Kasimba G
JF-Expert Member
- Jan 19, 2011
- 3,428
- 2,609
Kwa wafuatiliaji wa siasa ulimwenguni watakuwa pamoja na mimi kuwa siasa za majitaka wakati wa uchaguzi haziepukiki, kinadhalia inawezekana lakini kwa utekelezaji ni haiwezekani kabisa. Uchaguzi wa Marekani walisema Obama na Osama wana undugu kiasi cha kuteka hisia za wamerekani wahafidhina wengi na kumponda Obama kuwa hafai. Siasa za majitaka zilisema Obama sio raia wa Marekani zikapelekea Obama kujibu kwa kuonyesha cheti chake cha kuzaliwa n.k,
Urusi hapa juzi siasa za majitaka zilichukua kasi na kusababisha Putin kutokujiamini, bila ukachero Putin asingegombea. Siasa za majitaka huwa zinaaambatana na mambo ya hovyo machache ambayo mgombea aliishawahi fanya au anayofanya pamoja na mambo mengi ya uongo ya uchafuzi.
Naona watu wengi hata humu jamvini wanachangia kuwa siasa za majitaka zisipewe nafasi hapa kwetu Tanzania, je sisi ni kisiwa kilichojitenga na cha waelevu saana kiasi cha kuwa na utamaduni unaoenda tofauti kabisa na utamaduni duniani kwa sasa?
Kwa mtazamo wangu siasa za uchaguzi ni mkusanyiko wa siasa nyingi, majitaka , kuelezea sera, uzushi, ukweli n.k.
Nawasilisha.
Urusi hapa juzi siasa za majitaka zilichukua kasi na kusababisha Putin kutokujiamini, bila ukachero Putin asingegombea. Siasa za majitaka huwa zinaaambatana na mambo ya hovyo machache ambayo mgombea aliishawahi fanya au anayofanya pamoja na mambo mengi ya uongo ya uchafuzi.
Naona watu wengi hata humu jamvini wanachangia kuwa siasa za majitaka zisipewe nafasi hapa kwetu Tanzania, je sisi ni kisiwa kilichojitenga na cha waelevu saana kiasi cha kuwa na utamaduni unaoenda tofauti kabisa na utamaduni duniani kwa sasa?
Kwa mtazamo wangu siasa za uchaguzi ni mkusanyiko wa siasa nyingi, majitaka , kuelezea sera, uzushi, ukweli n.k.
Nawasilisha.