engmtolera
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 5,150
- 1,437
Sosthenes Nyoni
NDOTO ya mabingwa wa Tanzania, Simba kusombe kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika imebaki hadithi baada kupokea kipigo cha mabao 3-2 kutoka kwa TP Mazembe jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mabingwa hao mara mbili wa Afrika, waliuanza mchezo huo kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la kuongoza dakika ya 18, kupitia mshambuliaji wake Given Singuluma aliyeunganisha vizuri mpira wa kona uliopigwa na Patou Kabangu.
Shija Mkina aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Juma Jabu aliyeumia alipatia Simba bao la kusawazisha dakika 58, kufutia mpira wake wa krosi kwenda moja kwa moja wavuni na kumwacha Kidiaba Robert asijue la kufanya.
Mshambuliaji Allan Kaluyituka alipatia Mazembe bao la pili dakika 63, baada ya kuwazidi ujanja mabeki wa Simba, kabla ya Mbwana Samatta kuisawazishia tena Simba dakika ya 65, akiunganisha kwa kichwa mpira wa kona wa Amri Maftah kufanya matokeo hayo kuwa 2-2.
Nyota wa Zambia, Singuluma alimaliza ubishi kwa kupachika bao la tatu dakika 73, baada ya kupokea pasi nzuri ya Kaluyituka na kupiga shuti lilomshinda Juma Kaseja na kujaa wavuni.
Simba watajilaumu wenye kwa kupoteza nafasi nyingi za kufunga katika kipindi cha kwanza baada ya washambuliaji wake Samatta, Emmanuel Okwi na Mussa Mgosi kupoteza nafasi nyingi za wazi.
Dakika ya 3, Mgosi alishindwa kumalizia kona ya Okwi baada ya mpira wake wa kichwa kupaa juu, lakini mashabiki wa Simba wataikumbuka nafasi nzuri aliyokosa Samatta baada ya kumtoka beki wa Mazembe, Stopila Sunzu na kubaki yeye na kipa, lakini shuti lake lilidakwa na Robert Kidiaba.
Katika mchezo huo Simba walitawala sana sehemu ya kiungo na kufanya mashambulizi mengi, huku wapinzani wao wakicheza kwa kujihami na kufanya mashambulizi ya kushitukiza na kupiga mashuti ya mbali.
Awali mashabiki wanaodaiwa kuwa wa TP Mazembe walipambana na Polisi wakati wakijaribu kuingia kwenye jukwaa ambalo hakustahili kukaa.
NDOTO ya mabingwa wa Tanzania, Simba kusombe kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika imebaki hadithi baada kupokea kipigo cha mabao 3-2 kutoka kwa TP Mazembe jana kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mabingwa hao mara mbili wa Afrika, waliuanza mchezo huo kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la kuongoza dakika ya 18, kupitia mshambuliaji wake Given Singuluma aliyeunganisha vizuri mpira wa kona uliopigwa na Patou Kabangu.
Shija Mkina aliyeingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Juma Jabu aliyeumia alipatia Simba bao la kusawazisha dakika 58, kufutia mpira wake wa krosi kwenda moja kwa moja wavuni na kumwacha Kidiaba Robert asijue la kufanya.
Mshambuliaji Allan Kaluyituka alipatia Mazembe bao la pili dakika 63, baada ya kuwazidi ujanja mabeki wa Simba, kabla ya Mbwana Samatta kuisawazishia tena Simba dakika ya 65, akiunganisha kwa kichwa mpira wa kona wa Amri Maftah kufanya matokeo hayo kuwa 2-2.
Nyota wa Zambia, Singuluma alimaliza ubishi kwa kupachika bao la tatu dakika 73, baada ya kupokea pasi nzuri ya Kaluyituka na kupiga shuti lilomshinda Juma Kaseja na kujaa wavuni.
Simba watajilaumu wenye kwa kupoteza nafasi nyingi za kufunga katika kipindi cha kwanza baada ya washambuliaji wake Samatta, Emmanuel Okwi na Mussa Mgosi kupoteza nafasi nyingi za wazi.
Dakika ya 3, Mgosi alishindwa kumalizia kona ya Okwi baada ya mpira wake wa kichwa kupaa juu, lakini mashabiki wa Simba wataikumbuka nafasi nzuri aliyokosa Samatta baada ya kumtoka beki wa Mazembe, Stopila Sunzu na kubaki yeye na kipa, lakini shuti lake lilidakwa na Robert Kidiaba.
Katika mchezo huo Simba walitawala sana sehemu ya kiungo na kufanya mashambulizi mengi, huku wapinzani wao wakicheza kwa kujihami na kufanya mashambulizi ya kushitukiza na kupiga mashuti ya mbali.
Awali mashabiki wanaodaiwa kuwa wa TP Mazembe walipambana na Polisi wakati wakijaribu kuingia kwenye jukwaa ambalo hakustahili kukaa.