Mzee wa Usafi
JF-Expert Member
- Apr 16, 2008
- 644
- 292
Uko sahihi kabisa Mtanzania mwenzangu. Kwenye suala la upelelezi Jeshi letu la Polisi bado lipo nyuma kabisa. Nimekuwa mfuatiliaji na muangaliaji wa kipindi cha TV Crime Investigation kwa muda mrefu. Ukiona vile wenzetu wanavyo tumia ujuzi na maarifa kupata ushahidi kabla ya kufanya ukamataji utasema kweli hawa ni wapelelezi. Sisi tukio linafanyika usiku ikifika asubuhi tayari wanafanya arrest , unapatwa na wasiwasi hivi washiriki wa matukio ni wajinga kiasi hicho?Inawezekana wanahusika, kila mifumo yetu ya upelelezi bado, yaani uwezo wa kumpiga mtu maswali ajikanyage mpaka aonekane kweli kahusika bado ni shida.
Hata kama mahakama haikubali lakini ni ukweli usio pingika vituoni watuhumiwa hiteswa kukiri kosa wanasahau kuwa wakienda mahakama na mtuhumiwa aka kana maelezo yaliyo andikwa na Polisi basi Jamhuri huwa haina njia mbadala ya kuithibitishia mahakama kuwa flani ndo musika wa tukio hilo.
Kwa wataalam wa sheria wanakuambia hakuna kesi rahisi Dunia kama kesi ya mauaji kwani shahidi namba moja ni marehemu, mashahidi wangine huwa ni wakuunga unga tu....kwani ni lazima mahakama ijiridhishe X ndo aliyetoa uhai wa Y bila mashaka yoyote.....