Shida ya maji Kimara - Mbezi ya kutengeneza?

Feb 15, 2009
99
2
Kuna stori naifuatilia kuhusu kasheshe ya maji maeneo ya Kimara - Mbezi, kama mnavyofahamu kwa wale wakazi wa maeneo ya Kimara - Suka - Temboni- mpaka Mbezi tatizo la maji limekuwa kama halitatuliki yaani uwezi amini kuwa pamoja na bomba kubwa kupita maeneo hayo lakini maji ya bomba kwa wakazi wa maeneo hayo ni ndoto, lakini yasemekana tatizo hili ni la kutengeneza.

Kuna wanaonufaika na tatizo hili, zaidi wenye magari ya kuuza maji ambayo yamekuwa yakiongezeka kila uchao, watu hawa wananunua lita 20 ama ndoo moja kwa shilingi 20/= mpaka hamsini na kuuza sh 300/= mpaka 500/= inasemekana baadhi ya wakubwa pale DAWASCO na ata wizarani ndo wamiliki wa magari hayo yan ayoongezeka kila uchao.

ningali nafatilia nikipata dataz nitazimwaga hapa kwamba nnani wahusika wakuu.

CIAO.
 
Back
Top Bottom