Sh4.2bn earthquake relief cash ‘lying idle’

Mkuu Nguruvi3 hawa watu ni wahuni sana sijui kwanini wanataka kulidanganya Taifa mchana kweupe kuhusu kiasi halisi kilichokusanywa na uongo huo wanaousema ni kwa faida ya nani. UK imetoa 6.3 billion na kwingine inaonekana ni 6.7 billion (conversion rate inahusu hapa) India wametoa shilingi 545 million, Uganda shilingi 437 million, Majaliwa alikusanya bilioni 1.4 hii ni baadhi tu ya michango ambayo ni zaidi ya bilioni 8 sasa iweje leo tuambiwe zilikusanywa 5 billion tu!?

Na kama unavyosema hawa wana Kagera waliopata maafa haya nao ni walipa kodi nchini miaka nenda miaka rudi kwanini Serikali ishindwe kutoka bilioni 20 au hata zaidi kuwasaidia kwenye haya maafa!? Kwanini Serikali itegemee tu pesa za michango toka ndani na nje ya nchi? Nina wasiwasi hata hizo milioni 800 zilizotumika hazikuwafikia wahanga wa tetemeko kama ziliwafikia basi ni sehemu ndogo sana zilizowafikia.

Iweje wiki ya saba sasa Serikali inashindwa kusambaza pesa hizo kwa wahanga na huku wakiendelea kuishi nje, hawana maji, hawana chakula!? tatizo ni nini hasa Serikali inaendelea kuzikumbatia pesa hizi?

Hili la tetemeko linatatiza sana

Kwanza, tetemeko limeathiri watu na mali zao. Kwa hesabu zao zilihitajika Bilioni kadhaa kurudisha hali
Kwa minajili ya mjadala tuseme ni Bilioni 20. Hivi kweli serikali inayokusanya 1.2T imeshindwa kutoa bilioni 20 hadi tuite mabalozi kwa misaada?

Mh Makamba alitueleza, katika kero za muungano JMT ilitoa bilioni 29 kwa budget support ya Zanzibar
Serikali hiyo hiyo imeshindwa kutenga kiasi cha bilioni 20 kwa Walipa kodi wa Kagera!

Pili, tulisikia Kenya na Uganda wamechangia yakiwemo mataifa mengine na watu binafsi
Leo namba zinapishana, mara bilioni hizi mara zile
Ni wakati sasa kila kitu kiwekwe wazi wananchi wajue nini kilichangwa na kimeelekezwa wapi

Tatu, leo waziri mkuu bado anatembelea magofu ya shule. Ina maana hakuna kilichofanyika hadi wakati huu
Hivi hatuna wataalamu wanaoweza kuchora, na contractors wanaoweza kujenga shle katika muda mfupi?

Ile dhana ya hapa kazi ipo wapi?
 
au jaman hii habar sio ya kweli!?!
c.c lizabon,wakudadavua na wapiga mapambio wote wa lumumba
 
Maskini media za TZ
Maskini wapinzani wa TZ
Magufuli hagusiki wala haulizwi
Uozo alio fanya ktk kuwajibika na athari za Bukoba zinaiondolea haki ya serikali yake kutawala
Utawala wa hovyo hovyo unao ogopwa na upinzani wa hovyo hovyo
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Thursday, November 3, 2016
Distribute quake relief now, says MP


pic+distribute+quake+-mp.jpg

Bukoba Urban Member of Parliament Wilfred Lwakatare has asked the government to start disbursing relief supplies donated to his people to mitigate the effects of the 5.7 magnitude earthquake.

In Summary
  • According to Mr Lwakatare, Bukoba residents wonder, where all the supplies have gone, while they still suffer for nearly two months now. “The people have lost faith in the government, the money was donated to the victims of the earthquake, but no single sent has been given to any of them as we are speaking.”

By Athuman Mtulya @mtulya amtulya@tz.nationmedia.com

Dodoma. Bukoba Urban Member of Parliament Wilfred Lwakatare has asked the government to start disbursing relief supplies donated to his people to mitigate the effects of the 5.7 magnitude earthquake, which hit Bukoba Town on September 10.

According to Mr Lwakatare, Bukoba residents wonder, where all the supplies have gone, while they still suffer for nearly two months now. “The people have lost faith in the government, the money was donated to the victims of the earthquake, but no single sent has been given to any of them as we are speaking.”

Mr Lwakatare said that on Tuesday evening, while debating a budget framework and national development plan for the 2017/18 fiscal year. He said if the government was not ready to release the money, then they should at least subsidise prices of construction materials so that the affected families could start rebuilding their houses.

“The effects of the September earthquake are so deep, and have affected the economy of our town. We need urgent intervention from the government. The more we delay, the more we make our people groan in anguish,” he said.

Nkenge MP, Dr Diodorus Kamala (CCM), whose constituency was also affected, said there were conflicting directives from the government with some leaders encouraging people to mobilise their own resources and rebuild their houses, while others were telling them to wait for a geological survey to establish the safety of the area.

“My people ask, which way should they go? It is really confusing! They haven’t received any relief aid from the government and they are not receiving proper information,” said Dr Kamala.

Last week, the chairman of the Parliamentary Committee on Constitutional and Legal Affairs, Mr Mohamed Mchengerwa, told reporters that only Sh800 million had so far been spent out of Sh5 billion raised to support the government’s efforts to rebuild infrastructure in the affected areas.

Mr Mchengerwa said his committee had received government briefing on the matter. He also revealed that the official death toll had increased to 23 from 17 after six people, who were admitted to various hospitals died. They were among 440 people, who sustained injuries.
 
Mkuu Nguruvi3 hawa watu ni wahuni sana sijui kwanini wanataka kulidanganya Taifa mchana kweupe kuhusu kiasi halisi kilichokusanywa na uongo huo wanaousema ni kwa faida ya nani. UK imetoa 6.3 billion na kwingine inaonekana ni 6.7 billion (conversion rate inahusu hapa) India wametoa shilingi 545 million, Uganda shilingi 437 million, Majaliwa alikusanya bilioni 1.4 hii ni baadhi tu ya michango ambayo ni zaidi ya bilioni 8 sasa iweje leo tuambiwe zilikusanywa 5 billion tu!?

Na kama unavyosema hawa wana Kagera waliopata maafa haya nao ni walipa kodi nchini miaka nenda miaka rudi kwanini Serikali ishindwe kutoka bilioni 20 au hata zaidi kuwasaidia kwenye haya maafa!? Kwanini Serikali itegemee tu pesa za michango toka ndani na nje ya nchi? Nina wasiwasi hata hizo milioni 800 zilizotumika hazikuwafikia wahanga wa tetemeko kama ziliwafikia basi ni sehemu ndogo sana zilizowafikia.

Iweje wiki ya saba sasa Serikali inashindwa kusambaza pesa hizo kwa wahanga na huku wakiendelea kuishi nje, hawana maji, hawana chakula!? tatizo ni nini hasa Serikali inaendelea kuzikumbatia pesa hizi?


HER ZA KUTOKA UK NI KWA AJILI YA KUJENGA SHULE ZAO ZA IHUNGO KAMA HISTORIA YAO.ZINAMAELEKEZO MAALUMU
 
Nakumbuka zile bilioni 4 zilizobaki kwenye bunge maalum la katiba jinsi mzee 6 alivyozitafutia namna ya kuzitumia. Chama chakavu ni kile kile.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
mafisadi warudishe hela zetu..
tuliwachangia ndugu zetu na si vinginevyo..
ivi mbaya ni nani..
kati ya yule aliyetaka kuchangisha ili ziwafikie wahanga kwa haraka akatumbuliwa?
na huyu aliyechangisha akatokomea nazo kusikojuilikana ?
 
Huu ni uongo wa hali ya juu. Uingereza pekee yake imetoa shilingi 6.7 billion kusaidia wahanga wa tetemeko la ardhi iweje Serikali iseme zimekusanywa bilioni 5 tu!? List ya wachangiaji wote na kiasi walichochanga iwekwe hadharani mara moja ili kama kuna wizi umefanywa katika pesa hizi basi hao wezi wanaanikwe hadharani kwa kuiba pesa za wahanga wa tetemeko.

Upigaji ni popote mkuu hajalishi ni nani anayesimamia.
 
Ni pesa za wahanga wa tetemeko na hakuna popote ilipoelezwa jinsi pesa zile zilivyotumika miezi miwili sasa. Unakusanya pesa za wahanga wa tetemeko unatakiwa kutoa kiasi kamili cha pesa zilizokusanywa bila kuzitenganisha kwa namna yoyote ile.

HER ZA KUTOKA UK NI KWA AJILI YA KUJENGA SHULE ZAO ZA IHUNGO KAMA HISTORIA YAO.ZINAMAELEKEZO MAALUMU
 
Kagera jamani tuna kosa gano God, yaani Ukimwi umepiga sawa, MV Bukoba ikatufanya yake sawa, tetemeko nalo likatupiga na sasa wenye nguvu zao michango yetu ya kujikimu kidogo yaelekea nayo wanapiga watakavyo Yaani UK peke yake imetoa kama 6.5Bil leo wanasema jumla ya michango yote ni 5bil.
Haya bwana wacha wafanye yao uku Mungu akiwaona
 
Daaaaaaah,hivi kesi ya yule RAS wa kagera na mwenzake ya kufungua akaunti ya kuchangia wahanga wa tetemeko inaendeleaje,isije ikawa waliondolewa ili kuwapisha watu wale vyao kiulaini
 
Serikali hii ni wahuni. Uingereza peke yake ilichangia 6.7 billion na nchi mbali mbali zilichanga pesa nyingi. Michango yote hii iliyokusanywa ni zaidi ya bilioni 15, iweje Serikali iseme pesa zilizochangwa ni shilingi 5.4 billion tu? Zaidi ya bilioni 10 ambazo zinahusisha michango toka nchi mbali mbali zimekwenda wapi? Serikali iweke hadharani list ya nchi na Watanzania mbali mbali ndani na nje ya nchi waliochangia/zilizochangia wahanga wa tetemeko. Msikilizeni Mkuu wa mkoa hapa chini.



Majaliwa katika kuhamaisha michango toka mabalozi mbali mbali nchini na pia Watanzania hakuzungunzia kabisa kwamba michango wanayokusanya itakuwa ni kwa ajili ya taasisi za Serikali tu bali alisema ni misaada ya wahanga wa tetemeko ambao ni Wananchi sasa iweje Serikali ibadili kauli kwenye hili? Serikali katika ofisi ya Waziri Mkuu ina kitengo cha maafa, je kitengo hiki hakina bajeti? Na kama kina bajeti bajeti hiyo imetumika vipi kusaidia wahanga wa tetemeko la ardhi? Au ni kitengo jina tu hakina msaada wowote kwa wahanga wa maafa nchini? Msikilizeni Majaliwa hapa na kauli yake ambayo haikugusia kabisa kwamba michango hiyo itaelekezwa kwenye taasisi za Serikali tu.

 
Serikali isidhulumu hata senti moja ya pesa za wahanga. Watuwekee list ya wote waliochangia ili tuthibitishe ukweli wa kauli yao kwamba pesa zilizochangwa ni 5.4 billion tu kitu ambacho hakina ukweli wowote.
 
Hii awamu ndio inakuja na kasi ya ufisadi na wanatumia nguvu nyingi kuzima watu wasihoji lkn poa siku akitoka tutafunua makaburi, yeye si kasema hayafunui.
 
Jamani tunaelekea wapi?Watu wanaroho za kishetwani hivi.Halafu jumapili mtu anaenda kanisani.[HASHTAG]#Shetaniwarhead[/HASHTAG]
Mkuu hayo makanisa yenyewe ya kitapeli ndio mana wako kimya hawaongei lolote
 
Back
Top Bottom