Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,798
- 12,240
Moja ya vitu vinavyotafuna rasilimali za nchi hii ni sikukuu za kitaifa za serikali. Mbali na sikukuu zipatazo 15 za kitaifa za serikali na dini ambazo ni rasmi, kuna sikukuu zisizo na idadi za serikali ambazo hutumia fedha nyingi kuziadhimisha. Inaelekea kila siku ya Mungu nchi hii kuna sikukuu! Chache ninazozikumbuka:
- Siku ya kupanda miti,
- Siku ya Ukimwi
- Siku ya kifua kikuu
- Wiki ya maji
- Wiki ya mazingira
- Siku ya manesi
- Siku ya utepe mweupe
- Siku ya walemavu
- Siku ya watoto yatima
- Siku ya ushirika
- Wiki ya nenda kwa usalama
- Siku ya haki za binadamu
- Siku ya vyombo vya habari
- Siku ya chanjo ya polio
- Wiki ya maonyesho ya biashara za ndani
- Wiki ya maonyesho ya biashara za nje a.k.a sabasaba
- Wiki ya maonyesho ya kilimo a.k.a. nanenane