Mbabani
JF-Expert Member
- Jun 20, 2022
- 1,171
- 3,359
Habari wanamichezo.
Hivi karibuni zimeibuka tetesi Simba SC wanahitaji kuajiri kocha mkuu na kocha anaepewa nafasi kubwa ni yule Mbrazil wa Vipers.
Kwa mtazamo wangu naona Simba SC wanajiandaa kuivuruga timu na kuanza moja.
Kuhitaji kocha mpya kwa sasa huku timu ikiwa kwenye mbio za ubingwa ni kurudisha nyuma maendeleo ya timu hasa kiuchezaji, bado siku 40+ michuano ya klabu bingwa ianze je Simba SC wanatarajia nini?
Ikumbukwe ujio wa kocha mpya kwa sasa kunaweza kuathiri viwango vya baadhi ya wachezaji hivyo kupelekea timu kufeli kufikia malengo.
Kocha Mgunda anatosha vyema, kinachotakiwa kwa sasa Simba ni kujaza nafasi walizo puyanga katika usajili wa dirisha kubwa. Kikosi cha Simba kimekosa Mshambuliaji mahiri na kiungo mkabaji mahiri.
Wachezaji hawa walikuja kujaza nafasi tu ila viwango vyao ni vya kawaida.
1. Dejan (Mshambuliaji) ameshaondoka.
2. Outtara (beki wa kati)
3. Nelson Okwa (Kiungo mshambuliaji)
4. Victor Akpan (Kiungo mkabaji) usajili mbovu kabisa (uwezo anazidiwa na Majogoro)
Iwapo Simba SC itasajili wachezaji wa viwango vya juu kuziba nafasi hizo 4 ambapo nafasi moja tayari Ntibazonkiza ameshasajiliwa basi haina haja ya kocha mpya.
Watu wanaohusika kwenye usajili watazame pia nafasi hizi:-
1. Beki wa kulia (Kapombe hana mbadala sahihi)
2. Beki wa kushoto (Gadiel Michael uwezo wake umeshuka)
3. Beki wa Kati (Onyango sio kuaminika sana, Kennedy amefeli kushindana na Onyango)
4. Kiungo Mkabaji wa viwango vya CAF (hizi tetesi za kutaka kumsajili Nashon wa Geita Gold naona Simba hawapo siriazi kabisa)
Mgunda akipewa wachezaji sahihi na imani ataifikisha timu mbali.
Kama ni habari za kocha mpya, subirini msimu uishe ndiyo muajiri kocha mpya lakini pia aje na wasaidizi wake.
Hivi karibuni zimeibuka tetesi Simba SC wanahitaji kuajiri kocha mkuu na kocha anaepewa nafasi kubwa ni yule Mbrazil wa Vipers.
Kwa mtazamo wangu naona Simba SC wanajiandaa kuivuruga timu na kuanza moja.
Kuhitaji kocha mpya kwa sasa huku timu ikiwa kwenye mbio za ubingwa ni kurudisha nyuma maendeleo ya timu hasa kiuchezaji, bado siku 40+ michuano ya klabu bingwa ianze je Simba SC wanatarajia nini?
Ikumbukwe ujio wa kocha mpya kwa sasa kunaweza kuathiri viwango vya baadhi ya wachezaji hivyo kupelekea timu kufeli kufikia malengo.
Kocha Mgunda anatosha vyema, kinachotakiwa kwa sasa Simba ni kujaza nafasi walizo puyanga katika usajili wa dirisha kubwa. Kikosi cha Simba kimekosa Mshambuliaji mahiri na kiungo mkabaji mahiri.
Wachezaji hawa walikuja kujaza nafasi tu ila viwango vyao ni vya kawaida.
1. Dejan (Mshambuliaji) ameshaondoka.
2. Outtara (beki wa kati)
3. Nelson Okwa (Kiungo mshambuliaji)
4. Victor Akpan (Kiungo mkabaji) usajili mbovu kabisa (uwezo anazidiwa na Majogoro)
Iwapo Simba SC itasajili wachezaji wa viwango vya juu kuziba nafasi hizo 4 ambapo nafasi moja tayari Ntibazonkiza ameshasajiliwa basi haina haja ya kocha mpya.
Watu wanaohusika kwenye usajili watazame pia nafasi hizi:-
1. Beki wa kulia (Kapombe hana mbadala sahihi)
2. Beki wa kushoto (Gadiel Michael uwezo wake umeshuka)
3. Beki wa Kati (Onyango sio kuaminika sana, Kennedy amefeli kushindana na Onyango)
4. Kiungo Mkabaji wa viwango vya CAF (hizi tetesi za kutaka kumsajili Nashon wa Geita Gold naona Simba hawapo siriazi kabisa)
Mgunda akipewa wachezaji sahihi na imani ataifikisha timu mbali.
Kama ni habari za kocha mpya, subirini msimu uishe ndiyo muajiri kocha mpya lakini pia aje na wasaidizi wake.