Shule za Tanzania zina mashariti ya kishamba, hili tukio lilitokeaga Moshi

BLACK MOVEMENT

JF-Expert Member
Mar 11, 2020
2,712
6,515
Kule Moshi kuna shule moja ni ya kanisa sitaitaja jina ni zile shule zina mashariti lukuki ikiwemo kwamba kumuona mtoto ni hadi Visiting day.

Sasa kuna Jamaa alikuwa na mtoto anasoma kwenye hio shule jamaa yeye anaishi Dar ila ni mtu wa safari nje ya nchi sana kiasi kwamba anapishanaga na mtoto wake anaye soma Moshi.

Mtoto akiwa likizo Baba hayupo na Baba akirudi mtoto walisha fungua, hivyo ilikuwa ni anaweza kata mwaka hajaoanana na mtoto wake kwa sababu ya safari na kupishana.

Siku moja akawa na safari Arusha, sasa akaona hii pia ni nafasi pekee ya kumuona mtoto wake make hawajaonana mwaka.

Alivyofika shuleni alikutana na kizingiti cha mlinzi akimwambia huwezi onana na mtoto hadi siku ya Visiting Day, jamaa kakomaa kwamba ni lazima aonene na mtoto wake kwa sababu hajaonana naye mwaka mzima na hakuna namna anaweza ondoka bila kumuona.

Uongozi ukashikilia msimamo kwamba jamaa hawezi kamwe kumuona mtoto na huo ndio msimamo wa shule na hauwezi badilishwa kamwe.

Jamaa kaona isiwe tabu akauliza mnanidai? Yaani kuna ada yoyote nadaiwa? Uongozi ukasema hapana hudaiwi.

Okay nipeni mtoto wangu na kila kilicho chake niondoke naye, Uongozi ukadhania ni utani kumbe ndio jamaa anamanisha, sasa msimo ulibadilika kutoka kumuona na sasa ni anaondoka naye mazima, ilibidi kweli mtoto atolewe na jamaa akasepa naye na kwenda kumtafutia shule nyingine isio kuwa na ujinga kama huo.

Jamaa msimamo wake ilikuwa yule ni mtotot wake hajaonana naye mwaka na hakuna namna amaweza ondoka Moshi bila kumuona.

Ila ukiangalia jamaa alikuwa sahihi yeye ndie mwenye mtoto, ndie anaye lipa ada haiwezekani hujaonana na mtoto. Wako miaka bado ufike getini uambiwe hairuhusiwi kumuona.
 
Hiyo imetokea pia pale St. Gasper Dom wana huu ujinga, mzazi wakati wa likizo alikuwa anamtibu mtoto hospitalini na tatizo hata physical linaonekana, bad enough alikuwa na document ya hospital,

Mzaz alipompeleka mtoto, Shule ikakataa mtoto kisa kachelewa, tena hata masomo walikuwa hawajaanza, mzaz analipa ada kwa term mbili walimgomea amechelewesha mtoto, Mzaz akaona isiwe kesi akawaambia walete kila kitu cha mwanae akasepa navyo, akamuhamisha

Ifike sehem serikal ipige marufuk hiz mambo kwa private school kufanya hii kitu wanajiona kweli, hii haikubaliki
 
Peleka mtoto shule ya serikali hakuna huo ujinga.

Kwa Tanzania ya sasa kusomesha mtoto shule za private ni kupoteza hela kwa sababu wakimaliza form six ama four, hakuna kinachowatofautisha kati ya kusoma private ya milioni 8 na kusoma shule ya bure, wote ni zero brain, no life skills, no analytical skills or reasoning.

Wakifeli pia the same, aliepata zero private na aliepata zero serikalini wote wako sawa. Hakuna mwenye kumzidi mwenzake kwa chochote.

Now days Tanzania shule sio investment tena, ni mufilisi.
 
Unapompeleka mtoto shule husika siunapewa masharti ya shule husika?

Sasa kama uliyakubali ila unataka yavunjwe kibabe utapata tabu Tu.

Anaeteseka ni mtoto atahamishwa shule ngapi? Na shule zipi zitatakiwa kufuata masharti ya mzazi wa mtoto sio ya shule.

Anaepata hasara ni mzazi hizo shule mara nyingi zinawanafunzi wengi na kila muhula bado wanawapunguza wanafunzi kwa sababu mbalimbali, kuondoka na mwaanao huwakomoi kabisa ila watakua wanatolea mfano kwamba ukiona masharti ni magumu ondoka na mwano kama flani.
 
WaTz bana, wao wanataka kila kitu kiende kwa busara na sio sheria za taratibu zilizowekwa,.
Tatizo wangemruhusu huyo mzazi na kesho wakaja wazazi wengine 10 nao wana sababu hio hio, na kesho kutwa nayo, utakuja kuona hata ile sheria inavunjwa, shule inakuwa holela tu
 
Kule Moshi kuna shule moja ni ya kanisa sitaitaja jina,ni zile shule zina mashariti lukuki ikiwemo kwamba kumuona mtoto ni hadi Visting day.

Sasa kuna Jamaa alikuwa na mtoto anasoma kwenye hio shule jamaa yeye anaishi Dar ila ni mtu wa safari nje ya nchi sana kiasi kwamba anapishanaga na mtoto wake anaye soma Moshi.

Mtoto akiwa likizo Baba hayupo na Baba akirudi mtoto walisha fungua, hivyo ilikuwa ni anaweza kata mwaka hajaoanana na mtoto wake kwa sababu ya safari na kupishana.

Siku moja akawa na safari Arusha, sasa akaona hii pia ni nafasi pekee ya kumuona mtoto wake make hawajaonana mwaka.

Alivyo fika shuleni alikutana na kizingiti cha mlinzi akimwambia huwezi onana na mtoto hadi siku ya Visiting Day, jamaa kakomaa kwamba ni lazima aonene na mtoto wake kwa sababu hajaonana naye mwaka mzima na hakuna namna anaweza ondoka bila kumuona.

Uongozi ukashikilia msimamo kwamba jamaa hawezi kamwe kumuona mtoto na huo ndio msimamo wa shule na hauwezi badilishwa kamwe.

Jamaa kaona isiwe tabu akauliza mnanidai? Yaani kuna ada yoyote nadaiwa? Uongozi ukasema hapana hudaiwi.

Okay nipeni mtoto wangu na kila kilicho chake niondoke naye, Uongozi ukadhania ni utani kumbe ndio jamaa anamanisha, sasa msimo ulibadilika kutoka kumuona na sasa ni anaondoka naye mazima, ilibidi kweli mtoto atolewe na jamaa akasepa naye na kwenda kumtafutia shule nyingine isio kuwa na ujinga kama huo.

Jamaa msimamo wake ilikuwa yule ni mtotot wake hajaonana naye mwaka na hakuna namna amaweza ondoka Mosji bila kumuona.

Ila ukiangalia jamaa alikuwa sahihi yeye ndie mwenye mtoto, ndie anaye lipa ada haiwezekani hujaonana na mtoto.wako miaka bado ufike getini uambiwe hairuhusiwi kumuona.
Huyo jamaa ni mjinga kwani aliambiwa ampeleke mtoto hapo. Kila mahali kuna utaratibu na anaujua alishaukubalia hawez atembee na mwanae
 
Back
Top Bottom