Siku ya Ukimwi Duniani- Lets talk about our experiences!!!!

Kana-Ka-Nsungu

JF-Expert Member
Oct 4, 2007
2,257
353
'Would you like to test for HIV too?, we recommend it to people who have lived in Africa and Asia' Aliniuliza Daktari huku akinitazama usoni, nikajikuta nimeropokwa...'Yeah, I wont mind!'. Japokuwa nilikuwa nimeenda hospitali kwa matatizo mengine, nilijikuta nimefanya uamuzi mkubwa sana kiafya kwa mara ya kwanza katika maisha yangu na to be honest- I suffered for a good one week hadi nilipopata matokeo yangu.

Nilitamani sana majibu yangekuwa yanatoka papo kwa papo lakini niliambiwa ingebidi nisubiri kwa wiki nzima. Nikaanza kukumbuka vimeo vyoooote nilivyowahi kuvipitia, usiku nilikuwa silali bila kupiga mbili tatu ili nipate usingizi, nikaona haitoshi nikanunua kadi ya simu nikaanza kuwapigia washkaji bongo. 'I see hivi yule demu wangu flani wa zamani yuko wapi siku hizi' ndo lilikuwa swali kuu. Mara nyongo ikantumbukia katika ulizia ulizia yangu, moja ya mademu niliopitia nikaskia kavuta, moyo ukaanza kwenda mbio, nikamuuliza mshkaji ' Nini kilimsibu jamani?', akajibu 'Alifariki kwenye ajali ya gari'....nikashusha pumzi mhhhh....huku moyoni nikijisemea 'aah...hiyo poa!!'

Katika wazawaza yangu nikaanza kuwakumbuka ndugu zangu wote ambao ukimwi umewachukua. Mwaka 94 bado nakumbuka, Binamu yangu ndo kwanza kazi alikuwa kaipata TRA wakamuweka kwenye Road tolls, hela akazikamata kwa sana na mabinti nao wakaongezeka, hakutaka kusubiri watu wambadilishe nepi na kuuguza madonda- alijiua punde tu baada ya kugundua kuwa ana ngoma.

Mtoto wa mama mkubwa, mi nilikua namuita dada, sura na maumbile alikuwa kajaliwa. Ndoa yake ilipovunjika, akaanza kufanya biashara za kusafiri, mara leo Tanga kesho Boarder Taveta. Naskia alikuwa hana hiyana katika safari zake, I guess alikuwa concerned zaidi na 'cost cutting and profit maximisation' kuliko uhai wake, akiwa safarini akipata atakayemnunulia chakula na kumpa malazi- twende kazini! Akapata bwana ambaye naye alikuwa ni mfanyabiashara wa kusafiri, walikuwa wanaonana mara mojamoja kwa kuwa wote walikuwa ni watu wa kusafiri, akaamua kumzalia!Mara ya mwisho nilipomuona 2006 machozi yalinitiririka, siku sio nyingi baada ya kuondoka Bongo nikaskia wamemzika, mtoto aliyeachwa ana kila dalili za uathirika.

Binamu yangu huyu, nilimpenda sana, alikuwa ni mrembo haswa lakini nahisi alifika mahali akawa desperate kuingia kwenye relationship. Sijui hata alikutania wapi na huyu mwanajeshi!! jamaa akamuoa na chapchap akampiga mimba- baada tu ya kuzaa, binamu afya yake ikadhoofika na mauti yakamchukua. She was so innocent, huyu mjeshi alikuwa akienda kwenye kituo chake cha kazi anakaa huko for 3-6 months ndo anarudi kumuona mkewe na hadi leo sijui ni kwanini alikuwa haendi naye.


Kwakweli nilipata nafasi ya kuwaza mengi, nikawakumbuka pia marafiki zangu ambao wametangua mbele ya haki kwa sababu zinazohisiwa kuwa ni UKIMWI, siwezi kuwapa story zao hapa kwa kuwa am not sure na watu hawasemi hadi leo hii kama ndugu zao wakifa kwa UKIMWI, utaskia 'shinikizo la damu' au 'marehemu amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu'!

Majibu niliambiwa nigeyapata kwa text jumanne iliyopita kati ya saa 3 asubuhi na 11 jioni, basi siku hiyo hadi napata majibu yangu kila text iliyokuwa ikiingia ilikuwa kama hivi mtu kanichoma kisu! Mapigo ya moyo yananiongezeka huku nikitetemeka. Mishale ya saa nane nikakiona kitu kimeingia toka namba ya kiofisi, kufungua 'All results negative'!

Nice weekend, kama unaweza kapime kama mimi japokuwa sishauri kama una moyo mwepesi, its always good to know your status!

Kana-Ka-Nsungu.
 
yaani we acha tu!! wenzako huku tunasubiri tacaids na nacp wapatane tupigane vita ya pamoja
 
Mkuu Kana ka Nsungu umeeleza kisa kinachofanana na kilichonipata mwishoni wa mwezi September mwaka huu nikiwa Arusha
Nilikata shauri kwenda kupima baada ya kuwa naahirisha zaidi ya mara sita kwa visingizio mbalimbali ikiwemo kukosa muda lakini moyoni hofu ndio iliyokua ikinisumbua>
Siku ya siku nikaenda kituoni pale Kaloleni nikakuta chumba cha watu wanaosubiri ushauri nasaha kina watu waliokua katika mjadala wa namna ya maambukizi
Sikuwajali sana maana nilikua najua njia zote za maambukizi kwa hiyo macho yangu nikaelekeza ukutani kulipokua na takwimu za watu waliopima kuanzia January na majibu ya walioathirika kuendana na jinsia zao
Nilijipa moyo kuona wengi ni wanawake nikakumbuka kua kimaumbile wao ni rahisi zaidi kupata maambukizi
Wazo la kuondoka nije siku nyingine likanijia tena na nilipokua najiandaa kuondoka akatokea nesi mmoja akauliza "Nani amekuja kwa ajili ya kupima?" Nikanyosha mkono na akaniambia nimfuate
Yaliyojiri huko chumba cha upimaji na ushauri nasaha sitayasahau kwani picha ya siku zote nilizofanya ngono tangu kupima mara ya mwisho ilinijia lakini sikua na jinsi tena zaidi ya kusubiri majibu
Nilifurahi sana nilipopata majibu kua damu yangu ipo safi na nirudi kwa kupima mara ya pili mwezi January mwakani!
Juzi juzi katika maongezi na mchumba wangu ambae ni mjamzito akaniambia unajua clinic juzi walinipima UKIMWI? nikamuuliza majibu najua yatakua mazuri tu
"umejuaje?" akaniuliza kwa mshangao! Nikamwambia nilipima nikiwa Arusha! Swali lililofatia lilikua gumu zaidi "KWA NINI HUKUNIAMBIA KAMA UMEPIMA?"

Hapo ndio ugumu wa swala la kupima linapokuja! Je wangapi tupo tayari kwenda kupima? Je kesho upo tayari kwenda kupima na mpenzi au mwenzi wako? Je utahairisha mpaka lini?
HIMA HIMA JAMANI TWENDENI TUKAPIME KWANI KUISHI BILA KUJUA HALI YAKO NI SAWA NA KUPIGANA VITA UKIWA UMEFUNGWA KITAMBAA MACHONI
Nawasilisha
 
Matumaini, siku hizi mwanamke akibeba mimba ni lazima apimwe ngoma- sasa hata kama mtu hataki kupima sasa itafikia kipindi utajikuta unapata status yako tu, sema sio kila mwanamke atakuwa honest na kumuambia mumewe kama majibu ni Negative. Mara nyingi ukiona couple wanaenda kupima confidently, chances ni kubwa kuwa mmoja alishaenda kupima kimyakimya na ashajua yupo OK so amamburuza mwezie.
 
Matumaini, siku hizi mwanamke akibeba mimba ni lazima apimwe ngoma- sasa hata kama mtu hataki kupima sasa itafikia kipindi utajikuta unapata status yako tu, sema sio kila mwanamke atakuwa honest na kumuambia mumewe kama majibu ni Negative. Mara nyingi ukiona couple wanaenda kupima confidently, chances ni kubwa kuwa mmoja alishaenda kupima kimyakimya na ashajua yupo OK so amamburuza mwezie.
Kuna tatizo jingine kwa wale walio single. Wakishapima na kujua kuwa hawajaukwaa, badala ya kuchukua tahadhari basi wao wanaongeza spidi hasa kama tabia zao hapo awali zilikuwa ni za ukware kwa kudhani kuwa kama walisalimia kawali, basi hawataupata. Inasikitisha sana
 
Kuna tatizo jingine kwa wale walio single. Wakishapima na kujua kuwa hawajaukwaa, badala ya kuchukua tahadhari basi wao wanaongeza spidi hasa kama tabia zao hapo awali zilikuwa ni za ukware kwa kudhani kuwa kama walisalimia kawali, basi hawataupata. Inasikitisha sana

Kwa kweli huo ni upumbavu, inapoteza maana nzima ya kupima. Mimi UKIMWI kama nitaupata itakuwa kwa njia nyingine za maambukizi lakini sio ngono tena, kuna sehemu kadhaa nilipita na nimesalimika- hii ni ishara ya wazi kuwa Sir God alikuwa anataka anipe second chance. Kila demu saa hizi namtreat kama muathirika tu, ntacheza pekupeku na mama watoto- kama kuniua aniue yeye kihalali!!!
 
Kwa kweli huo ni upumbavu, inapoteza maana nzima ya kupima. Mimi UKIMWI kama nitaupata itakuwa kwa njia nyingine za maambukizi lakini sio ngono tena, kuna sehemu kadhaa nilipita na nimesalimika- hii ni ishara ya wazi kuwa Sir God alikuwa anataka anipe second chance. Kila demu saa hizi namtreat kama muathirika tu, ntacheza pekupeku na mama watoto- kama kuniua aniue yeye kihalali!!!
Kama wote tungekuwa tsimamo kama wako, kweli tungesalimika
 
Kama wote tungekuwa tsimamo kama wako, kweli tungesalimika

I have made mistakes in the past, wakati nasoma sekondari na chuo. Na ni kipindi hiki ndio kilikuwa kinatia hofu sana. Kwa kweli ndugu zangu, kama unaweza jitahidi kuavoid wanawake/ wanaume wakati umeshapiga tungi. Wakati tuko chuo tukidaka boom kuokota CD pale Chrisburger Mwenge au Magomeni kwa Macheni ilikuwa ni fashion, tunashindana tu nani kaokota mzuri, tena huko tunafika tumeshautwika chakari bwinde kuanzia asubuhi DUSO, tukishalewa tungi likishuka kwenye shipa kuu ndo tunaenda kulisaka balaa huko mtaani.

Siku nyingine unaweza ukawa na ndomu zako mfukoni, asubuhi unaamka na demu ukicheki mfukoni bado unazo na bao ushapiga! hata hukumbuki ilikuwaje hadi ukauza timu!

Au umevaa daluga lako lakini kwa kuwa umekunywa mikonyagi na ukachanganya na Safari, dakika 90 zinakaribia bado bilabila unaona aaahhhhh....isiwe tabu unaichomoa unaitupa hukooo! Au kukurukakara, juu chini mara ndomu imepasuka- unaskia flava imebadilika ghafla, kama umekula mtungi- hakyanani 9 out of 10 hutashuka ubadilishe, utakuja kujuta ukishapiga bao! Au mwenzi wako anaanza kukuambia uvue ndomu inamuumiza.........
 
I have made mistakes in the past, wakati nasoma sekondari na chuo. Na ni kipindi hiki ndio kilikuwa kinatia hofu sana. Kwa kweli ndugu zangu, kama unaweza jitahidi kuavoid wanawake/ wanaume wakati umeshapiga tungi. Wakati tuko chuo tukidaka boom kuokota CD pale Chrisburger Mwenge au Magomeni kwa Macheni ilikuwa ni fashion, tunashindana tu nani kaokota mzuri, tena huko tunafika tumeshautwika chakari bwinde kuanzia asubuhi DUSO, tukishalewa tungi likishuka kwenye shipa kuu ndo tunaenda kulisaka balaa huko mtaani.

Siku nyingine unaweza ukawa na ndomu zako mfukoni, asubuhi unaamka na demu ukicheki mfukoni bado unazo na bao ushapiga! hata hukumbuki ilikuwaje hadi ukauza timu!

Au umevaa daluga lako lakini kwa kuwa umekunywa mikonyagi na ukachanganya na Safari, dakika 90 zinakaribia bado bilabila unaona aaahhhhh....isiwe tabu unaichomoa unaitupa hukooo! Au kukurukakara, juu chini mara ndomu imepasuka- unaskia flava imebadilika ghafla, kama umekula mtungi- hakyanani 9 out of 10 hutashuka ubadilishe, utakuja kujuta ukishapiga bao! Au mwenzi wako anaanza kukuambia uvue ndomu inamuumiza.........

CANT BE BETTER PUT...The paining fact is that what you have said above is still going on today..the only difference will be the venues but the deadly procedures are the same...Most young men and women today contract HIV/AIDS in college/university and they will not know their status until just before marriage or in case they attend clinics where its mandatory to have the test. Voluntary counselling and testing (VCT) is thus more important than even the ARVs supply,as the swahili saying goes ''kinga ni bora kuliko tiba",meaning that VCT is in fact the only kinga to HIV/AIDS because if you go to get tested, the reflections you will go through of your past will definitely change the way you will lead your life,at least now you will be a bit more careful. And if found positive, the early knowledge will help you live longer and definitely prevent future infecting others.
 
kazi sio kupima kazi kuchukua majibu,hapo ndio ushujaa unapo tokomea mwituni.Kana ka Nsungu ni suala la kumshukuru Mola kwa hilo,pia wale ambao tumeonekana kuwa na VVU tusisahau aloe vera na kufauata ushauri wa madaktari.
 
thanks kwa kutukumbusha ni kweli akina mama tukishika tu ujauzito lazima kupimwa inasaidia sana kupunguza maambukiza ya kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto
 
Bado hayaepuka mwambie achukue tahadhari so long as bado yupo strong.

Mimi stage ya maambukizi ya UKIMWI kwa ngono zembe nimeshaipita kama nilivyosema hapo mwanzo, nshakua mtu mzima sasa na najua nini napaswa kufanya and how kama nitajikuta kwenye mazingira flani.

Lazima niwaongelee mabaa maid kwenye hii mada manake mchango wao kwenye maambukizi pengine ni mkubwa kuliko ule wa machangudoa. Na labda sababu kubwa leo hii sijaukwaa ni kwakuwa nilikua naokota CDs na sio bar maids. CD wako kwenye business and most of the time watakuwa na condoms zao na watainsist mteja uvae na wanaume wengi tunatumia condom kwao kwa kuwa tunawaogopa, wengi tunaamini ukipiga CD pekupeku ndo umeshajimaliza! Kwa upande wa dada zetu wahudumu wa mabaa- wengi tunawaona wako 'decent' japokuwa wengi wao kila siku wanaondoka na mwanaume tofauti muda wao wa kazi ukiisha. Noma ya hawa ni kwamba mwanaume ili uondoke naye, itabidi umnunulie bia kwa sana, na katika kumsubiri ili baa ifungwe uondoke naye -itabidi nawe uendelee kula maji, by the time mnaondoka kwenda kwenye mchezo wote mko tilalila, hamkumbuki hata kama kuna kitu kinaitwa condom.
 
Hngereni Kana Ka Nsungu pamoja na Matumaini
Nyie ni mabalozi wazuri. Hope tutafuata nyayo zenu Wapwa
 
Back
Top Bottom