Inasikitisha: Ni umbali wa km kama 2 tu, toka ukumbi wa BUNGE la JMT, ambapo wabunge wa CCM, CDM et al. na mawaziri hukutana, kuna Hospitali ya mkoa wa Dodoma ambapo wanawake wazazi hulala chini, ama wawili katika kitanda kimoja. Lakini sijawahi sikia mwanasiasa yeyote yule kutoka katika vyama tajwa akikataa mpango wa kukopeshwa zile mil 100 kwa ajili ya kununua gari. Miongoni mwa waliopokea fedha hizi ni wale ambao walikuwepo katika Bunge lililotangulia; kimsingi hawa bado wana magari yale ya awali. Pia wanasiasa hawa kila kukicha hujipitishia nyongeza ya malipo ya kila mwezi na posho ya vikao.Ingelikuwa vema kama sehemu ya fedha hizi zikapelekwa katika Hospitali hii, kuokoa maisha ya akina mama na watoto wao katika Hospitali hii.