Shamsa(i) Vuai na Makamba: Upeo, fikra na akili za Viongozi wetu!

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
"kabla ya migogoro haijatatuliwa ni lazima wahusika wakuu waamini kuwa kuna mgogo"

"itiini mamlaka iliyowazidi nguvu, hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu..."

Baada ya wananchi zaidi ya wanne [SIO WATATU] kufariki, zaidi ya 20 kujeruhiwa vibaya, nyumba kuwaka moto kutokana na mabomu ya polisi (wakisingizia zimechomwa!), mtoto wa miaka kumi na nne kupigwa risasi ya kiuno, mama mkwe wa RPC Hemed (alikuwa RCO Morogoro) kupigwa bomu (je na yeye alikuwa anaenda kuvamia kituo cha polisi?) n.k ndio 'wakuu' wanaamini kuna tatizo Arusha!! Wote tunaamini Mungu yupo, na SAUTI ya umma itashinda!

Katika hili jeshi la polisi limekosea SANA! Wao ndio wamevuruga amani ya Arusha na nchi nzima!
 
Huwa simwelewi makamba hata kidogo! Sijui ukatibu wake ni kwa maslahi ya nani! Siamini kwamba anawakilisha sisiem, tanzania itaendelea kama tukiwaondoa viongozi wa aina hii! Naamini kauli zake zimechochea damu kumwagika ar!
Tuwe makin!
"kabla ya migogoro haijatatuliwa ni lazima wahusika wakuu waamini kuwa kuna mgogo"

"itiini mamlaka iliyowazidi nguvu, hakuna mamlaka isiyotoka kwa mungu..."

baada ya wananchi zaidi ya wanne [sio watatu] kufariki, zaidi ya 20 kujeruhiwa vibaya, nyumba kuwaka moto kutokana na mabomu ya polisi (wakisingizia zimechomwa!), mtoto wa miaka kumi na nne kupigwa risasi ya kiuno, mama mkwe wa rpc hemed (alikuwa rco morogoro) kupigwa bomu (je na yeye alikuwa anaenda kuvamia kituo cha polisi?) n.k ndio 'wakuu' wanaamini kuna tatizo arusha!! Wote tunaamini mungu yupo, na sauti ya umma itashinda!

Katika hili jeshi la polisi limekosea sana! Wao ndio wamevuruga amani ya arusha na nchi nzima!
 
big up Kaka.mi nilitaka kukuuliza je sheria za nchi yetu zinasemaje pale kunapotokea mauaji ya mtu,ili kesi ifike mahakamani ni lazima kuwe na mtu anayeshataki au mwendesha mashataka kwa kuzingatia kuwa hili ni swala nyeti la upotevu wa maisha ya bianadamu anatakiwa kuanzisha upelelezi wake bila kusubiri kuwe na mtu alianzisha shtaka ama la...!maana haiwezekani kila siku tunasikia mauaji ya raia kutokana na nguvu za polisi lkn zaidi ya kesi ya Zombe(ambayo nayo kama ilikuwa kiini macho vile?,hautusikii kesi nyingine yeyote inayohusisha polisi katika mauaji ya raia....!Mi nadhani kwa namna fulani inabidi kitengo cha muendesha mashitaka,kisingehusishwa namna fulani moja kwa moja na polisi,mwendesha mashitaka mkuu asiwe chini ya IGP(nikosoe kama nakosea,kwani nadhani kwa sasa yupo chini ya IGP),ili kiweze kufanya kazi inayotakiwa pale inapotakiwa.nadhani mambo kama haya inapotokea kuwa kuna mtu kapoteza maisha katika mazingira ya namna hii,basi mwendesha mashitaka aweze kuchukua hatua nara moja.
Other than that,we're proud kaka,unatuwakilisha vyema "wanaWU-MIREMBE".....
 
Back
Top Bottom