Siasa ya Ujamaa na kujitegemea bado ni Itikadi ya CCM?

mgeni wenu

JF-Expert Member
Jan 2, 2012
3,664
1,730
Napenda saana kujua kuhusu siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ni Sera ya CCM au Serikali(hasa katika kipindi hiki cha vyama vingi)na pia naomba kujua kama siasa hii Inatekelezeka,au imebaki kama Kauli mbiu?..
Nimejaribu kuwauliza wengi(hasa Wazee wastaafu) na wanasema haikuwa Sera ya Chama ila ni Fikra za Mwenyekiti(mwl Nyerere)na C C M yake enzi hizo, na pia Nimepata Jibu la Ajabu kutoka kwa Mzee mmoja hapa Morogoro kuwa Ujamaa ulizaliwa kwa Nyerere ukakulia kwa Mwinyi,ukaugulia kwa Mkapa na Ukafia kwa Kikwete ila Utazikwa na Vyama Vingi..
Sasa napenda Kujua ni sawa Kuuzika au ifanyike mbinu ya kuufufua?..
MY take: ni Bora kuacha mabaya ya Serikali zilizopita na Kuchukuwa yaliyoa Mazuri tu kwa Afya ya Taifa,JE ujamaa na kujitegemea ni Kuuchukuwa au Kuuacha? Nategemea mengi toka kwenu...
Ni mimi Mgeni wenu
 
Ujamaa na Kujitegemea ni contradiction.

Ujamaa maana yake ni kutegemeana. Kujitegemea maana yake ni kutokuwa mjamaa.

Ukiwa mjamaa huwezi kujitegemea. Ukijitegemea huwezi kuwa mjamaa.

"Ujamaa na Kujitegemea" ni contradiction, moja ya sababu ulishindwa.
 
Ni kweli ujamaa uli fail kipindi cha Hayati Baba wa Taifa Mwalimu J.K Nyerere ila kama ni mfuatilia mzuri wa hotuba zake aliwahi kuulizwa swali hilo na Waandishi wa habari na alijibu kwamba " Ujamaa uli fail kwasababu ya baadhi ya washiriki wake kumgeuka, watu ambao alitegemea wangemsapoti walimgeuka, lakini pia Mwalimu alikuwa muwazi alisema kama ujamaa ulikuwa mbaya basi ndani kulikuwa na mazuri pia kwanini yale mazuri yasichukuliwe yakafanyiwa kazi kwa manufaa ya watanzania. Binafsi namuunga mkono kulikuwa na mambo mengi sana mazuri ndani ya mpango huo tatizo ni kwamba watu hawakumuelewa pamoja na tamaa za baadhi ya watu.
 
Napenda saana kujua kuhusu siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ni Sera ya CCM au Serikali(hasa katika kipindi hiki cha vyama vingi)

Ipo kwenye katiba ya nchi hivyo basi ni ya serikali sio ya chama japo inaweza kuhusianishwa na chama kwa sababu katiba ilitungwa wakati wa chama kimoja

na pia naomba kujua kama siasa hii Inatekelezeka,au imebaki kama Kauli mbiu?..

Inatekelezeka kama kutakuwa na uongozi thabiti/imara ila kwa sasa sio hata kauli mbiu kwasababu imebaki kwenye makaratasi tu

Nimejaribu kuwauliza wengi(hasa Wazee wastaafu) na wanasema haikuwa Sera ya Chama ila ni Fikra za Mwenyekiti(mwl Nyerere)na C C M yake enzi hizo, na pia Nimepata Jibu la Ajabu kutoka kwa Mzee mmoja hapa Morogoro kuwa Ujamaa ulizaliwa kwa Nyerere ukakulia kwa Mwinyi,ukaugulia kwa Mkapa na Ukafia kwa Kikwete ila Utazikwa na Vyama Vingi..sina maelezo kuhusu hii kauli ya mzee. Sasa napenda Kujua ni sawa Kuuzika au ifanyike mbinu ya kuufufua?..

sio sawa kinachotakiwa ni kuiboresha mbonaa China wajamaa lakini wanaendelea kwa hiyo commitment ya viongozi katika kutekeleza majukumu inatakiwa

MY take: ni Bora kuacha mabaya ya Serikali zilizopita na Kuchukuwa yaliyoa Mazuri tu kwa Afya ya Taifa,JE ujamaa na kujitegemea ni Kuuchukuwa au Kuuacha? Nategemea mengi toka kwenu...

Nikweli ulilolisema tuige mazuri
 
Nashukuru kwa Majibu ambayo kwa kisi fulani yananifanya nifikirie tena upya
Napenda saana kujua kuhusu siasa ya Ujamaa na Kujitegemea ni Sera ya CCM au Serikali(hasa katika kipindi hiki cha vyama vingi)

Ipo kwenye katiba ya nchi hivyo basi ni ya serikali sio ya chama japo inaweza kuhusianishwa na chama kwa sababu katiba ilitungwa wakati wa chama kimoja

na pia naomba kujua kama siasa hii Inatekelezeka,au imebaki kama Kauli mbiu?..

Inatekelezeka kama kutakuwa na uongozi thabiti/imara ila kwa sasa sio hata kauli mbiu kwasababu imebaki kwenye makaratasi tu

Nimejaribu kuwauliza wengi(hasa Wazee wastaafu) na wanasema haikuwa Sera ya Chama ila ni Fikra za Mwenyekiti(mwl Nyerere)na C C M yake enzi hizo, na pia Nimepata Jibu la Ajabu kutoka kwa Mzee mmoja hapa Morogoro kuwa Ujamaa ulizaliwa kwa Nyerere ukakulia kwa Mwinyi,ukaugulia kwa Mkapa na Ukafia kwa Kikwete ila Utazikwa na Vyama Vingi..sina maelezo kuhusu hii kauli ya mzee. Sasa napenda Kujua ni sawa Kuuzika au ifanyike mbinu ya kuufufua?..

sio sawa kinachotakiwa ni kuiboresha mbonaa China wajamaa lakini wanaendelea kwa hiyo commitment ya viongozi katika kutekeleza majukumu inatakiwa

MY take: ni Bora kuacha mabaya ya Serikali zilizopita na Kuchukuwa yaliyoa Mazuri tu kwa Afya ya Taifa,JE ujamaa na kujitegemea ni Kuuchukuwa au Kuuacha? Nategemea mengi toka kwenu...

Nikweli ulilolisema tuige mazuri
 
Swadakta nafikiri hapo kwenye RED ndipo Mwl N6yerere alikwama, Ujamaa ndio Siasa ya Kweli ya Uchumi inyoweza kuwakomboa Watanzania

Ahsante Kiranga.


Ujamaa na Kujitegemea ni contradiction.

Ujamaa maana yake ni kutegemeana. Kujitegemea maana yake ni kutokuwa mjamaa.

Ukiwa mjamaa huwezi kujitegemea. Ukijitegemea huwezi kuwa mjamaa.

"Ujamaa na Kujitegemea" ni contradiction, moja ya sababu ulishindwa.
 
Ujamaa na Kujitegemea ni contradiction.

Ujamaa maana yake ni kutegemeana. Kujitegemea maana yake ni kutokuwa mjamaa.

Ukiwa mjamaa huwezi kujitegemea. Ukijitegemea huwezi kuwa mjamaa.

"Ujamaa na Kujitegemea" ni contradiction, moja ya sababu ulishindwa.


Mkuu Kiranga nimesoma hii post yako zaidi ya mara kumi nikijaribu ku-prove kama hii kitu uliyoandika ni logical "Truth" ama ni "Fallacy"

Jibu limeniambia ulichoandika ni logical "Truth" kama wazee wetu wangeweza ku-work out hii kitu tangu miaka ile ya 70 tungekuwa mbali!
 
Naomba ni-define Ujamaa upya; kwamba ni: Kujenga uchumi wa nchi kwa kuangalia maslahi ya watu, kwa maana ya maendeleo yanayomlenga mtu. Aina hizi za siasa ni maarufu sana kule Kaskazini mwa Ulaya (Scandia). Kama ni madini basi tuyasimamie kwa manufaa ya wote (nchi) n.k.
Kujitegemea maanake (maana yangu) NCHI iwe na uwezo wa kujipangia mambo yake na kuyafanikisha kizalendo.

Kama hayo yanakubalika, basi tunahitaji kuyarudia kwa kasi mpya??
 
Ujamaa na kujitegemea was out tanzanians choice after independencebut selfishfism policy of nyerere. Ukiangalia sana katika miaka yote ya utawala wa nyerere, utaona alifanyaaa juu chini ili aabudiwe kama mungu na umma wa kitanzania waati anajenga uchumi mbaya sana Tanznaia. alikuwa anaimbiwa kwaya na TOT kuwa yeyey ni mwenye busara, mzuri kifikira, fikira zake zidumu na sahihi, bababmlezi wa umma, kipaji chake kazaliwa nacho, babab mlezi wa taifa na mambo mengi wakati watu mikoani na vijijini wanatembea uchi wa nyama na kero ya kurudia dalasa la saba inawakumba vijana kila kukicha.

Huyu Nyerere alikuwa katili sana, siasa ya ujamaa na kujitegemea haikuwa kwa ajili ya kujenga uchumi bali ni kujenga jina takatifu la nyrere tuu ingawa alikuwa hastahili. jiulize, kwa nini alitunyima uhuru wa kuona TV na kufaidi mafunzo ya tokanayo na TV kwa miaka 27 ya utawala wake wa kujinjijenga kama mungu mtu? kwa nini alikuwa hataki kujenga shule za secondari mpaka ngazi ya kata kama anavyofanya mkapa na kikwete?

Mashabiki wake wanamsfifu kuwa kagomboa africa, huo ni upuuzi, alistahili kumgomboa mtanzania kwanza yule aliyekuwa anarudia dalasa la saba mara kumi ili kutafuta elimu ya secondari na wengine kuja mjini kutafuta kazi. Kwa nini aliwaita watu unemployed, eti, wazururulaji badala ya kuwatafutia kazi? Mbona kikwete kawajengea machina comlex badala ya kuwapeleka keko rumande? unaona jinsi julius alivyokuwa katili ili mradi tuu afanywe mungu mtu na baraza la maaskaofu wakatoliki Tanzania?

Ujamaa na kujitegemea, kwa taarifa yako, ulikuwa ni utumwa ndani ya serikali huru. ona alivyofanya operation vijiji vya ujamaa! , nyerere,halafu aliwarudisha kenya , wale watu waliotaka kumpndua moi mwaka 1982, moi akawauwa wote, kweli hili ni jambo la kumpendeza mungu mpaka aitwe mtakatifu jamani? Mbona hakuwasamehe akina macghee na wenzake , akina member lee, mpaka wakafia Gerezani?

Ujamaa ulivyomfyanya Nyerere mungu mtu, leo hii, ukitaja mabaya ya nyerere hadharani, utasikia mtu anakutukania baba yako kama vile umekashifu dini yake? wewe soma africa now gazete la mwaka 1985, ambalo nyerere alijifanya kulaani Mkataba wa Mkomato accord, kati ya wakati ulke sauth africa vs msumbiji. Ona jinsi mataifa ya africa yalivyomtukana Nyerere ndipo utajua kuwa huyu mtu hakuwa na jina kama tulivyodanganywa na wapambe wake katika africa. halau anagalia. tulipopigana na Iddi Ammin, nchi zote za OAU, hazikutuunga mkono na vita yetu na Uganda, ingawa Iddi Ammini alituchokoza!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Ujamaa na kujitegemea was out tanzanians choice after independencebut selfishfism policy of nyerere. Ukiangalia sana katika miaka yote ya utawala wa nyerere, utaona alifanyaaa juu chini ili aabudiwe kama mungu na umma wa kitanzania waati anajenga uchumi mbaya sana Tanznaia. alikuwa anaimbiwa kwaya na TOT kuwa yeyey ni mwenye busara, mzuri kifikira, fikira zake zidumu na sahihi, bababmlezi wa umma, kipaji chake kazaliwa nacho, babab mlezi wa taifa na mambo mengi wakati watu mikoani na vijijini wanatembea uchi wa nyama na kero ya kurudia dalasa la saba inawakumba vijana kila kukicha.

Huyu Nyerere alikuwa katili sana, siasa ya ujamaa na kujitegemea haikuwa kwa ajili ya kujenga uchumi bali ni kujenga jina takatifu la nyrere tuu ingawa alikuwa hastahili. jiulize, kwa nini alitunyima uhuru wa kuona TV na kufaidi mafunzo ya tokanayo na TV kwa miaka 27 ya utawala wake wa kujinjijenga kama mungu mtu? kwa nini alikuwa hataki kujenga shule za secondari mpaka ngazi ya kata kama anavyofanya mkapa na kikwete?

Mashabiki wake wanamsfifu kuwa kagomboa africa, huo ni upuuzi, alistahili kumgomboa mtanzania kwanza yule aliyekuwa anarudia dalasa la saba mara kumi ili kutafuta elimu ya secondari na wengine kuja mjini kutafuta kazi. Kwa nini aliwaita watu unemployed, eti, wazururulaji badala ya kuwatafutia kazi? Mbona kikwete kawajengea machina comlex badala ya kuwapeleka keko rumande? unaona jinsi julius alivyokuwa katili ili mradi tuu afanywe mungu mtu na baraza la maaskaofu wakatoliki Tanzania?

Ujamaa na kujitegemea, kwa taarifa yako, ulikuwa ni utumwa ndani ya serikali huru. ona alivyofanya operation vijiji vya ujamaa! , nyerere,halafu aliwarudisha kenya , wale watu waliotaka kumpndua moi mwaka 1982, moi akawauwa wote, kweli hili ni jambo la kumpendeza mungu mpaka aitwe mtakatifu jamani? Mbona hakuwasamehe akina macghee na wenzake , akina member lee, mpaka wakafia Gerezani?

Ujamaa ulivyomfyanya Nyerere mungu mtu, leo hii, ukitaja mabaya ya nyerere hadharani, utasikia mtu anakutukania baba yako kama vile umekashifu dini yake? wewe soma africa now gazete la mwaka 1985, ambalo nyerere alijifanya kulaani Mkataba wa Mkomato accord, kati ya wakati ulke sauth africa vs msumbiji. Ona jinsi mataifa ya africa yalivyomtukana Nyerere ndipo utajua kuwa huyu mtu hakuwa na jina kama tulivyodanganywa na wapambe wake katika africa. halau anagalia. tulipopigana na Iddi Ammin, nchi zote za OAU, hazikutuunga mkono na vita yetu na Uganda, ingawa Iddi Ammini alituchokoza!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

You too, are a great thinker!
 
Ujamaa na Kujitegemea ni contradiction.

Ujamaa maana yake ni kutegemeana. Kujitegemea maana yake ni kutokuwa mjamaa.

Ukiwa mjamaa huwezi kujitegemea. Ukijitegemea huwezi kuwa mjamaa.

"Ujamaa na Kujitegemea" ni contradiction, moja ya sababu ulishindwa.

Haya sasa ni makusudi ya kupotosha!
 
Who knows labda this time tunaweza kukubaliana, nikumbushe objection yako ilikuwa nini?

Kwamba the kujitegemea half of it was about building a nation that is not foreign aid dependent (as it is now) and ujamaa being about living together peacefully despite the differences in our religious convictions, ethnic backgrounds, etc.
 
Hii ni Thread nzuri sana hasa kwa wakati huu. Wakati tunapata uhuru 50 years ego ilibidi tuanzishe utamaduni wetu ambao haukufanana na ule wa kikoloni. Kwa hiyo Mw. Nyerere alianzisha mfumo wa ujamaa 1968. Wakati huo walikuwa wasomi wachche sana Tanganyika. Ili kujenga taifa linalo jitegemea Ujamaa ulikuwa ni mwelekeo mzuri kwa wakati ule. Ingawaje nchi ilikuwa maskini hasa baada ya kushuka bei za katani na kahawa ambayo ndiyo mazao mawili ya biashara tuliorithi baada ya uhuru lakini Elimu ilikuwa bure na hata tiba bure. Palikuwa hamna mafisadi. Najuwa wapo msiopenda ujamaa kwa hiyo I am sorry but the truth has to come out.

Ajili ya muelekeo huu wa kiujamaa, nchi yetu iliwekewa vikwazo vingi vya uchumi na ndiyo vilivyo rudisha nyuma maedeleo. Hivi leo wasomi ni wengi na rasilimali nyingi tunazo lakini hali ya uchumi na maedeleo ni mbaya zaidi kuliko wakati wa ujamaa. Na hii ni kwa sababu wananchi wanahangaika na ukata na hawapati muda wa kutafakari maendeleo ya nchi yao kwa hiyo wanaridhika na repoti wanazopewa na serkali yao. Uki tafakari demogrphicaly uchumi wa nchi na population utaona how much tumerudi nyuma. We will not be able to progress in this condition of apathy.
 
Back
Top Bottom