mkiani LA jogoo linaloangalia juu,Siku ile ndipo nilipogundua kuwa kwenye Yale manyoya ya jogoo ya mkiani makubwa jogoo wengine yao yanayoangalia juu na wengine chini.

Ikabidi niende sokoni kununua jogoo kwa ajili ya kupata nyoya tu,lakini nilikuwa na mawenge nikanunua mwenye nyoya linaloangalia chini,nikalipeleka kwa mganga akalikataa akaniambia kalete linaloangalia juu,nikaenda tena kununua LA jogoo linaloangalia juu.
Nikampelekea mganga akafanya uganga wake akachanganya na dawa nyingine akanipa karatasi akaniambia niandike ninayoyataka nikaandika akachukua ile karatasi akachanganya na lile nyoya na madawa yake akaniambia niongozane na msaidizi wake tupande mlima tukachome dawa mlimani,ila tukianza tu kupanda hakuna kuongea,huo mlima alikuwa anautumia kwa shughuli zake za uganga na matambiko tukapanda mlimani na kiberiti ,mlimani kulikuwa na upepo mkali sana,kila tukiwasha njiti inazima kwa sababu ya upepo ikabidi tushuke chini.
 
Moja ya kitu ulichoshindwa kukifuata katika simulizi yako ni utaratibu, yaani umechemsha kwelikweli Daraja la miti yaani umeanza vizuri, baadaye umechanganya soda, energy drink na gambe humo humo nadhani maji yatakuwa chini 😷!.
 
Semina za kipuuzi kma hizi mi sinaga time nazo kabisa😂😂😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom