Simiyu: Ahukumiwa kuchapwa viboko 8 kwa kosa la ubakaji

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,309
5,464
photo_2023-09-12_08-12-10.jpg
Mahakama ya Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu imemhukumu Boniphace Abel (18) mkazi wa Nyashimba Magu Mkoani Mwanza adhabu ya kuchapwa viboko nane (8) kwa kosa la kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka 17 na kumsababishia majeraha.

Mbali na adhabu hiyo, Mshtakiwa ametakiwa na Mahakama hiyo kumlipa Mwathirika kiasi cha Sh. 300,000 (Laki tatu) kama fidia kutokana na kitendo alichomfanyia.

Hakimu wa Mahakama hiyo Robert Kaanwa, wakati akitoa hukumu hiyo ameamuru Mshitakiwa kupimwa kwanza Afya yake na Daktari kama anaweza kuhimili adhabu hiyo ya viboko.

Awali, kabla ya hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Wilaya Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Jaston Mhule alielezea Mahakama kuwa Mshitakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 130(1)(2)e na 131(2) vya Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kama ilivyo fanyiwa marejeo Mwaka 2022.

Mhule ameeleza kuwa Mshtakiwa akiwa katika msiba wa Babu yake mnamo tarehe 10/07/2023 huko Kijiji cha Mahembe ndani ya Wilaya Itilima alimbaka mhanga mwenye umri wa Miaka 17 na kumsababishia maumivu.

Mhule amesema Sheria inaweza isizungume moja kwa moja muathirika kupewa fidia lakini Mahakama inaweza kuamua hivyo kutokana na kusikiliza pande, ndipo inaweza kuamua fidia au la.

Kifungu cha 131 Kifungu Kidogo cha Pili cha Sheria Kanuni ya Adhabu inaeleza kama mshtakiwa wa kesi ya ubakaji akiwa na umri wa miaka 18 kushuka chini adhabu yake ni viboko tu, idadi ya itategemea na afya ya mhusika.

Mshtakiwa kabla ya kuchapwa viboko inatakiwa afanyiwe vipimo vya afya na Daktari atoe cheti cha kuonesha kuwa kwa idadi vya viboko ambayo amehukumiwa na Mahakama inaweza kumfaa au inatakiwa kupunguziwa adhabu.

Sheria inaeleza mshtakiwa wa ubakaji akiwa na umri wa miaka 19 kuendelea akikutw ana hatia kifungo cha chini ni miaka 30 na inaweza kwenda mbele zaidi ya hapo hadi kuwa kifungo cha maisha.
 
Mahakama ya Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu, imemhukumu Boniphace Abel (18) mkazi wa Nyashimba Magu Mkoani Mwanza adhabu ya kuchapwa viboko Nane (8) kwa kosa la kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka 17 na kumsababishia majeraha.

Mbali na adhabu hiyo, Mshitakiwa ametakiwa na Mahakama hiyo kumlipa Mwathirika kiasi cha Sh. 300,000 (Laki tatu) kama fidia kutokana na kitendo alichomfanyia.

Hakimu wa Mahakama hiyo Robert Kaanwa, wakati akitoa hukumu hiyo ameamuru Mshitakiwa kupimwa kwanza Afya yake na Daktari kama anaweza kuhimili adhabu hiyo ya viboko.

Awali kabla ya hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Wilaya Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Jaston Mhule alielezea Mahakama kuwa Mshitakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 130(1)(2)e na 131(2) vya sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyo fanyiwa marejeo mwaka 2022.

Mhule ameeleza kuwa Mshitakiwa akiwa katika msiba wa Babu yake ,mnamo tarehe 10/07/2023 huko Kijiji cha mahembe ndani ya wilaya itilima alimbaka mhanga mwenye umri wa Miaka 17 na kumsababishia maumivu.
Hakubaka huyo, wote wanalingana rika, hiyo ni "ashki majnun".

Kiislam hapo litakiwa walambwe viboko wote wawili halafu waowane.

Hao vijana ni afadhali kuliko wale wanaofanya ushoga na kusagana.
 
Mahakama ya Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu, imemhukumu Boniphace Abel (18) mkazi wa Nyashimba Magu Mkoani Mwanza adhabu ya kuchapwa viboko Nane (8) kwa kosa la kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka 17 na kumsababishia majeraha.

Mbali na adhabu hiyo, Mshitakiwa ametakiwa na Mahakama hiyo kumlipa Mwathirika kiasi cha Sh. 300,000 (Laki tatu) kama fidia kutokana na kitendo alichomfanyia.

Hakimu wa Mahakama hiyo Robert Kaanwa, wakati akitoa hukumu hiyo ameamuru Mshitakiwa kupimwa kwanza Afya yake na Daktari kama anaweza kuhimili adhabu hiyo ya viboko.

Awali kabla ya hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Wilaya Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Jaston Mhule alielezea Mahakama kuwa Mshitakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 130(1)(2)e na 131(2) vya sheria ya kanuni ya adhabu sura ya 16 kama ilivyo fanyiwa marejeo mwaka 2022.

Mhule ameeleza kuwa Mshitakiwa akiwa katika msiba wa Babu yake ,mnamo tarehe 10/07/2023 huko Kijiji cha mahembe ndani ya wilaya Itilima alimbaka mhanga mwenye umri wa Miaka 17 na kumsababishia maumivu.
Kwa hiyo Watoto walibakana 🤣🤣
 
Sasa Kwa nini mhusika alipeleka kesi Mahakamani?
Utakuta kasshinikizwa, au ni wazazi au walezi au jamii.

Wangapi wadogo kuliko huyo wanalambwa mimba kiulaini na mambo yanaishia kwenye mabaraza ya kifamilia au kijuujuu tu.

Kuna mila Tanzania hii mtoto wa kike alivunja uongo tu kama hajashulikiwa anasakamwa kwao.

Hali kashalika kama mvulana hajaanza kuonesha urijali wake mapema.

Tanzania kesi kama hizo inatakiwa hakimu atumie hekima sana, kuna sheria za dola, kuna sheria za dini na kuna sheria za kimila na zote zinatumika kwa namna moja au nyengine.
 
Back
Top Bottom