Sheria inakataza Upinzani kufanya Mabadiliko katika Baraza la Mawaziri vivuli?

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,434
7,055
Nimekaa nikatafakari. Nikaona ni vyema nililete hili suala hapa ili sote tupate kufahamishana.

Miezi michache baada ya Serikali ya Awamu ya 5 kuingia madaraka na Rais John Magufuli kutangaza Baraza la Mawaziri, Februari 2016 Kiongozi wa Upinzani Freeman Mbowe naye alitangaza Baraza lake la Mawaziri vivuli bungeni > Mbowe atangaza Baraza kivuli la Mawaziri, Mbatia ndani. Zitto, Kubenea nje - JamiiForums

Umepita muda mrefu sasa na mambo mengi yametokea kwenye siasa za nchi yetu, hasa kwenye siasa za vyama. Na kwa bahati nzuri au mbaya, imeonekana kwamba viongozi na wanachi kwa ujumla, sote tumekuwa tukienda na upepo. Yaani, tunaenda na matukio kwa kadri yanavyotokea kiasi cha kusahau kuangalia mambo mengine. Hili la Baraza Kivuli likiwemo.

Mathalani, baadhi ya Wizara zilivunjwa na kuunganishwa. Nyingine zilitenganishwa na kadhalika. Vilevile, Wabunge wamehama mostly kutoka Upinzani kwenda Chama Tawala. Hivyo, naamini mambo haya yote ni lazima yatakuwa yameathiri lile Baraza Kivuli ambalo kimsingi ni relfection ya Baraza halisi linaloundwa na Rais wa JMT.

Ukipitia Baraza la Mawaziri vivuli, utagundua mapungufu ya wizara kubaki vile vile (mfano Wizara ya Nishati na Madini, ), Bado Wabunge waliohama vyama wanatajwa kuwa ni viongozi wa wizarani (Mfano Mwita Waitara, Abdallah Mtolea) n.k.

Je, kwanini Upinzani bado hawajafanya maboresho kwenye Baraza la Mawaziri vivuli ili kuendana na athari ya mabadiliko ya kimfumo yaliyofanywa na Serikali katika wizara mbalimbali? Ni sheria/Katiba inawabana au wamesahau!?
 
Baraza la Mawaziri kivuli limejaa vichaa wengi, hakuna mtu anayelichukulia serious, kila vichaa wamo humo hata Bon Mashavu na yeye 2020-2025 anaweza kuwa Waziri kivuli.
 
Mmmm! Anthony Komu naye kaenda lini huko wanakounga mkono juhudi za jiwe? Anyway point yako ni ya msingi, wataalamu watatujuza!
 
Watakuwa wanasubiri wale mawazi ambao wana ndoto ya uwazi kutumbuliwa kwanza. Usumbufu kubadili baraza kwa sababu Jiwe kabadili au walafi wamehama
 
Naona unatumia data za kwenye vikao vyenu zilizowaonyesha kua komu naye atakua mwenzenu
 
Mmmm! Anthony Komu naye kaenda lini huko wanakounga mkono juhudi za jiwe? Anyway point yako ni ya msingi, wataalamu watatujuza!
Nadhali automatically siyo waziri kivuli tena (kama tu awali alikuwa) baada ya CC ya CDM kumwondolea vyeo vyake vyote (isipokuwa uanachama/ubunge) baada ya kudaiwa kupanga mipango miovu dhidi ya baadhi ya viongozi wa CDM. Kwa hiyo nafasi yake itakuwa wazi. Hata hivyo Yeye ameamua kuunga na mkono akiwa ndani ya CDM.
 
Baraza la Mawaziri kivuli limejaa vichaa wengi, hakuna mtu anayelichukulia serious, kila vichaa wamo humo hata Bon Mashavu na yeye 2020-2025 anaweza kuwa Waziri kivuli.

Kama hao ni wakichaa basi wewe ni taahira kabisa, halafu kumbuka vichaa hawako upinzani tu hata huko kwenu wapo, wengine mpaka wanafikia kwenda kupima kwa rula samaki waliokwisha andaliwa mezani kuliwa.
 
Baraza la Mawaziri kivuli limejaa vichaa wengi, hakuna mtu anayelichukulia serious, kila vichaa wamo humo hata Bon Mashavu na yeye 2020-2025 anaweza kuwa Waziri kivuli.
Wangekuwa hivyo si wangeshakuwa Mawaziri kamili.
Nakumbuka jiwe aliwahi kutangaza sifa za kuwa kwenye Baraza lake la Mawaziri ni sharti uwe KICHAA Kama yeye
 
Nimemuondoa Komu kwenye list. Nakiri udhaifu, aliingia humo kimakosa. Naomba radhi sana.
Mengine yaliyobaki tuendelee nayo.
 
Back
Top Bottom