Sheria Inachukua Mkondo Gani Kama Mtu Anatangaza Anataka Kujiua au Atajiua?

Ndallo

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
7,619
4,292
Mimi sio mwanasheria na pia naomba kujua sheria inachukua mkondo gani endapo mtu anawaita watu na mbele ya makamera jamii au ulimwengu wote wakamsikia akidai atajiua? hii ni mujibu wa sheria zetu hapa kwetu Tanzania! mfano mojawapo ni huu hapo jana TBC1 kutuonyesha live bila chenga bwana Abdalah Zombe kuuambia uma wa watanzania kua chama cha chadema kikichukua madaraka basi atajitoa kafara kwakujinyonga Je kama basi indendapo chama hiki cha demokrasia na maendeleo endapo kitapata ridhaa ya kuongoza nchi huyu bwana atachukuliwa hatua gani kwa mujibu wa sheria? Naomba kuwasilisha
 
Suicide ni jinai, kutangaza ni attempt to suicide ambayo uhukumiwa maisha. Ni jinai!
 
Mimi sio mwanasheria na pia naomba kujua sheria inachukua mkondo gani endapo mtu anawaita watu na mbele ya makamera jamii au ulimwengu wote wakamsikia akidai atajiua? hii ni mujibu wa sheria zetu hapa kwetu Tanzania! mfano mojawapo ni huu hapo jana TBC1 kutuonyesha live bila chenga bwana Abdalah Zombe kuuambia uma wa watanzania kua chama cha chadema kikichukua madaraka basi atajitoa kafara kwakujinyonga Je kama basi indendapo chama hiki cha demokrasia na maendeleo endapo kitapata ridhaa ya kuongoza nchi huyu bwana atachukuliwa hatua gani kwa mujibu wa sheria? Naomba kuwasilisha

Kwa sasa hivi kujiua au kutishia kujiua ni kosa la jinai. Lakini endapo Chadema kitapata ridhaa ya kuongoza nchi, kitabadilisha sheria chap chap ili huyu bwana ajinyonge bila kuvunja sheria za nchi. Baada ya huyu jamaa kujingonga, Chadema itarudisha sheria kama ilivyokuwa. LOL.
 
Suicide ni jinai, kutangaza ni attempt to suicide ambayo uhukumiwa maisha. Ni jinai!

Suicide itakuaje jinai? Sioni mantiki yoyote hapo. Kama suicide ni jinai adhabu yake ni nini sasa?

Na hata attempted suicide nayo haitakiwi kupewa adhabu ya maisha na haitakiwi kumuadhibu aliyetaka kujiua. Badala yake kinachotakiwa kufanyika ni kumsaidia huyo mtu kwa sababu ni wazi kabisa kuwa ana matatizo yanayohitaji msaada.
 
kujiua ni kosa la jinai... kwasababu imeainishwa huna ruhusa ya kutoa uhai wa binadamu yeyote ... ikiwamo na uhai wako mwenyewe.. kwa hiyo ukijiua unakuwa umeidhulumu nafsi ya kiumbe hai.. ndio maaana wanaojaribu kujiua wakipona wanashtakiwa....
 
Back
Top Bottom