abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
Waziri wa Maji, Makaazi, Nishati na Ardhi, Ali Juma Shamhuna yupo katika shindikizo kubwa la wajumbe wa baraza la wawakilishi wakimtaka aachie ngazi kutokana na kuchukua uamuzi wake binafsi juu ya suala la ombi la ongezo la bahari kuu kuwasilishwa huko Umoja wa Mataifa (UN) Jana katika baraza la wawakilishi la Visiwani Zanzibar kulikuweko majadiliano makali kuhusu hoja iliowasilishwa na mwakilishi wa eneo la Mji Mkonge wa Zanzibar, Ismail Jussa Ladhu, Hii imetokana na ombi la serikali ya Muungano wa Tanzania kwa Umoja wa Mataifa kuomba nyongeza ya mpaka katika Bahari ya Hindi ni kuipokonya Zanzibar haki yake. Yeye alitaka kuwepo mazungumzo ya kuamua nani anamiliki eneo hilo kati ya Tanzania na Zanzibar. Othman Miraji alimpigia simu Salim Said Salim, mwandishi wa habari mkongwe Visiwani humo, kutaka kujuwa nini kilichozunguka katika hoja hiyo ya Mwakilishi Jussa hata Wazanzibari kuwa na hamu na mjadala huo.